Sikuwa mjinga, niliamini niko sahihi, leo Ndugai amejibu

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
SIKUWA MJINGA, NILIAMINI NIKO SAHIHI, LEO NDUGAI AMEJIBU.

Na Yericko Nyerere

Job Ndugai mfuasi kindakindaki wa hayati John Magufuli aliyeapa kumuongeza muda wa kutawala Tanzania, ananirejesha nyuma miaka miwili iliyopita 22 December 2019 nilipoandika Makala nikipinga hotuba ya Rais Magufuli akikataa kuendelea na ujenzi wa Mradi ya Bandari ya Bagamoyo, nilipinga hoja alizozijenga Rais ili kuualalisha katazo lake juu ya mradi husika.

Nilieleza wazi kwamba, Kuna mambo katika nchi yanahitaji uchunguzi kubaini pengine kuna hujuma katika taifa, hii inatokana na michakato mingi muhimu ya kichumi na kijamii imekuwa ikiishia njiani na kuliacha taifa katika hasara kubwa. Hii ni hujuma inahitaji mwarobaini kulitibu.

Mifano ya michakato ambayo kwamiaka mingi imeikuwa ikiishia njiani ni kama vile sekta ya nishati ambapo uzalishaji wa umeme limekuwa jambo linalotumiwa kama mchakato wakuzuka na kufa kwa miaka mingi sana tangu mwaka 1994 ilipokuja kitu kinaitwa umeme wa dharula kuokoa taifa (IPTL), ikafata michakato mingi yenye kuumiza taifa na haikufanikiwa hadi tukafika kuchimba Gesi mtwara tukapoteza mabilioni, gesi hadi Kinyerezi, kufumba na kufumbua mradi umetelekezwa sasa tunaimba mradi wa Bonde la Rufiji. Twende tuendelee..

Serikali ya awamu ya nne ilianzisha mradi wa kimkakati kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara duniani, mradi huu ilikuwa ni kujenga bandari ya Bagamoyo kwa ubia kati ya China na Omani wenye thamani ya dola bilioni 10, Serikali ya Tanzania katika mradi huu ilikuwa haiweki pesa yoyote isipokuwa ardhi na raslimali zingine, huku Uchina na Omani wakiweka mtaji na utaalamu.

Kwamjibu wa mapendekezo ya mkataba wa awali wa mradi huo, ni kwamba kungeundwa chombo maalumu cha nchi zote tatu ambacho kingekusanya mapato ya mradi huu na kusimamia gawio la pande zote, hii inamaana kwamba TRA ya Tanzania isingekuwa na haki ya kukusanya mapato moja kwa moja kutoka katika mradi badala yake ingekusanya gawio toka kwa chombo cha wabia kinachokusanya mapato ya mradi wa nchi zote tatu.

Huu ni moja ya mradi ambo kimsingi ulikuwa umeitangazia dunia vita vya kiuchumi toka kwa washindani wetu ambao ni nchi jirani na zinazotuzunguka. Kwakuwa Afrika yote ingepokelea bidhaa zake toka ulimwenguni hadi Bagamoyo, sawa na ilivyo Dubai ambayo ndio mlango wa Afrika kupokelea bidhaa zake.

Afrika inaingiza bidhaa toka Uchina kwa 88.8% na kiwango cha 98% ya bidhaa hizo zinapita Dubai. Hivyo kujengwa kwa Bandari ya Bagamoyo kungefunga nyia ya Dubai na bidhaa zote za Afrika kutoka China kupita Bagamoyo. Hii inamaana kwamba uchumi wa Dubai na Marekani ambayo ndio mdau mkuu ungemegwa. Mradi huu ulikuwa ndio msingi halisi wa kuanzisha mradi wa reli ya kisasa ya SGR, bila Bandari itakayozalisha mizigo kwa wingi SGR itakuwa ni kwakubeba abiria tu badala ya mizigo.

Serikali ya awamu ya tano katika hali ya kustaajabisha imeutupilia mbali mradi huo kwakutoa sababu ambazo hazina nguvu na zingine za kushangaza sana, mimi naitafsiri kama ni hujuma kwa taifa, izingatiwe kuwa tayari taifa lilishaingia gharama kubwa kuanzia kwenye upembuzi yakinifu, na kusaini mikataba ya awali. Kitendo cha kusitisha katika hatua hii ni kulitia hasara taifa. Moja ya hoja zilizotolewa na rais kama sababu ni kwamba masharti ya wabia nikuwa TRA hairuhusiwi kukusanya mapato, hoja hii ya Rais alikuwa sahihi lakini bahati mbaya alishindwa kufafanua wazi sababu za TRA kutokuwa miusanya mapato ya ubia. Pengine hili Rais alidanganywa.

