Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,885
- 6,885
Chelsea baada ya kutambua kuwa uwezo wa kuchukua ubingwa nchini Uingereza imeshindikana, wakaamua kupoteza hata nafasi za kuingia nne bora ingawa wangekazana wengeweza. Walichoamua ni kuelekeza nguvu zao zote kwenye ubingwa wa Ulaya, na kweli wamefanikiwa. Kwani wapinzani wao walikuwa na mawili ya kugombea ubingwa nchini mwao na kugombea ubingwa wa ulaya wakati huo huo. Chelsea wamefanikiwa kuchukua ubingwa huo kwa sababu nguvu zote walielekeza huko, ndio maana siku za karibuni wameweza kufungwa au kutoka sare na timu dhaifu za ligi ambazo hazikuwa na nguvu ya kuifunga Chelsea.
Simba licha ya kuvimba vichwa kuchukua ubingwa mapema, lakini walivyokomalia Yanga kwa nguvu zote nilishangaa wakati huo huo wameshajihakikishia ubingwa. Mchezo wa mwisho haukuwa na umuhimu kwa simba ila kutimiza ratiba tu. Wangeweza kuchezesha zaidi kikosi cha pili ili kuwapumzisha kikosi cha kwanza kwa ajili ya mchezo mgumu wa Sudan. Tatizo la wazi ni kwamba soka letu si la kisayansi, ila ni la mfumo wa mitaani kutambiana.