Simba SC yapokea kichapo kutoka vibonde wa Dubai

utopolo og

JF-Expert Member
Nov 29, 2022
526
1,303
Klabu ya Simba leo imekubali kipigo cha goli 1-0 dhidi ya timu dhaifu ya Al Dhafra katika mchezo wa kirafiki uliomalizika jioni ya Leo.

Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa mazoezi wa timu hiyo ya Al Dhafra ulikosa mvuto kutokana na timu zote kucheza mchezo wa kujilinda zaidi.

Baada ya mchezo huo kocha mkuu wa Simba mbrazili Robertinho amewaahidi wana Simba wasiwe na waiwasi kwani anasuka kikosi cha maangamizi hivyo matokeo ya mchezo huu yasiwavunje moyo..

N.b Al Dhafra inashika mkia ligi ya UAE.

20230113_180505.jpg
20230113_180520.jpg
20230113_180540.jpg
20230113_180530.jpg
 
Maoni ya mdau

Dubai na mpira wa na wapi?

Mbaya zaidi mmegongwa na timu ambayo inagombania kushuka daraja.. Ni timu ambayo imechezesha kikosi cha tatu.

Nilipo sikia tu kocha wetu anampa sifa kedekede KIBU DENIS.. Nikajua hapa hamna kocha..

Amefungwa mapinduzi, na leo amefungwa na timu mbovu huko DUBAI.
Kocha tuachie timu yetu, huna ulicho mzidi MGUNDA.
 
Back
Top Bottom