Simba uso kwa uso na Yanga fainali ya kombe la Mapinduzi

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Sep 11, 2020
69
104
20210111_224146.jpg


Michezo miwili ya nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi imepigwa leo hii katika Dimba la Amani visiwani Zanzibar. Mchezo wa awali uliwakutanisha miamba wa michuano hiyo Azam FC dhidi ya Yanga.

Mchezo huo umemalizika kwa Yanga kufanikiwa kufuzu fainali baada ya dakika tisini za mchezo kumalizika kwa sare ya 1-1 na kulazimika kwenda kwenye hatua ya mikwaju ya penati ambapo Yanga SC wameshinda kwa mikwaju 5-4.

Kwingineko Simba imetinga fainali za mashindano hayo baada ya kuitandika Namungo bao 2-1 .

Fainali ya mashindano hayo itawakutanisha watani wa jadi Simba SC na Yanga CS siku ya tarehe 13 Januari 2021 katika Dimba la Amani Visiwani Zanzibar.

Mara ya mwisho Simba na Yanga kukutana katika fainali za kombe la Mapinduzi ni 2017 ambapo Simba alishinda kwa mikwaju ya penati.
 
1610394461395.png

Timu ya Simba ya Tanzania Bara imefanikiwa kutinga fainali ya michuano ya Mapinduzi baada ya kuichapa timu ya Namungo kwa mabao 2 - 1.

Mabao ya simba yalipatikana kunako kipindi cha kwanza ambapo Mshambuliaji wa Kinyarwanda Medie Kagere alianza kufunga goli la kwanza mnamo dakika ya 6 ya mchezo baada ya kutumia vyema makosa yaliyofanywa na Humud.

Bao la pili la Simba lilipatikana katika dakika ya 40 na Miraji Athumani ambaye alimalizia faulo iliyopigwa na Hassan Dilunga, kwa kufunga goli hili Miraji Athumani amezidi amejikita kileleni katika orodha ya wafungaji bora kwa msimu huu katika michuano ya Mapinduzi,

Bao la kufutia machozi la Namungo lilipatikana kunako dakika ya 87 ambapo liliwekwa kimiani na Stephen Sey aliyemalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Shiza Kichuya.

Kwa matokeo haya Simba anatinga fainali na kwenda kukutana na Mtani wake wa Jadi Yanga ambao pia waliwashinda Azam kwa mikwaju ya penati na kufanikiwa kutinga hatua hiyo.
 
Special tred kuelekea Finally ya Mapinduzi Cup Tambo Pamoja na vijembe.

Miamba miwili ya Tanzania kukutana kweye uwanja wa AMANI Tarehe 13,2021 hapo kesho

Finally zinawakutanisha wawili hawa baada ya Yanga kuwatoa Azam fc kwenye mikwaju ya Penalty


Huku Mnyama mkali akiwafunga NAMUNGO SC magoli 2:1






alikamwe-___CJ6xETYnVOb___-.jpg
 
Kwa Sasa Simba sio level za yanga.
Kilichobakia Sasa ni ule UTANI WA JADI tulioachiwa na mababu zetu.
Ila kwa viwango vya mpira
Hauwezi kuifananisha simba na Yanga.
SIMBA WAPO JUU SANAA.
wamatopeni Sasa mmekua na-kiburi


Group Stage la Sasa limekua cheap tofauti namiaka mitatu ya nyuma kipindi Yanga wanashiliki


Kulikua na stage 3 Sasa hv Sasa hivi Kuna Stage 2 tu


Yanga wakati wote hawatukuwahi kuwekewa timu nyepesi Kama hizi mlizokutana nazo awamu hii


Kwanza niwahanga wa Corona Pili mngekutana na mwarabu yoyote Basi ndio ingekua mwisho wenu
 
Plateau na platinum Ni nyepesi?
wamatopeni Sasa mmekua na-kiburi


Goup Stage la Sasa limekua cheap tofauti namiaka mitatu ya nyuma kipindi Yanga wanashiliki


Kulikua na stage 3 Sasa hv Sasa hivi Kuna Stage 2 tu


Yanga wakati wote hawatukuwahi kuwekewa timu nyepesi Kama hizi mlizokutana nazo awamu hii


Kwanza niwahanga wa Corona Pili mngekutana na mwarabu yoyote Basi ndio ingekua mwisho wenu
 
Plateau na platinum Ni nyepesi?
Plateau amekua mwepesi kwasababu wachezaji wake wengi walikutwa na Corona Pili yule hakua bigwa kwenye nchi yake Bali kipindi Cha ligi yao inasimama kwasababu ya Corona yenye ndio alikua akiongoza ligi.

Platinum ni mwepesi tulimpiga 5 Taifa mwaka 2015 akiwa na wachezaji nyota Kama Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Aubrey Chirwa.

Yamwaka huu mchezaji tishio ni Perfect Chikwende.

wakina Issa Ndala uwezi kufananisha na Kamusoko tulimfunga 5 Taifa timu yakawaida sana ile.

Kwanza yule goaly kipa wa PLATINUM umeekewa kipa chguo la 3 chaguo namba 1 amekutwa na Corona


Mtani uishukuru Corona imekubeba mwaka huu na itaendelea kukubeba kwasababu mwarabu utaenda cheza bila kuwa na mashabiki zile 5 zitapungua, Safari hii
 
Back
Top Bottom