nyama tamu
Member
- Oct 2, 2021
- 42
- 83
Waungana husema sio busara sana kufanya maamuzi ukiwa na furaha au hasira.ila yote kwa yote ni namna tu ya kuiweka timu ktk hali nzuri
Shida ya simba ya juzi sio kuuza watu. Bali game plan mbovu na sub zisizoeleweka
Benchi la ufundi la Yanga limekamilika kila idara! Tuna shida gani sisi mpaka tufikie hatua ya kumchukua kocha wa kukaa jukwaani wakati wa mechi za kimataifa, kutokana na elimu yake ya kuunga unga!!Yanga wamchangamkie kocha huyo
100%Huyu walompa ukocho mkuu binafsi nina mashaka nae ingawa anaweza kuwa na vyeti vya elimu ya kutosha juu ya taaluma yake. Lkn kuwa na cheti na nin unachokifanya kulingana na taaluma yako ni vitu viwili tofauti.
Simuoni kama ni kocha anaweza kuivusha simba na sioni kama ana mbinu zaid za kuisaisia timuz lkn pia sioni kama ni aina ya makocha ambao ana hamasa kwa wachezaji ili kuwahimiza zaidi hasa timu inapokuwa inacheza na ikawa inahitaji matokeo kwa udi na uvumba.
Na hili tuliliona sote wakati wa mechi na wa-Botswana, jamaa alikuwa kasimana tu ni kimya hakuna chochote anachowahimiza wachezaj kufanya hii ilikuwa tofauti na alivyokuwa akifanya kocha wa Wa-Botswana.
Kwa huyu kocha binafsi bado naona pengo.
Timu haiwezi kuvuna pesa kama ingeingia makundi na MUDI kapiga hesabu za kocha mkuu Gomez, kocha wa makipa na kocha wa viungo mishahara yao mikubwa na hawezi kuendesha kwa hasara kiasi hicho. Hivyo kaamua kupitia mlango wa nyuma kumtimua Gomez ambae hata kwenye benchi la ufundi kwenye club bingwa hayupo?? Sasa je Gomez kafukuzwa kwa kosa la mechi ipi?? Why asingefukuzwa kocha ambae alisimama kwa sifa za CAF??
MUDI kwaani ukisema ukweli kwamba unapunguza gharama za kuendesha timu kuna nani angekuhoji , umeuza Konde boy na Chama ukaleta Banda na kanoute kwenye michezo ya wanaume ulidhani utavuna nn?? Muogopeni Mungu wenu. Hata Uchebe ulimtoa kihivyo
Pale kila mtu alikuja kivyake.......kumbukaKocha mkuu huwa anakuja na timu yake, mara nyingi huja na mtaalamu wa viungo, kocha wa makipa, mtaalamu wa saikolojia n.k
Hivyo kocha mkuu akiachia ngazi ni wazi hata jopo lake litaondoka tu...
kocha wa viungo ni Mmisri na sio MtunisiaYeye ni mtunisia na Nabi ni mtunisia huoni ndio alikuwa lango la GSM?
Hukuona wachezaji walikata Moto dakika 45 za mwisho?
Alifeli Sana na ndie alieshauri wachezaji waende kupokea tuzo JKNC
Naunga hojaWachezaji nao wachukuliwe hatua kali, haiwezekani Wawa na Manula wanaangalia tu kama wachumba
We piga kelele, ila ndiyo kashatimuliwa. Kocha amepewa pre season ya kutosha kuliko makocha wote Bongo, kacheza zaidi ya mechi kumi, kashinda mbili tu! Tena kwa papatu papatu! Mbaya zaidi timu inacheza hovyo kuliko kipindi chochote ndani ya miaka minne! Yaani kuondoka wachezaji wawili tu, ndiyo amepata wenge?! Hana mbinu za maana, alikuwa anatembelea gia ya kishingo! Atupishe tu!Hakuna chombo chochote cha Serikali kiliwahi kusema Mo kaweka bil 20 Simba, labda Serikali ya huko uliko. Kilichokuwepo ni tume ya ushindani kupitia utaratibu wa uwekezaji wa club ya Simba ili kujiridhisha kuwa taratibu za ushindani zimefuatwa ili baada ya hapo mchakato uendelee.
Huu si ushuzi mkubwa.......Kwa kauli aliyoitoa ni Mo Dewji baada ya simba kufungwa nilijua tu Gomes hawezi kupona
Nakumbuka kabla hajawa muwekezaji simba alitoa kauli kama hiyo Omog ambaye kwa sasa ni kocha wa Mtibwa Sugar nae akafungasha
Bado Ole Guna Sosha sasa ili niwe na amani ya moyo.
View attachment 1987249
Hoja ya kujadili ni USALITI.Huu ndio mwanzo wa migogoro, kuna kila dalili timu itaanza ku-under perform
Adel Zrane aliachwa na Pierre Lechantre.Kocha mkuu huwa anakuja na timu yake, mara nyingi huja na mtaalamu wa viungo, kocha wa makipa, mtaalamu wa saikolojia n.k
Hivyo kocha mkuu akiachia ngazi ni wazi hata jopo lake litaondoka tu...
Adel Zrane ana PhD kwenye sport science anakosaje vigezo ?Nimemsikia Ibrahim masud maestro akidai "huyo kocha wa viungo na magolikipa pia walikosa vigezo (sifa/ elimu) na mechi yao ya mwisho kuruhusiwa kuwepo kwenye benchi ni ile ya Dodoma jiji" .