SIMIYU: Samwel Makeja afikishwa mahakamani kwa uhujumu uchumi. Tumpongeze RC Kafulila kwa hili

Jabali la Siasa

JF-Expert Member
Jul 10, 2020
2,476
2,105
KATIBU WA AMCOS WILAYANI MASWA KORTINI KWA UHUJUMU UCHUMI.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) imemfikisha Katibu Wa Chama Cha Msingi cha Ushirika (Amcos)cha Mbaragane katika wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu,Samwel Makeja katika mahakama ya wilaya hiyo kwa makosa mawili ya Uhujumu Uchumi.

Katibu huyo alisomewa leo mashitaka yake yanayomkabili mahakamani hapo ambayo ni Ubadhirifu wa fedha na kuchepusha fedha.

Mwendesha Mashtaka wa Takukuru Albertina Mwigilwa ameieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi,Chirstian Rugumila kuwa Mshtakiwa alitenda makosa hayo Oktoba 4 mwaka 2021 katika Wilaya ya Maswa.

Mwendesha Mashtaka huyo aliendelea kuieleza mahakama kuwa kosa la kwanza ni kwamba mshitakiwa akiwa Katibu wa Amcos ya Mbaragane alifanya ubadhilifu Sh 2,000,000/-ambazo alipaswa kulipia ushuru wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Simiyu(SIMCU) katika musimu wa ununuzi wa pamba wa mwaka 2021/2022.

Amesema kosa hilo ni kinyume ya kifungu cha 28 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura 329 marejeo ya mwaka 2019.

Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa katka kosa la pili mshtakiwa alichepusha fedha hizo kwa madhumuni yake binafsi kinyume na kifungu cha 29 cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa Sura ya 329 marejeo ya Mwaka 2019.

Mshitakiwa mara baada ya kusomewa mashitaka hayo aliyakana na hivyo kesi kupangwa tena Juni 24,mwaka huu ambapo atasomewa hoja za awali kwani upelelezi wa kesi hiyo umeshakamilika.


pia soma USHIRIKA SIMIYU MAHAKAMANI KWA UHUJUMU UCHUMI
 
Mil 2 tu hizo wangetaifisha Mali zake zenye thaman hyo ingetosha.

Mahakaman watapoteza muda na pesa itakayozid pesa anayotuhumiwa.

Na pengine akawabwaga kwa korti pia.
Hii sio awamu ya kulipa pesa kama mlivyoaminishwa, Mahakama ndio waamuzi wala sio DPP,

TULIENI NCHI INYOOKE KWA HAKI
 
Nasema hiviiii, "embu ifike wakati Sasa Serikali iache kuchezea pesa zetu kwa kesi ambazo mwisho wake mtu mmoja t ana simama na kusema Hana haja ya kuendelea na mashtaka, tumeshudia humu kesi nyingi zinatumia gharama kubwa at end of day unaambiwa zimefutwa, so! What for?
 
KATIBU WA AMCOS WILAYANI MASWA KORTINI KWA UHUJUMU UCHUMI.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) imemfikisha Katibu Wa Chama Cha Msingi cha Ushirika (Amcos)cha Mbaragane katika wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu,Samwel Makeja katika mahakama ya wilaya hiyo kwa makosa mawili ya Uhujumu Uchumi.

Katibu huyo alisomewa leo mashitaka yake yanayomkabili mahakamani hapo ambayo ni Ubadhirifu wa fedha na kuchepusha fedha.

Mwendesha Mashtaka wa Takukuru Albertina Mwigilwa ameieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi,Chirstian Rugumila kuwa Mshtakiwa alitenda makosa hayo Oktoba 4 mwaka 2021 katika Wilaya ya Maswa.

Mwendesha Mashtaka huyo aliendelea kuieleza mahakama kuwa kosa la kwanza ni kwamba mshitakiwa akiwa Katibu wa Amcos ya Mbaragane alifanya ubadhilifu Sh 2,000,000/-ambazo alipaswa kulipia ushuru wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Simiyu(SIMCU) katika musimu wa ununuzi wa pamba wa mwaka 2021/2022.

Amesema kosa hilo ni kinyume ya kifungu cha 28 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura 329 marejeo ya mwaka 2019.

Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa katka kosa la pili mshtakiwa alichepusha fedha hizo kwa madhumuni yake binafsi kinyume na kifungu cha 29 cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa Sura ya 329 marejeo ya Mwaka 2019.

Mshitakiwa mara baada ya kusomewa mashitaka hayo aliyakana na hivyo kesi kupangwa tena Juni 24,mwaka huu ambapo atasomewa hoja za awali kwani upelelezi wa kesi hiyo umeshakamilika.


pia soma USHIRIKA SIMIYU MAHAKAMANI KWA UHUJUMU UCHUMI

Chana cha msingi( CCM). Hawa watu ni ndugu
 
Nasema hiviiii,"embu ifike wakati Sasa Serikali iache kuchezea pesa zetu kwa kesi ambazo mwisho wake mtu mmoja t ana simama na kusema Hana haja ya kuendelea na mashtaka,tumeshudia humu kesi nyingi zinatumia gharama kubwa at end of day unaambiwa zimefutwa, so! What for
Bila katiba mpya tutaendelea kulaumiana sana
 
Hiki ni kipindi ukiwa mwizi wa kuku lazima unyooke..., ila wale kina Symbion et al huu ndio wakati wao....

Tunadeal na vidagaa, wale wachelewesha kupatikana kwa Crane kule Bwawa la Nyerere.., tuwape muda....
 
KATIBU WA AMCOS WILAYANI MASWA KORTINI KWA UHUJUMU UCHUMI.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) imemfikisha Katibu Wa Chama Cha Msingi cha Ushirika (Amcos)cha Mbaragane katika wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu,Samwel Makeja katika mahakama ya wilaya hiyo kwa makosa mawili ya Uhujumu Uchumi.

Katibu huyo alisomewa leo mashitaka yake yanayomkabili mahakamani hapo ambayo ni Ubadhirifu wa fedha na kuchepusha fedha.

Mwendesha Mashtaka wa Takukuru Albertina Mwigilwa ameieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi,Chirstian Rugumila kuwa Mshtakiwa alitenda makosa hayo Oktoba 4 mwaka 2021 katika Wilaya ya Maswa.

Mwendesha Mashtaka huyo aliendelea kuieleza mahakama kuwa kosa la kwanza ni kwamba mshitakiwa akiwa Katibu wa Amcos ya Mbaragane alifanya ubadhilifu Sh 2,000,000/-ambazo alipaswa kulipia ushuru wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Simiyu(SIMCU) katika musimu wa ununuzi wa pamba wa mwaka 2021/2022.

Amesema kosa hilo ni kinyume ya kifungu cha 28 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura 329 marejeo ya mwaka 2019.

Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa katka kosa la pili mshtakiwa alichepusha fedha hizo kwa madhumuni yake binafsi kinyume na kifungu cha 29 cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa Sura ya 329 marejeo ya Mwaka 2019.

Mshitakiwa mara baada ya kusomewa mashitaka hayo aliyakana na hivyo kesi kupangwa tena Juni 24,mwaka huu ambapo atasomewa hoja za awali kwani upelelezi wa kesi hiyo umeshakamilika.


pia soma USHIRIKA SIMIYU MAHAKAMANI KWA UHUJUMU UCHUMI
Uhujumu uchumi!Ml 2!atatoka kesho tu huyo.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom