Simbachawene: Toeni gawio kwa wananchi

sir.JAPHET

JF-Expert Member
May 18, 2012
699
133
[h=2][/h] Jumatatu, Septemba 03, 2012 05:16 Na Benjamin Masese, Dar es Salaam

NAIBU Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, ameziagiza halmashauri zote kuhakikisha inatoa kipaumbele cha mgao wa mapato ya uwekezaji wa mafuta, madini na gesi katika maeneo ambako nishati hizo zimegunduliwa na kuchimbwa.

Agizo hilo alilitoa katika Kijiji cha Msimbati mkoani Mtwara jana, wakati alipozungumza na wananchi wa kijiji hicho.

Alisema ni vema wananchi katika maeneo hayo wakapata manufaa ya haraka kwa rasilimali hizo.

Alisema si busara kwa watu wanaoishi na wawekezaji wanaochimba gesi au mafuta katika maeneo yao huku wakiwa hawana maendeleo na huduma muhimu zilizo bora.

“Kuna kodi ambazo hawa wawekezaji wanalipa serikalini na hii kodi kuna kiasi kinarejeshwa katika Serikali za Mitaa ambazo mamlaka zake zinaanzia ngazi ya kijiji, sasa ni vyema wenzetu wa halmashauri mkaweka kipaumbele na mgao wa mapato katika maeneo yaliyo na nishati hiyo, ili nao wanufaike na waone tija ya kuwapo miradi mikubwa katika maeneo yao,” alisema Simbachawene.

Alisema hata migogoro mingi inayotokea kati ya wawekezaji na wenyeji inatokana na wananchi kutoona manufaa ya uwekezaji jambo ambalo ni vema likatatuliwa kwa kuwapa mgao na kuchochea maendeleo kwa kuboresha miundombinu, maji, zahanati na huduma nyingine muhimu.

“Hawa watu wetu hawana tatizo na mipango ya Serikali lakini pengine sisi viongozi na wataalamu wetu tunawachanganya, leo (jana) natoa agizo hili hapa lakini unaweza kukuta utekelezaji wake unachukua muda mrefu au haulitekelezwi,” alisema Simbachawene na kuongeza:

“Sasa wananchi wanapouliza hawajibiwi vizuri, hii si busara hawa watu wasiishie kubugia vumbi la magari ya wawekezaji kwa hiyo ni vema wanufaike na miradi yao.

“Sisemi fedha zote mtakazopata mzigawe kwa maeneo hayo tu, hapana, lakini ninachotaka kuona ni maeneo ya uwekezaji yanapewa kipaumbele.

“Najua kutaibuka mvutano mkubwa kwa madiwani kutaka kila mmoja katika kata yake kupata mgao, lakini hilo si tatizo ila kinachotakiwa ni busara itumike.”

[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
 
Back
Top Bottom