Simba naona mnakuja kivingine rage mbaya weweeeeeeeeeeee!!hapo watatulia tu

NAPITA

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
5,076
2,243
…
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Mhe; Ismail Aden Rage, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa aliyekuwa msanii maarufu wa muziki na filamu, Hussein Ramadhani Mkiety, maarufu kwa jina la Sharo Milionea, kilichotokea jana usiku mkoani Tanga.
Kwa niaba ya klabu ya Simba na kwa niaba yake binafsi, Mwenyekiti anapenda kutuma salamu za pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki wote wa marehemu kutokana na msiba huu mkubwa sana si kwao pekee bali kwa taifa zima la Tanzania.
Sharo Milionea hakuwa msanii wa kawaida. Yeye ni miongoni mwa kizazi kipya cha vijana wa Kitanzania walioamua kutafuta maisha kwa kutumia vipaji walivyopewa na Mungu. Yeye alijitumbukiza zaidi katika uchekeshaji na baadaye akaonyesha uwezo mkubwa katika fani ya muziki.
Sharo alikuwa maarufu kiasi kwamba makampuni makubwa yalikuwa yameanza kumtumia kwenye matangazo yao ya kibiashara. Hii ilionyesha kwamba makampuni yalibaini faida itakayopatikana kwao kwa kumtumia msanii huyu ambaye bado alikuwa na heshima kubwa kwenye jamii kutokana na haiba yake na uwezo wake kwenye kazi alizokuwa akifanya.
Msiba huu umekuwa pigo kubwa kwa tasnia ya filamu ambayo bado inaomboleza vifo vya wasanii kama Steven Kanumba, Mlopelo na John Steven Maganga, waliofariki dunia mwaka huu pia.
"Ifahamike kwamba Sharo Milionea alikuwa miongoni mwa wasanii wa Kitanzania waliotuma maombi Simba ya kutaka kushiriki kwenye mchakato wa kutengeneza wimbo rasmi wa klabu ya Simba. Yeye alikuwa miongoni mwa wasanii waliokuwa wakiumizwa na ukweli kwamba klabu kama Simba inashindwa kufanya biashara ya kuuza nyimbo zake ilhali wanunuaji wapo," alisema Rage.
Kwa klabu ya Simba, namna pekee ya kumuenzi marehemu ni kufanyia kazi mambo ambayo alikuwa akitushauri kwenye eneo la biashara. Ni matumaini yetu kwamba iwapo tutafanya lile alilokuwa akitushauri, atakuwa mwenye amani huko alikotangulia mbele ya haki.
Rage amewaomba wasanii wa tasnia ya filamu na muziki kuwa watulivu na wenye subra kwenye kipindi hiki kigumu kwao. Kila kitu katika maisha ya wanadamu kinapangwa na Mwenyezi Mungu na ndiyo maana Waswahili wana msemo kuwa Kazi ya Mungu haina makosa.
Mola na ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Hussein Ramadhani Mkeity (Sharo Milionea).
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC.
 
Kichwa kikikosa akili mwili upo taabuni

Niaje KubwaJinga?
Hebu nipe tathmini yako kisoka, wakati huu ambapo uongozi wa Munyama una mengi ya kuwaeleza washabiki wake; ombwe la uongozi, sakata la familia ya Petit Mafisango, ugomvi kati ya Rage (sio uongozi) na tawi la Mpira Pesa, matokeo mabovu kwenye ligi na kadhalika, kuna haja ya kujipendekeza kutuma salamu za rambirambi kwa marehemu Hussein? Basis waliyoitoa eti Sharo alikuwa anataka kufanya nyimbo yao ya timu, kwa hiyo wanatuma rambirambi kwa mshauri wao wa kibiashara.
Ptuuuuuh...
Kwa maoni yangu huku ni kujibaraguza, kutafuta huruma-au kuwasahaulisha washabiki wa Simba wasizingatie matatizo ya klabu kwa sasa, mchanga wa macho huu.
Sijasahau uwanja wa Bunju ambao kiuhalisia haupo...
 
Atajaribu kila njia sijui kama kifo cha wale waliopata ajali huko sumbawanga hawa wahusu pia Naomba kamwaga atuambie marehumu alikuwa mshauri wa uchumi ndani ya SSC?
 
Soka limewashinda sasa wanajifanya waombolezaji wazuri.

Kama mnaujua uchungu wa kufiwa, mbona mlitafuna rambi rambi za Mafisango?
 
