Simba SC yailaza Ruvu Shooting, yabaki kileleni kwa tofauti ya alama nne

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,777
102,141
Kikosi cha Simba leo kinacheza mchezo wa 18 katika ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Ruvu Shooting uwanja wa Uhuru Dar es Salaam
Nitawaletea kikosi chote cha Mnyama hivi punde. Msimamo wa Ligi ni kama unavyoonesha
========

SUB Dk 52, Simba inafanya mabadiliko ya kwanza kwa kumtoa Mo Ibrahim na kumuingiza Juma Luizio
Dk 49, inafanya shambulizi kali hapa, Bukungu anaachia shuti kali hapa, mpira unamkuta Kotei anaingia vizuri anaachia shuti kali, goal kick
DK 46, mpira unaanza kwa kasi, bado upo katikati hakuna timu iliyofika kwenye lango la mwenzake

MAPUMZIKO
GOOOOOOOOO, Mpira wa krosi safi, Mo Ibrahim anaunganisha kwa shuti kali kabisa hapa
-Kona safi inachongwa hapa, Banda anajitishwa vizuri hapa. Goal kick
-Simba wanaingia vizuri kabisa, Zimbwe anapiga krosi lakini Makwaya anaokoa, konaaa
DAKIKA 3 ZA NYONGEZA

Dk 45 sasa, mpira mwingi unachezwa katikati zaidi
Dk 43, nafasi nyingine kwa Simba, MZamiru anauwahi mpira ukizagaa anaachia shuti kali lakini unapita juuuu
KADI Dk 41, kipa Bidii Hussuein analambwa kadi ya njano kwa kupoteza muda
Dk 40, Simba wanapoteza nafasi nyingine ya wazi, Pastory anashindwa kulenga
KADI Dk 38, Jabir Aziz Stima analambwa kadi ya njano kwa kumrushia daruga Athanas
Dk 36, mkwaju wa adhabu wa Abdi Banda unapigwa na kupaa juu ya lango

DK 32, Zimbwe anaingia vizuri lakini JKT wanakuwa wepesi kuokoa
Dk 29, Shooting wanafanya shambulizi kali hapa, kona. Hii ni kona ya kwanza ya Ruvu leo
Dk 26, Mo Ibarahim anaachia mkwaju mkali lakini Juhudi anadaka kwa ustadi mkubwa hapa
Dk 20, Ruvu wanaonekana kuwa na kasi zaidi na kuanza ksuhambulia kwa kasi zaidi
DK 14, krosi safi, mpira unapigwa na kugonga mwamba. Lakini sasa kipa wa Ruvu yuko chini akitibiwa
Dk 13, Mo Ibra anaingia vizuri hapa ndani ya 18, Ruvu wanaokoa na kuwa konaaaaa
Dk 11, mpira umesimama hapa Kisiga akiwa anatibiwa hapa
Dk 9, Simba wanafanya shambulizi la haraka, Mwanjale anapanda akigongeana na wenzake, anatoa krosi safi kwa Pastory, yeye na nyavu anapaishaa buuuuu
Dk 6, Simba wanaendelea kulisakama lango la Ruvu, Mo Ibra anaingia vizuri na kupiga shuti kali, kipa anadaka mpira unamtoka lakini anawahi
Dk 4, krosi nzuri ya Kichuya, Athanas anaunganisha tena, lakini Shooting wanaokoa
Dk 2, krosi safi ya Zimbwe, Athanas anapiga kichwa hapa lakini ni goal kick
Dk 1, Simba wanaanza kwa kasi wakionekana wamepania kupata bao

Kwa hisani ya Saleh Jembe

 
Iv mapinduz inaanza Lin na kama inawezekan nsaidien ratiba ya siku 2 za mwanzo
 
Kikosi cha Simba leo kinacheza mchezo wa 18 katika ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Ruvu Shooting uwanja wa Uhuru Dar es Salaam
Nitawaletea kikosi chote cha Mnyama hivi punde. Msimamo wa Ligi ni kama unavyoonesha

Msimamo wa ligi ulioweka hapo ni wa uongo. Timu ya wananchi ina Point 40 na sio 37 kama inavyoonyesha kwenye post namba moja.

Either mka update page yenu ta facebook or weka nyingine.
 
Kosi La Maangamizi..

6b8cdf71184f9afb274bc569d5041d30.jpg
 
ruvu jesh kamata huyo mkia rudisha huko porin kwe nafas yake ya tatu alioizoea
 
ruvu jesh kamata huyo mkia rudisha huko porin kwe nafas yake ya tatu alioizoea
Naomba nikupe taarifa: Tangu ligi ya msimu huu imeanza Mnyama ni yupo kileleni tu.. hajawahi shuka. Leo ni lazima ashinde ili aendelee kujiwekea udhibiti wa nafasi yake aliyozoea.
 
Masau Bwire kasema leo anakuja na rungu.Sasa kama anadhani simba ni nyau aje tu! Yaani simba mnyama umue na rungu? Leo ndiyo atajua maana ya NGUVU MOJA.
 
Naomba nikupe taarifa: Tangu ligi ya msimu huu imeanza Mnyama ni yupo kileleni tu.. hajawahi shuka. Leo ni lazima ashinde ili aendelee kujiwekea udhibiti wa nafasi yake aliyozoea.
mkuu leo ni kwata ya kimyakimya mnatakiwa mshushwe huko..masau bwile na jeshi lake hawataki mchezo kabisa
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom