Simba SC kuelekea Derby na Yanga SC naona mnalirudia tena Kosa lile lile ambalo niliwaonya huko nyuma, tukifungwa mtatukoma Mashabiki

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
Magori, Salim, Kocha Matola, Somo na Mkuu wa Itifaki Makoye ni mara ngapi mnataka niwe nawakumbusha hili ambalo huwa mnalipuuza kama siyo Kulisahau kila tukicheza na Yanga SC na Wanatufunga?

Nilishawaambia kuwa hata kama Timu yetu sasa inaendeshwa Kisasa (Professionally) ila kwa Utamaduni wa hizi Timu kila zinapokutana Mambo ya Kiutamaduni ( Kiuchawi ) ni Muhimu na Wajibu kufanyika iwe isiwe.

Hii tabia ya kila Simba SC inapokaribia Kucheza na Yanga SC basi Timu ikijiandaa kule Bunju (Uwanjani Kwetu) Mashabiki wa kila aina wanaruhusiwa Kuingia Kiutamaduni ( Kiuchawi ) ni Hatari sana Kwetu.

Simba SC hivi mnavyofanya Mazoezi hayo ya Wazi kujiandaa na Mchezo wa Derby na Yanga SC huku mnaruhusu Mashabiki (Watu) wa kila aina waingie mnajiamini nini?

Hamjui kuwa hata Yanga SC nao hufanya Umafia kwa Kutuma Watu wao (Wachawi) kuja Kutuangalia, Kutusoma na hata Kufanya Uchawi (Unyangindo) pale pale Bunju na kufanya tufanye vibaya na hata Watufunge Mechi yao?

Leo tena mmerudia lile lile mlilolifanya katika ile Mechi ambayo Zawadi Mauya alinifanya nilale Saa 2 Kamili Usiku na hata Kusahau Kula na Kuvua Viatu mpaka Asubuhi nilipoamka kwa Kutufunga lile Goli lake tamu la Muwa wa maana uliombabatiza Shomary Kapombe na ukajaa Kimiani.

Tafadhali Simba SC hebu kuanzia Kesho Jumatano hadi Ijumaa fanyeni Mazoezi pamoja na Maandalizi yenu Kimya Kimya tena huku mkiweka Ulinzi Mkali na Kuzuia Watu ( Mashabiki ) Kuja Bunju (Mo Simba Arena) ili Kuzuia (Kuondokana) na hizi Hujuma ambazo zinaweza Kujirudia na hatimaye Jumamosi Yanga SC wakatulaza mapema tena.

Na nisiwaficheni kuwa Yanga SC kuelekea Mechi yao na Sisi huwa wanajiandaa vyema kwa Umafia wa ndani na nje ya Uwanja huku Wakiroga sana na Kujificha kabisa wasijulikane waliko na hata kama ikitokea Watu kujua waliko bado huzuia kabisa Kuingia ( Kwenda ) kutizama Maandalizi (Mazoezi) yao.

Tafadhali tuacheni Kujiamini tutaumia. Na ikitokea tukafungwa na Yanga SC kwa kutokuwa Waangalifu nao Kimkakati na Kimafia hasa Kipindi hiki tunaenda Kucheza nao Walahi na Hakyamungu Sisi akina Mightier hatutowaelewa na Viongozi mtatukoma kwa Vagi ( Fujo ) letu kwani mtakuwa mmezembea Ushauri wetu Sisi Watu wa Mpira hasa na Watoto wa Mjini vile vile.

Hata akina Asante Kotoko FC na Hearts of Oak ( Ghana ), Al Ahly na Zamalek ( Egypt ), Kaizer Chiefs FC na Orlando Pirates ( South Africa ), AFC Leopards na Gor Mahia ( Kenya ), River Plate FC na Boca Junior ( Argentina ) na Flamengo na Corinthians au Palmeiras na Sao Paolo ( Brazil ) nao kuelekea Derbies zao hizo huongeza Umakini wa ndani na nje ya Uwanja.

Mightier nikisema Jambo mlizingatie..!!
 
Walikuwa wapi kutumia uchawi wao Nigeria,hizo imani za kishirikina hazina nafasi ndugu,wekeza kwenye professionalism kuliko kwenye ushirikina Mkuu sumaku haiwezi nasa kwenye ubao,mchawi atakuweza pale wewe nae ni mchawi na nguvu zako za kishirikina zikizidiwa!
 
Ushirikina hauna nafas katka maswala haya unatakiwa kuwa wa kimataifa kivitendo
 
Kunapokuwa na Kombe uwanjani, Simba huwa hawana dharau. Watafanya kama walivyofanya kule Kigoma.

Pia kuna tetesi zinasema Simba tayari imeshatoa kafala lililoambatana na Kiongozi wao kufariki kwa Covid + Tunguli. Hivyo Yanga itapoteza mechi zote za mwaka huu. Kazi ilishafanyika kitambo.
 
Kwa kikosi cha Simba cha mwaka huu, Yanga hata Waroge kwa waganga wachawi milioni 40, tutawafunga tu.

Labda wachezaji wa Simba waidharau hiyo mechi.

Uwezo wa wachezaji wa Simba msimu huu ni mkubwa mara kumi ya uwezo wa wachezaji wa Yanga wa msimu huu.

Simba hatuna haja ya kuroga ni kuongeza bidii tu ya mazoezi.

Kama wameshindwa kuwaroga Rivers United wakabaki wanarukaruka tu kama kuku wa broira kwao kwa Mkapa.

Ni kwamba hawana jipya tena ondoeni wasiwasi.
 
Nilivyoona ni wewe wala sijasoma ujinga wako.
Umezoea kuandika majungu na umbea.
Juzi ulisema Yanga wamewahonga Rivers bilions ili washinde mchezo wao.
Lao umekuja na hekaya nyingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani unajua fika kuwa Mightier Mimi naandika Maujinga yangu 24/7 hapa lakini bado tu huachi Kunifuatilia na Kunisoma nikisema kuwa husumbuliwi tu na Upumbavu mwingi ulionao bali pia unaugua Uwendawazimu nitakuwa nakosea?

Cc: kukumsela
 
Hiyo mechi inachezwa jumangapi?

Maana hilo la siku huwa ni hatua namba moja ya kubashiri matokeo ya mechi ya hawa wanga wa K'koo...
 
Mchawi hafungiwi mlango wewe gentamicin.

Tunaujua Simba mnaloga Sana Sana , hata makombe hayo manne mliiloga yanga mechi za nje .

Na hata hili la clabu bingwa Africa Simba mliiloga yanga Kwa kuwapa chakula walipokuwa pre season na ninyi mlivunja kwenda misri pre season yenu ili mkawalishe madawa wachezaji WA yanga siyo kwamba hatujui Ila huu ndiyo mwisho wenu
 
Mchawi hafungiwi mlango wewe gentamicin.

Tunaujua Simba mnaloga Sana Sana , hata makombe hayo manne mliiloga yanga mechi za nje ...
Kama kuroga ni rahisi hivyo, Kwa nini na nyie msiroge? Mpira ungekuwa na hayo unayofikiria, Nigeria angechukua makombe yote duniani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom