Silaha Putin aliyojisifia inaweza kupiga popote duniani imefeli vibaya kwenye majaribio

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,769
Mapema mwaka huu Raisi Putin wa Russia alitamba kwamba sasa Urusi ina silaha (missile) ambayo inaweza kupiga sehemu yeyote duniani. Ukweli ni kwamba wakati Putin akifanya majigambo haya, silaha hiyo ilikuwa bado inatengenezwa na mainjinia wa Urusi.

Silaha hiyo imetengenezwa kwa namna ambayo inapopigwa inaanza kuendeshwa kwa kutumia mafuta ya petroli, na baadaye inaendeshwa kwa nguvu za nyuklia.

Wanasiasa wa Kremlin wa Urusi walilazimisha mainjinia waanze kufanya majaribio ya siala hiyo ili kuonyesha ulimwengu nguvu za kijeshi za Urusi. Japo mainjinia walisema walihitaji muda zaidi ili kuikamilisha silaha hiyo, waliambiwa lazima wafanye majaribio sasa. Walipofanya majaribio silaha hiyo ilifeli kwa kuwa ilifanikiwa kwenda kilometa 35 tu kabla ya kulipuka na kuanguka chini. Mara nyingine ilienda kama kilomita 8 na kufeli.

Hili limekuwa jambo la kufedhehesha kwa Urusi.

Sasa wanamazingira wanakuja juu kuuliza ikiwa silaha hizo zilifeli na kulipuka sehemu ambazo hazikuwa zimepangwa kulipuka, ni nini athari za mionzi ya nyuklia sehemu zilipoangukia?

Source: MSN

Putin claimed a new nuclear missile had unlimited range – but it flew only 22 miles in its most successful test yet
 
Nilichomuelewa mleta mada ni kwamba, Putin alipokuwa anatamba, aliongea kana kwamba tayari hiyo silaha tayari ipo, lakini nyuma ya pazia ilikua haijakamilika bado.Na majaribio ya kuelekea utimilifu wake yameshindikana kwa sasa.

Hilola mazingira linaweza kuzua mjadala na kusababisha ukomo wa kuendelea na huo mradi. Itategemea na watakavyotoa maelezo ya madhara yaliyosababishwa na anguko lahichi chombo kwenye eneo lisilokusudiwa.
 
Nilichomuelewa mleta mada ni kwamba, Putin alipokuwa anatamba, aliongea kana kwamba tayari hiyo silaha tayari ipo, lakini nyuma ya pazia ilikua haijakamilika bado.Na majaribio ya kuelekea utimilifu wake yameshindikana kwa sasa.

Hilola mazingira linaweza kuzua mjadala na kusababisha ukomo wa kuendelea na huo mradi. Itategemea na watakavyotoa maelezo ya madhara yaliyosababishwa na anguko lahichi chombo kwenye eneo lisilokusudiwa.
Huyo ataendelea tu mana ni kama kiduku tu akiamua jambo kaamua
 
Sasa umeshasema silaha za majaribio, sasa hapo cha kufedhehesha na cha ajabu ni kipi

Kama tu unajua Kiingereza;

"Russian President Vladimir Putin bragged earlier this year that his country had a new nuclear-powered missile with unlimited range – but it has yet to perform a successful test over multiple attempts, according to sources with direct knowledge of a U.S. intelligence report on the weapons program"
 
Nilichomuelewa mleta mada ni kwamba, Putin alipokuwa anatamba, aliongea kana kwamba tayari hiyo silaha tayari ipo, lakini nyuma ya pazia ilikua haijakamilika bado.Na majaribio ya kuelekea utimilifu wake yameshindikana kwa sasa.

Hilola mazingira linaweza kuzua mjadala na kusababisha ukomo wa kuendelea na huo mradi. Itategemea na watakavyotoa maelezo ya madhara yaliyosababishwa na anguko lahichi chombo kwenye eneo lisilokusudiwa.
Ahsante Mkuu. Unajua ndio maana mkiwa shule kunakuwa na mtu wa kwanza hadi wa mwisho darasani. Kuna watu ni wagumu kuelewa na wepesi kubisha na kukosoa!
 
Majaribio hufeli unajifunza

"Mapema mwaka huu Raisi Putin wa Russia alitamba kwamba sasa Urusi ina silaha (missile) ambayo inaweza kupiga sehemu yeyote duniani. Ukweli ni kwamba wakati Putin akifanya majigambo haya, silaha hiyo ilikuwa bado inatengenezwa na mainjinia wa Urusi"

Hakusema wanafanya majaribio.
 
"Mapema mwaka huu Raisi Putin wa Russia alitamba kwamba sasa Urusi ina silaha (missile) ambayo inaweza kupiga sehemu yeyote duniani. Ukweli ni kwamba wakati Putin akifanya majigambo haya, silaha hiyo ilikuwa bado inatengenezwa na mainjinia wa Urusi"

Hakusema wanafanya majaribio.
Haya mambo wanayajua wenyewe tu kwa mimi ninavyoona maana kinachosemwaga au kuonekana hadharani kinakuaga ni tofauti na mambo ya uhalisia wana hesabu zao wenyewe wanazijua haya mambo mengine yanakuaga tu yakupima upepo wa kidiplomasia
 
Kama tu unajua Kiingereza;

"Russian President Vladimir Putin bragged earlier this year that his country had a new nuclear-powered missile with unlimited range – but it has yet to perform a successful test over multiple attempts, according to sources with direct knowledge of a U.S. intelligence report on the weapons program"
Kama tu unajua Kiingereza, KWA HIO UNANIFANYA MM NI MWANACCM SIJUI KIENGEREZA, utaitwa mchochezi bro hahahahahahah
 
Haya mambo wanayajua wenyewe tu kwa mimi ninavyoona maana kinachosemwaga au kuonekana hadharani kinakuaga ni tofauti na mambo ya uhalisia wana hesabu zao wenyewe wanazijua haya mambo mengine yanakuaga tu yakupima upepo wa kidiplomasia
chezea Mrussi wewe hawezi fanya hayo hata siku moja km 35......Marekani wangechekelea dunia nzima ingejua
 
Back
Top Bottom