Simba na yanga ni kama ccm na chadema

AMARIDONG

JF-Expert Member
Jun 24, 2010
2,502
180
VIGOGO wa soka hapa nchini Simba na Yanga za jijini Dar es Salaam leo zinatarajiwa kuanza kujinoa kwa ajili ya kukabili mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara unaoanza kutimua vumbi Januari 15 mwakani.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam, maofisa habari wa klabu hizo walithibitisha timu zao kuanza programu za mazoezi leo kwa kuanzia na gym.
Ofisa Habari wa mabingwa watetezi Simba, Clifford Mario Ndimbo, alisema, mazoezi yatakayoanza leo yatakuwa chini ya kocha msaidizi Amri Said ‘Jap Stam’, huku akisubiriwa kocha mkuu, Mzambia Patrick Phiri.
Kwa upande wake, Ofisa Habari wa Yanga Louis Sendeu, alisema, pia nao wataanza na gym chini ya kocha mkuu, Mserbia Kostadin Papic huku wakiwasubiri nyota wao walioko timu za taifa za bara na visiwani ambao wanashiriki michuano ya Chalenji inayoendelea jijini Dar es Salaam.
Klabu hizo zimeimarisha vikosi vyao wakati wa dirisha dogo kwa kusajili nyota wawili kila moja, ambapo Simba imemnyakua mshambuliaji Ali Ahmed Shiboli kutoka KMKM ya Zanzibar na kumrejesha kundini beki wake Meshack Abel aliyekuwa kwa mkopo African Lyon huku Yanga ikimtwaa Davies Mwape na Juma Seif Kijiko kutoka JKT Ruvu ya Pwani.
 
vigogo wa soka hapa nchini simba na yanga za jijini dar es salaam leo zinatarajiwa kuanza kujinoa kwa ajili ya kukabili mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka tanzania bara unaoanza kutimua vumbi januari 15 mwakani.
wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini dar es salaam, maofisa habari wa klabu hizo walithibitisha timu zao kuanza programu za mazoezi leo kwa kuanzia na gym.
ofisa habari wa mabingwa watetezi simba, clifford mario ndimbo, alisema, mazoezi yatakayoanza leo yatakuwa chini ya kocha msaidizi amri said ‘jap stam', huku akisubiriwa kocha mkuu, mzambia patrick phiri.
kwa upande wake, ofisa habari wa yanga louis sendeu, alisema, pia nao wataanza na gym chini ya kocha mkuu, mserbia kostadin papic huku wakiwasubiri nyota wao walioko timu za taifa za bara na visiwani ambao wanashiriki michuano ya chalenji inayoendelea jijini dar es salaam.
klabu hizo zimeimarisha vikosi vyao wakati wa dirisha dogo kwa kusajili nyota wawili kila moja, ambapo simba imemnyakua mshambuliaji ali ahmed shiboli kutoka kmkm ya zanzibar na kumrejesha kundini beki wake meshack abel aliyekuwa kwa mkopo african lyon huku yanga ikimtwaa davies mwape na juma seif kijiko kutoka jkt ruvu ya pwani.

heeeee mbona haieleweki kicha na mkia viko kushoto kulia?????????
 
amekurupuka, na hajui kuwasilisha mada yake

isipokuwa wakati wa mechi ya simba na yanga katika uwanja wa ccm kirumba oktoba 16 mwaka huu, kwenye jukwaa la yanga kulikuwa na bendera nyingi za ccm na kwenye jukwaa la simba kulikuwa na bendera nafikiri moja ya chadema

hakuna mahusiano ya siasa na michezo especially baada ya kuingia kwa mfumo wa vyama vingi, hata hivyo yanga hawajaacha mchezo wao wa kijinga wa kushangilia cc, ccm kwenye nyakati kadhaa kadhaaa hivyo labda yale mahusiano ya yanga na ccm bado yanaendelea na kwa kuwa katika bendera ya chadema kuna rangi nyekundu na nyeupe mbali ya ile ya blue, then washabiki wa simba walio chadema watakuwa na furaha zaidi kupeperusha bendera ya chadema kuliko yule wa yanga aliye chadema au wa simba aliye ccm
 
Back
Top Bottom