Ningemuelewa kama wangemtenda vyema Mafisango other wise ni usanii tu, inamaana msiba wa mtunga nyimbo ya club unauma sana kuliko mchezaji? Tuachie Simba yetu tupumue.
 
Ningemuelewa kama wangemtenda vyema Mafisango other wise ni usanii tu, inamaana msiba wa mtunga nyimbo ya club unauma sana kuliko mchezaji? Tuachie Simba yetu tupumue.
vipi simba sasa mnataka kufungua tawi la ze comedy?nacheka kweli kweli hapa nilipo,yanga wanaenda uturuki mmoja wenu aombe lifti kwenye dege linalowapeleka angalao atasimama muifuate ile ramani ya uwanja.
 
eee?tungeni wimbo huu ehee tumekosa vyoteeeeee,wakati tulikua na vyoteeeee,sasa itakuaajeeeee,na shari katutokaaaaaa,sijui tutawaelezajeeeeee, wanachama na wapenziiiiiiiiii,ule uwanjaaaaaaa,nakelvin yondaniiiiiiii,na mbuyu twiteeeeeeee sijui itakuajeeeeeeeeee..........blah blah blahhhhhhhhhhhh.........halafu sijuiiiiiiiiiii......itakuajeeeeeeeee
 
Niaje KubwaJinga?
Hebu nipe tathmini yako kisoka, wakati huu ambapo uongozi wa Munyama una mengi ya kuwaeleza washabiki wake; ombwe la uongozi, sakata la familia ya Petit Mafisango, ugomvi kati ya Rage (sio uongozi) na tawi la Mpira Pesa, matokeo mabovu kwenye ligi na kadhalika, kuna haja ya kujipendekeza kutuma salamu za rambirambi kwa marehemu Hussein? Basis waliyoitoa eti Sharo alikuwa anataka kufanya nyimbo yao ya timu, kwa hiyo wanatuma rambirambi kwa mshauri wao wa kibiashara.
Ptuuuuuh...
Kwa maoni yangu huku ni kujibaraguza, kutafuta huruma-au kuwasahaulisha washabiki wa Simba wasizingatie matatizo ya klabu kwa sasa, mchanga wa macho huu.
Sijasahau uwanja wa Bunju ambao kiuhalisia haupo...


Heshima mbele Mphamvu...
Ishu hapo ni ndogo mno.
Rage anataka kuiongoza timu kama vile anaongoza jimbo.
Anatumbukiza Siasa kwenye maswala ya Soka.
Anatumbukiza bla bla za siasa katika mambo ya Soka.
Hayo mambo ya kwenda kuandika waraka mrefu kama huo wakati timu iko katika wakati mgumu ni mbinu ya kuwasahaulisha wanachama wa Simba zile jazba walizonazo juu ya uozo wa timu yao uliojitokeza hivi karibuni.

Tumeshashuhudia wanasiasa wa Tanzania kujificha nyuma ya tukio flani ili kukwepa majukumu waliyonayo.

Mfano wanasiasa kuushadadia msiba wa Marehemu Kanumba wakati wana mengi ya kujieleza na kuyajibu kwa wananchi waliowachagua.

So wanachama wa Simba amkeni, msidanganywe na hio ujinga.
Mnachezewa akili na huyo Baniani
 
Wapenda sanaa wa bongo tumeguswa na kuumizwa na kifo cha Sharo milionea....Lakini Rage apeleke rambirambi za Patrick Mafisango kwanza, hatujasahau walivyodhurumu zile rambirambi za mkongoman wa tu! R.I.P MUTESA PATRICK MAFISANGO....R.I.P SHAROMILIONEA
 
Heshima mbele Mphamvu...
Ishu hapo ni ndogo mno.
Rage anataka kuiongoza timu kama vile anaongoza jimbo.
Anatumbukiza Siasa kwenye maswala ya Soka.
Anatumbukiza bla bla za siasa katika mambo ya Soka.
Hayo mambo ya kwenda kuandika waraka mrefu kama huo wakati timu iko katika wakati mgumu ni mbinu ya kuwasahaulisha wanachama wa Simba zile jazba walizonazo juu ya uozo wa timu yao uliojitokeza hivi karibuni.

Tumeshashuhudia wanasiasa wa Tanzania kujificha nyuma ya tukio flani ili kukwepa majukumu waliyonayo.

Mfano wanasiasa kuushadadia msiba wa Marehemu Kanumba wakati wana mengi ya kujieleza na kuyajibu kwa wananchi waliowachagua.

So wanachama wa Simba amkeni, msidanganywe na hio ujinga.
Mnachezewa akili na huyo Baniani

Wakati uchaguzi wa Simba unafanyika miaka mitatu nyuma, niliwashangaa wanachama wa Simba kumchagua ex-mwenyekiti wa Moro United kuwa mwenyekiti wao mpya, lau kama ingekuwa ni nafasi ya kuajiriwa isingenishangaza, ila ilikuwa nafasi ya kuchaguliwa ambayo kwa uzoefu wangu mdogo inawahusu wanachama tu.
Sasa Ismail Aden alikuwa mwanachama wa timu mbili kwa wakati mmoja?
Kujificha nyuma ya matukio huyu ex-konvict hakuanza leo, mwaka ule aliporejesha umeme jengo la Simba ilikuwa ndio habari ya mjini, wakati kiuhalisia sio big issue kivile, mara ngapi watu huwa tunarudisha umeme majumbani kwetu?
Unazi ndo umetufikisha hapa, tunapokutana washabiki wa Sunche na Kapeto na kuanza kubishana kila mtu anatetea upande wake hata kama maji matupu, na hapo ndipo washabiki wa Simba wanapolazimika kumbeba mtu ambaye amewahi kukaa jela kwa tuhuma za ubadhilifu ndani ya soka.
Shall we make it? Chambilecha Hamza Kassongo...
 
Wakati uchaguzi wa Simba unafanyika miaka mitatu nyuma, niliwashangaa wanachama wa Simba kumchagua ex-mwenyekiti wa Moro United kuwa mwenyekiti wao mpya, lau kama ingekuwa ni nafasi ya kuajiriwa isingenishangaza, ila ilikuwa nafasi ya kuchaguliwa ambayo kwa uzoefu wangu mdogo inawahusu wanachama tu.
Sasa Ismail Aden alikuwa mwanachama wa timu mbili kwa wakati mmoja?
Kujificha nyuma ya matukio huyu ex-konvict hakuanza leo, mwaka ule aliporejesha umeme jengo la Simba ilikuwa ndio habari ya mjini, wakati kiuhalisia sio big issue kivile, mara ngapi watu huwa tunarudisha umeme majumbani kwetu?
Unazi ndo umetufikisha hapa, tunapokutana washabiki wa Sunche na Kapeto na kuanza kubishana kila mtu anatetea upande wake hata kama maji matupu, na hapo ndipo washabiki wa Simba wanapolazimika kumbeba mtu ambaye amewahi kukaa jela kwa tuhuma za ubadhilifu ndani ya soka.
Shall we make it? Chambilecha Hamza Kassongo...


Na huyohuyo mla Mirungi alisemaje vile endapo Yondani atachezea Yanga?
 
Na huyohuyo mla Mirungi alisemaje vile endapo Yondani atachezea Yanga?

Alitishia kuishtaki Yanga na TFF kwa kumsaini mchezaji usiku tena kwa kumuiba kambini.
Hata kwenye sakata la Twite, nilishangaa kwanini wanachama wa Lunyasi walishindwa kumwajibisha mwenyekiti wao kwa kutumia resources za timu kwenda Rwanda kusajali mchezaji kwa magumashi, badala yake wakaungana nae kuwalaumu kina Bin Kleb kwa kuwachezea rafu.
Leo hii Mpira Pesa wametumia haki yao kikatiba kuita mkutano halali, wametokea wanachama walioshikwa masikio kumuunga mkono Rage.
 
Alitishia kuishtaki Yanga na TFF kwa kumsaini mchezaji usiku tena kwa kumuiba kambini.
Hata kwenye sakata la Twite, nilishangaa kwanini wanachama wa Lunyasi walishindwa kumwajibisha mwenyekiti wao kwa kutumia resources za timu kwenda Rwanda kusajali mchezaji kwa magumashi, badala yake wakaungana nae kuwalaumu kina Bin Kleb kwa kuwachezea rafu.
Leo hii Mpira Pesa wametumia haki yao kikatiba kuita mkutano halali, wametokea wanachama walioshikwa masikio kumuunga mkono Rage.


Wanasema the end justfy the means...
Kazi kwao
 
attachment.php
 
Whats the context?
Ni kwamba hata maneno aliyoyatamka Rage au Simba kuhusu misiba ya wasanii au wachezaji yawe mabaya au mazuri namna gani, at the end of the day kazi kuu ya klabu ya soka ni kuwa na timu inayoshinda mechi muhimu na vikombe muhimu, na mfano ni huo wa 5 - 0. That's the context !
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom