Simba na Yanga zitaweza ushindani wa Afrika? Al Ahly imemuajiri kocha wa Mamelodi, Mosimane kwa mshahara wa Dola za Kimarekani 120,000 kwa mwezi

Mimi hoja yangu ni kubahatisha. Hiyo Simba iliyomtoa Zamalek mwaka 2003 ilimtoa Zamelek kwavile Simba walikuwa na uwezo mkubwa kuliko Zamalek?
ili Simba ionekane haikubahatisha toa takwimu ya kufanya vizuri kila msimu unaofuatia baada ya kufikia hatua fulani ya mafanikio.

Kuhusu usajili, Simba ilifanya usajili na kisha kutokana na aina ya usajili uliofanywa tukaambiwa safari hii Simba itafika hatua ya nusu fainali.
Wachezaji wa kimataifa
1. Tairone Santos da Silva
2.Gerson Fraga
3.Wilker da Silva
4.Shiboub
5.Deo Kanda
6. Kahata
1. Hiyo UD Songo kumtoa Simba ina uwezo kuliko Simba?

2. Unajua maana ya kuboresha kikosi kweli wewe..? ANATOKA
Okwi
Gyan
Kwasi
Kotei
Zana
Halafu unasema waliboresha kikosi kweli uko sawa wewe?

Timu inayocheza MECHI 10 ZA CAF INASHINDA MECHI 6 unasema Imebahatisha..

TIMU 8 BORA AFRIKA amebahatisha? (kichwani uko sawa wewe)

Tumia akili toa UYANGA Kichwani kubali kuwa Simba alikuwa vizuri.
 
1.) Kwahiyo unakataa kuwa kwenye mpira hakuna bahati kuwa upande wa timu?
2. Unaposema Mpira ni mistake, timu ikifanya mistake haiondoi ubora wake. Unaweza kuniambia ni kwanini msimu wa nyuma hakukuwa na mistake hizo hadi mkafika hatua ya robo fainali?

3) Unaposema Mpira ni mistake, na timu ikiadhibiwa kwa kufanya mistake haiondoi timu iliyoadhibiwa ubora wao. Hapo hauoni kwa kauli hii inaonesha kabisa hii timu iliyoiadhibu timu iliyobora, imebahatisha tu kumfunga?
wewe ndio wale waliosema Leicester City kubeba EPL alibahatisha..
 
1. Hiyo UD Songo kumtoa Simba ina uwezo kuliko Simba?

2. Unajua maana ya kuboresha kikosi kweli wewe..? ANATOKA
Okwi
Gyan
Kwasi
Kotei
Zana
Halafu unasema waliboresha kikosi kweli uko sawa wewe?
kwahiyo kuondoka kwa hao wachezaji na kisha kusajili wengine ilikuwa sio kuboresha kikosi bali ni Kufanyaje?
Kwahiyo ukiondoa baadhi ya wachezaji ambao wanaonekana sio sehemu ya mipango mipya ya mwalimu ama timu, na kusajili wengine unaona watafaa, kumbe inakuwa sio kuboresha kikosi bali inaitwaje?
 
wewe ndio wale waliosema Leicester City kubeba EPL alibahatisha..
Kama hakubatisha kwanini msimu uliopita wasilitwae kwa kutumia kanuni, mikakati, misingi ile ile walioifanya hadi wakachukua kombe?
 
Timu inayocheza MECHI 10 ZA CAF INASHINDA MECHI 6 unasema Imebahatisha..

TIMU 8 BORA AFRIKA amebahatisha? (kichwani uko sawa wewe)

Tumia akili toa UYANGA Kichwani kubali kuwa Simba alikuwa vizuri.
Sasa kama hamkubahatisha kwanini hakufikia tena hatua ile ile mliyofika msimu wa 2018/2019?
 
Kama hakubatisha kwanini msimu uliopita wasilitwae kwa kutumia kanuni, mikakati, misingi ile ile walioifanya hadi wakachukua kombe?
Kombe ni mashindano.. yeye aliwini kwa kupata point nyingi kuliko wenzie wakati huo.

Unaposema mbona hajabeba tena.. Soka sio kunya mkuu, ubora unapanda na kushuka.

Kubali Alikuwa bora wakati huo sio kubahatisha.
 
Mimi naona UD Songo alibahatisha hakuwa na uwezo. Haya wewe niambie je UD Songo anauwezo kuliko Simba ndio maana kamtoa au ilibahatisha?
Kwa RANK ya ubora Ud songo yupo chini kwa Simba.

Hizi timu zimecheza mechi 2 (home+away) unatolewa unasema Wamebahatisha?
we uliona Ud songo amezidiwa kipi kwenye mechi zile?
 
Sasa kama hamkubahatisha kwanini hakufikia tena hatua ile ile mliyofika msimu wa 2018/2019?
Waambie Yanga wabahatishe..

