Mbu
JF-Expert Member
- Jan 11, 2007
- 12,753
- 7,844
...haya wadau, tuhabarishane maendeleo, mafanikio, kusua sua hata kuporomoka kwa chama letu, Mnyama Mkali, Simba taifa kubwa!
Wengine sie, ushabiki tuliuanzia miaka hiyo, unaunga foleni ya kuingia national stadiumtangu saa tano asubuhi... vumbi, jua, mbwa na virungu vya FFU, lakini mwisho wa siku aaah... tunatoka tunachekelea kumnywesha Yanga goli 6-0, kipigo mpaka kipa wao Benard Madale aliangua chozi!...
Enzi hizo Kajole Machela akichonga kona hizooooo zinaingia zenyewe golini!... mambo yakoje siku hizi?
Wengine na tujikumbushe!
Wengine sie, ushabiki tuliuanzia miaka hiyo, unaunga foleni ya kuingia national stadiumtangu saa tano asubuhi... vumbi, jua, mbwa na virungu vya FFU, lakini mwisho wa siku aaah... tunatoka tunachekelea kumnywesha Yanga goli 6-0, kipigo mpaka kipa wao Benard Madale aliangua chozi!...
Enzi hizo Kajole Machela akichonga kona hizooooo zinaingia zenyewe golini!... mambo yakoje siku hizi?
Wengine na tujikumbushe!