Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,001
- 9,866
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, David Silinde amesema serikali inatoa elimu bila ada sio elimu bure hivyo wazazi washiriki katika kutoa michango mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya shule.
Aidha Waziri wa Elimu, Joyce Ndalichako amesema waraka wa serikali namba 3 wa 2016 ulieleza ushirikishwaji wa wazazi katika maendeleo ya shule lakini shule hairuhusiwi kufukuza watoto kwa sababu ya michango ya maendeleo ya shule.
Majibu hayo yalikuja baada ya Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Aida Khenani ambaye alisema kwa sasa michango inaendelea ila kwa kibali maalumu cha kudai michango hiyo.
Aidha Waziri wa Elimu, Joyce Ndalichako amesema waraka wa serikali namba 3 wa 2016 ulieleza ushirikishwaji wa wazazi katika maendeleo ya shule lakini shule hairuhusiwi kufukuza watoto kwa sababu ya michango ya maendeleo ya shule.
Majibu hayo yalikuja baada ya Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Aida Khenani ambaye alisema kwa sasa michango inaendelea ila kwa kibali maalumu cha kudai michango hiyo.