Timu ndogo kuitoa kubwa sio bahati pekee bila uwezo wa kumudu mchezo.

Mpira ni dakika 90 usipozitumia vzr unatolewa (huo ndio mpira)
 
Kwa RANK ya ubora Ud songo yupo chini kwa Simba.

Hizi timu zimecheza mechi 2 (home+away) unatolewa unasema Wamebahatisha?
we uliona Ud songo amezidiwa kipi kwenye mechi zile?
Mbona hujibu swali langu je UD Songo anauwezo kuliko Simba ndio maana kamtoa?
 
Mimi naona UD Songo alibahatisha hakuwa na uwezo. Haya wewe niambie je UD Songo anauwezo kuliko Simba ndio maana kamtoa au ilibahatisha?
Man Utd anapofungwa na Palace huwezi kusema Palace wamebahatisha ila Man wamezidiwa mbinu. (huo ndio uwezo sio bahati)

Timu ikuzuie kuifunga, halafu yenyewe ivunje ngome yako ikufunge halafu useme bahati bila uwezo.

nini maana ya MPIRA ni dakika 90..?

Kumbe timu ndogo ikishinda ni bahati? (nilikuwa sijui)
Mbona timu zetu zinasajili wachezaji wao (wanaobahatisha?)
 
Waambie Yanga wabahatishe..

Timu ndogo kuitoa kubwa sio bahati pekee bila uwezo wa kumudu mchezo.

Mpira ni dakika 90 usipozitumia vzr unatolewa (huo ndio mpira)
Unataka kusema Simba ya 2019/2020 ilishuka uwezo na ndio maana ikatolewa mapema?
 
Unataka kusema Simba ya 2019/2020 ilishuka uwezo na ndio maana ikatolewa mapema?
Ndio.. ni moja ya sababu.

waliondoka wachezaji muhimu kwenye timu na kuleta wageni ambao hawakufiti kama walioondoka.

Lakini haina maana kwamba wasingevuruga kikosi wangefika tena makundi au Robo.. Soka sio (a e i o u)
 
kwahiyo kuondoka kwa hao wachezaji na kisha kusajili wengine ilikuwa sio kuboresha kikosi bali ni Kufanyaje?
Kwahiyo ukiondoa baadhi ya wachezaji ambao wanaonekana sio sehemu ya mipango mipya ya mwalimu ama timu, na kusajili wengine unaona watafaa, kumbe inakuwa sio kuboresha kikosi bali inaitwaje?
Mkuu kuboresha timu ni kuongeza nguvu ya wachezaji wazuri kama au zaidi ya waliopo.

Huwezi kumuacha MAKAMBO na TAMBWE.. Halafu ukaleta MOLINGA na YIKPE ukasema unaboresha timu.
 
Mkuu kuboresha timu ni kuongeza nguvu ya wachezaji wazuri kama au zaidi ya waliopo.

Huwezi kumuacha MAKAMBO na TAMBWE.. Halafu ukaleta MOLINGA na YIKPE ukasema unaboresha timu.

Hapo unazungumza hivyo wakati tayari Molinga na Yikpe wameshachezea Yanga takribani mechi kadhaa na kuonekana ni wabovu. Lakini kumbuka wakati Simba inafanya usajili walijua kwa asilimia mia kuwa hao waliowasajili ni bora zaidi kuliko waliowaacha na ndio kauli ya kuboresha kikosi inapokuja. Na ndio maana tambo zikaanza kuwa safari hii kikosi sijui cha bilioni ngapi sijui tutafika nusu fainali klabu bingwa.
 
Ndio.. ni moja ya sababu.

waliondoka wachezaji muhimu kwenye timu na kuleta wageni ambao hawakufiti kama walioondoka.

Lakini haina maana kwamba wasingevuruga kikosi wangefika tena makundi au Robo.. Soka sio (a e i o u)

Soka sio a e i o u bali ni nini mkuu?
 
Hapo unazungumza hivyo wakati tayari Molinga na Yikpe wameshachezea Yanga takribani mechi kadhaa na kuonekana ni wabovu. Lakini kumbuka wakati Simba inafanya usajili walijua kwa asilimia mia kuwa hao waliowasajili ni bora zaidi kuliko waliowaacha na ndio kauli ya kuboresha kikosi inapokuja. Na ndio maana tambo zikaanza kuwa safari hii kikosi sijui cha bilioni ngapi sijui tutafika nusu fainali klabu bingwa.
Usizungumzie Tambo mkuu.. ongelea uhalisia. Hao wa asilimia 100 Umewaona uwezo wao au je wako sawa na walioachwa?

Okwi na Kotei VS Fraga na Kanda...

Wachezaji ambao wamekupa mafanikio tena kikosi cha kwanza huwezi kuwaacha ili ulete wachezaji wa majaribio ambao sio kikosi cha kwanza..

Itawachukua muda kuja kukupa mafanikio mpaka uwape muda.
 
Back
Top Bottom