Simbachawene: Kuna Mawaziri walipinga kuhamia Dodoma lakini Magufuli ni 'jiwe' amewahamisha

Queen V

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
776
1,330


Mbunge wa Kibakwe katika Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, George Simbachawene alifanya mahojiano na Radio A FM ya Dodoma alipoalikwa kuzungumzia Builders Expo inayofanyika Jijini Humo.

Katika mahojiano hayo, Simbachawene amemsifia Rais Magufuli kwa kusema unapozungumzia yanayotokea hivi sasa nchini, lazima uanze kwa kumtaja Magufuli. Amesema kuwa Watanzania kwa pamoja tuliwaza tu endapo tungapata Rais wa namna hii na sasa Mungu ametupa tulichokitaka.

"Hii ni awamu ya vitendo na si maneno tu. Nchi yetu ilikuwa haijajengwa vizuri, hatuna miundombinu inayoendana na wakati tulionao wala inayoenda kulingana na maendeleo ya watu. Angalia wenzetu tuliopata uhuru pamoja nao. Tumewasaidia South Africa kupata uhuru wao, tumepata uhuru sawa na Malaysia, Singapore na hatukupata uhuru mbali sana na Ghana, Nigeria lakini wametupita miundombinu." alisema Simbachawene.

"Kutokana na dunia ya sasa kuwa kama kijiji, watu watakimbia nchi na kwenda kuzuri. Tanzania ina amani, watu wakarimu, wapole na rasilimali nyingi lakini tuna miundombinu ya kuendana na hali ilivyo sasa? Hapana!" aliongeza Simbachawene.

Aliendelea kueleza kuwa ni dhahiri tulikuwa tunahitaji Rais wa kujenga nchi na kila awamu huwa na vipaumbele vyake. Amani tunayo, ardhi nzuri tunayo, tuna madini, mbuga za wanyama na tunashangilia. Lakini nchi inajengwa?

"Dodoma squatter zilitaka kuingia. Dar imekuwa squatterized hadi kupanga tena huwezi! Mwanza vivyo hivyo. Kwanini tuna rasilimali nyingi lakini nchi haijengwi interms of miji, mabarabara, reli, airway wakati ni lazima uwe na mambo haya ndio nchi iitwe nchi? Hata ukiwa na nafasi nzuri lazima ujenge nyumba."

"Sasa nchi hii inajengwa kweli kweli. Baada ya miaka 5 au 10 ya Rais Magufuli tutajikuta Tanzania hata kama tunasema Rais sio rafiki wa mtu(Rais hapaswi kuwa rafiki wa mtu, anapaswa kuwa rafiki wa nchi zaidi na si kundi wala mtu) tuna maendeleo makubwa." Alisisitiza.

Aidha kuhusu suala la Serikali kuhamia Dodoma, Simbachawene ambaye alikuwa Waziri TAMISEMI kabla ya kujiuzulu wadhifa anasema iIlikuwa ngumu kukubaliana kuhamia Dodoma kwani baadhi ya Mawaziri walipinga sana walilalamika kuhusu kuacha familia na mali zao zilizopo Dar es Salaam.

Aliendelea kueleza, “Rais Magufuli alisema hiiiiiii mtahamia tu na hii ni process, inapofeli analaumiwa aliyeanzisha lakini inapofaulu ndipo mnajua kuwa kiongozi wenu ni jiwe”

Anasema haukuwepo mpango ulioandikwa ukapitishwa kuhusu Serikali kuhamia Dodoma lakini uamuzi ulishakuwepo toka 1973, miaka 40+ baadae ndo unatekelezwa, hivyo hakukuwa na maana ya kujadiliana na watu.

"Serikali yote iko Dodoma amebaki Rais wetu. Na yeye anaendelea kujenga pale Ikulu ya Chamwino Dodoma hivyo tunaamini Rais anaingia muda si mrefu." alimalizia Simbachawene.
 
Hawa wasomi na wanasiasa waliopata fursa muhimu walipaswa kutulia na kutumia fursa walizopata kuwekeza viwanda nk kwani wana connection za uhakika. Ajabu kutwà kucha kujipendekeza kwa mtukufu wapewe vyeo/ Ajira.Nani kawalaani hawa!?
 
Dodoma haina tija ktk kuinua uchumi wa taifa. Aahamie haraka anaweza asirudi 2020 siasa ni upepo akaishia kuiona kwenye tv
 
Simbachawene toka umekuwa kiongozi katika taifa hili mpaka leo tulitegemea uwe mfano wa kuigwa kwa kuajiri watanzania wasiopungua 1000 kwenye ajira rasmi na wengine deiworker lakini umegeuza siasa ajira sasa..

Ni vyema pia ukapeleka hoja binafsi bunge livunjwe tufanye kazi tuache maneno..
 
Vipi ulipata nafasi ya kuuliza kwanini tunahamia dodoma kwa haraka hivyo?? Namaanisha concrete reason na sio ndoto ya Mwalimu na sababu zake za 1970...
 
Ungesema jiwe haliwezi kuja Dodoma kwani kubeba vote 20 sio mchezo ikiwa na 1.5 tr kwenye sandarusi
 
Ni Wizsra na wafanyakazi wa chini ndo wamehamia Dodoma kwenye mabanda ya mabati, Mawaziri bado wako Dar karivu na mteuzi wao hawataki kumwacha peke take maana atakuwa lonely atakosa wa kumsifia kwa juhudi anazofanya. Mkuu wao alikuwa ahamie, December lakini hadi Leo yuko Dar karibu na mdogo wake. Mleta mada anatafuta kurudishiwa uwaziri ameukosa siku nyingi wenzake wakila bata.
 
Hawa wasomi na wanasiasa waliopata fursa muhimu walipaswa kutulia na kutumia fursa walizopata kuwekeza viwanda nk kwani wana connection za uhakika. Ajabu kutwà kucha kujipendekeza kwa mtukufu wapewe vyeo/ Ajira.Nani kawalaani hawa!?
Wakati mwingine jaribu kuwa unaunga hata mguu hoja.. sio kila kitu unakitizama in negative way..
 
Huwa nashindwa kumtofautisha na musiba
Halafu kwenye ripoti ya mererani huyu alitajwa kusaini mkataba wa kilaghai but yuko huru
 
Hawa wasomi na wanasiasa waliopata fursa muhimu walipaswa kutulia na kutumia fursa walizopata kuwekeza viwanda nk kwani wana connection za uhakika. Ajabu kutwà kucha kujipendekeza kwa mtukufu wapewe vyeo/ Ajira.Nani kawalaani hawa!?
Mtu akisema ukweli wa moyoni mwake kwako wewe ni kujipendekeza?
 
Mbona Na yeye anampinga Mh Rais ujenzi kituo cha afya mtera kwenye majengo waliyoyaacha wachina anataka veta Na ametamba Kwamba hakitajengwa kituo cha afya pamoja Na kuwa Mh Rais alitoa maagizo kijengwe kituo cha afya kabaki kulumbana Na DIWANI wa mtera mpka hawasalimiani none sense ili lijamaa.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom