Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,352
- 9,810
Utopolo wanajifurahisha tu
Hongera sana Chige kwa ufafanuzi uliotukuka,it seems your parents didn't waste their school fees.Na hata kama hivyo vipengele vipo bado kuna mazingira ya kufanya vipengele visifuatwe...
Lazima pawe na kifungu kinachompa haki Chama kutengua hicho kifungu au mkataba mzima!!
Kwa mfano, Yanga wanamtaka Chama na wapo tayari kumlipa mshahara wa $100K, wakati Simba wapo tayari kumlipa ONLY $50K (assuming other things remain constant), hapo huwezi KUMLAZIMISHA Chama akacheze kwenye maslahi duni wakati yeye mpira ni kazi yake!
Kutokana na hilo, anaweza kuvunja mkataba na Berkane na kulipa gharama za kuvunja mkataba, na akishafanya hivyo hicho kipengele kinachombana will not exist anymore!
Suala litabaki kwa Kolo na Berkane... je, kuna kipengele kinachosema something like "ikiwa Chama anavunja mkataba na Berkane ili arudi Tanzania kucheza soka, basi Berkane watakiwa kulipa % ya pesa iliyolipwa kwenye uvunjaji wa mkataba" kama compensation dhidi ya kifungu kilichomtaka Chama asicheze Tanzania except kwa timu yake ya zamani!!
Lakini pamoja na suala la maslahi bora/duni, Chama anaweza kurudi Simba only if he's willing to do so lakini kama HATAKI, huwezi kumlazimisha kwenda kwenye klabu asiyo tayari kuichezeaunless kama upo tayari kumlipa mshahara wakati he doesn't deliver!!
Kwahiyo kitakachotokea ni kuvunja mkataba ili hatimae kifunmgu husika kuwa void!!
Lakini yote kwa yote, kwa jinsi soka la Tanzania lilivyotawala siasa, usikute hata kwa huyo Konde Boy hicho kipengele hakipo!!
Hivi Mashabiki wa Kolo unawabebea mbereko gani yaani kwa mfano hasa baada ya kuzuka taarifa kwamba "kumbe Konde kwenda Al Ahly ilikuwa ni janja tu ya kutafuta njia ya kwenda Yanga kwavile piga ua Kolo wasingekubali kumuuza kwenda Yanga"!
A smart way ni kuwaambia "kuna kipengele kinachomlazimisha akitaka kurudi TZ, basi lazima iwe Simba"... hapo watu watabaki roho kwaaaatu, tena hata kama unasema "kinachomkataza kusajiriwa na Yanga kama anarudi TZ"!!
Kama nyani walivyodanganywa kuhusu MorrisonMbumbumbu wamezoea kudanganywa.
Kelele nyingiiii ujaonyesha comenti yoyote ya chama pia ujaonyesha icho unachosema hakuna mkataba wa kumtaka kurejea Simba Kama akishindwa. Unaishia kujiumauma tu ooh Mimi simba. Aliyekwambia wewe nyani Nani? Mpaka useme wewe Simba?Nakumbuka KEROZENE nilipochangia Uzi wakati Chama alipouzwa nilisema hapa hapa kuwa ile ilikuwa ni Gia tu, ila muda mchache atarudi Tanzania na Kutua Yanga SC.
Kuna sababu Kuu Nne ambazo niliziona wakati nachangia huo Uzi kuwa Chama atatua Yanga SC moja ikiwa ni ukaribu wake na Ridhiwani Kikwete, Haji Manara Mwenyewe, Familia ya Rais Mstaafu Kikwete na Kutoelewana Kwake na Mwekezaji wa Simba SC Mohammed Mo Dewji.
Sijui ni kwanini wana Simba SC wenzangu leo tunakubali Kudanganywa na Uongozi wetu kuwa Chama ana Vipengele vinavyomzuia Kutua Yanga SC wakati kwa Ushahidi uliopo CEO wa Simba SC Barbara Gonzalez aliweka wazi juu ya hilo kwa Mchezaji Luis Jose Miquissone tu na siyo kwa Clatous Chota Chama.
Achilia mbali yote haya ila kama ukiwa Mfuasi ( Follower ) wa Mchezaji Clatous Chota Chama ( hasa Instagram ) kwa jinsi ambavyo huwa 'anakomenti' hasa kwa 'Kejeli' na 'Dharau' pindi Simba SC ilipofungwa na Yanga SC Ngao ya Hisani, ilipofungwa na Jwaneng Galaxy katika Kombe la Klabu Bingwa Afrika na ilivyotoka Sare katika Mechi zake za mwanzo katika NBC Premier League huwezi si tu Kuamini bali hata Kukubali kuwa anarejea / atarejea Simba SC yetu.
KEROZENE nauheshimu sana Uongozi wangu wa Simba SC na naipenda mno Klabu yangu ya Simba SC ila kwa hili la Chama kurejea Simba SC au ana Vipengele vya Kumzuia kutua Yanga SC nalikataa na nasema ni Uwongo wa Mchana kweupe na sijui kwanini Wametudanganya na kwamba ikitokea kweli akatua Yanga SC watatueleza nini.
Counter pekee ambayo Simba SC wanaweza Kuifanya kwa haraka ili Kujiweka salama ni wao pia kufanya 'Umafia' wa Kumsajili Kiungo Khalid Aucho ( ambaye ndiyo Roho ya Yanga SC ) kwa sasa au Kusajili Wachezaji Mahiri zaidi ya Aucho na Bangala na siyo hizi 'porojo' zao wanazotupa na bahati mbaya Mashabiki wengi wa Simba SC wanaamini / wanawaamini.
Kwa Chama kuja tena Simba SC tusahau.
Usipende sana kudakia mambo na kukifanya mjuaji sana mitandaoni. Hapo jamaa katolea mfano na amesema kabisa ni mfano.Mkuu hapo umeandika $100k ukimaanisha nini?
Ulimaanisha Dollar 100,000?
Kwamba mwamba wa lusaka atakua analipwa na GSM 230,000,000 kwa mwezi?
Watu mna utani sana unajua hata ingekuwa $10,000 bado ni utani, maana ni zaidi ya M 22, yanga inawezaje ku afford hizo gharama kwa kumlipa mchezaji mmoja?
Punguza ukali mtani, kwani Aucho mmeshamlipa?Usipende sana kudakia mambo na kukifanya mjuaji sana mitandaoni. Hapo jamaa katolea mfano na amesema kabisa ni mfano.
Na unaongeleaje kuhusu hawa kima wa pori la Utopolo?Mbumbumbu wamezoea kudanganywa.
Hata kama ni mfano, zipo kanuni za kutolea mifano ambazo zinakubalika logically nanmifano yake tunasema ni mifano "hai"Usipende sana kudakia mambo na kukifanya mjuaji sana mitandaoni. Hapo jamaa katolea mfano na amesema kabisa ni mfano.
sanaaaaaKitu kizito