Pili rais alisema kuwa masharti ya wabia nikuwa Tanzania hairuhusiwi kuendeleza bandari zake zingine. Hoja hii nayo inautata mwingi sana, Bandari zingine zote ziko kwaajili ya ndani, na mradi huu ulikuwa kwa shughuli za kimataifa. Sasa hoja ya kuwa tusikarabati bandari zetu zilizopo ni hoja isiyo na mashiko, Hili inawezekana kabisa Rais hakuambiwa ukweli.

Hoja ya Tatu aliyoitumia Rais Magufuli kukataa mradi ule, ilikuwa kwamba, wabia wanataka wapewe umiliki wa ardhi kwa miaka 99. Hili si la mwekezaji bali la sheria zetu ambazo zinatoa uwekezaji katika ardhi kwa miaka 33 hadi 99. Sasa hoja hii haiwezi kuwa kwa wabia wawili tu kati ya watatu ikiwemo Tanzania yenyewe. Hili nalo kuna uwezekano watu waliamua kumpotosha rais wetu.

Chakusikitisha kwa nchi yangu, Katikati ya mvutano wetu na wabia hadi Rais Magufuli kusitisha mradi, Rais wa Msumbiji Philip Nyusi kwakutumia majasusi wake waliotanda kila pembe ya Afrika na kwingineko, amefanya mageuzi makubwa, amechukua wazo lilelile ambalo limekataliwa Dar es Salaam na wajuvi, amekwenda kulisimika katika Bandari ya Nacala kwakuingia ubia na Wachina kwa Dola bilioni 5 za Kimarekani, hii ni Bandari inayotarajiwa kuwa lango kuu la kiuchumi Afrika.

Wakati hili halijapoa, Mwaka 2017 tu juzi Tanzania tulipowazuia wazungu wasisafirishe madini ghafi na makinikia yao, tuliimba nyimbo kwamba Tanzania itajenga vinu vya kuchenjulia madini hapahapa, na nyimbo ziliimbwa kisiasa zikaitikiwa kishabiki kwa beti za kinafiki kwelikweli. Leo nyimbo haziimbwi, hakuna anayejua kama viwanda vimeshajengwa au laa na hakuna anayehoji hilo kwakuwa ukihojihoji tu basi ukinusurika sana utaenda mochwari au Ubelgiji, tulishazoe vimbunga kwamba vitavuma na kutulia.

Lakini huku sisi tukiwa tumebadili nyimbo sasa tunaimba nyimbo za Standard Gauge nk, Rwanda kwakutumia majasusi wao waliotanda kila pembe ya Dunia, imelichukua wazo lilelile la Tanzania imejenga vinu vya kuchenjulia madini na inatarajiwa kwamba hadi 2024 Rwanda iwe ndio nchi ya kwanza barani Afrika inayosafirisha madini kwa wingi nje ya Afrika. Kumbuka na elewa Rwanda sio mzalishaji wa Dhabu, Almasi wala chochote kiitwacho madini isipokuwa kwenye kilimo cha chai na kahawa huko. Hivyo anategemea viwanda vyake vipokee madini ghafi toka Tanzania, Kongo, Zambia akusanye kodi yake na kugonga muhuri wa madini unaotambulisha kuwa ni madini toka Rwanda nk. Sisi tumelala. Siasa inanguvu bana.

Kwa maoni yangu ninafiki kuna tatizo kubwa kwenye eneo la Ujasusi katika nchi yetu, hasa ujasusi wa Kiuchumi, na hili ndilo lilikuwa msingi wa mimi kuandika Kitabu changu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi. Michakato mingi ya kiuchumi katika nchi hii imekuwa haina mafaa ama inaliacha taifa katika makovu makubwa yasiyozibika. Hii inazaa uhalali wa kuhitaji mageuzi makubwa katika Idara ya Ujasusi nchini kuanzia kwenye ideology, sheria, misingi, kanuni, na mambo anuai ndani ya idara ya ujasusi nchini.

Ujasusi kwa nchi zilizoendelea kama China, Israel, Urusi na Marekani, unafanywa na watu ambao ni smart na wanajengwa kuwa smart ili kuweza kumudu ugumu wa kazi hiyo na kuifanya kazi hiyo kwa mafanikio makubwa. Majasusi katika nchi hizo hawapewi kazi kwasababu ya ujomba ujomba na kujuana.

Ni kweli asilimia kubwa ya information's zenye thamani katika kazi ya ujasusi huwa zinaletwa na "human intelligence" badala ya magazeti, TV na source nyingine za habari.

Kwa maana hiyo basi ni lazima kuwe na watu competent ambao wana uwezo wa kukusanya habari za kijasusi ili tuweze kupata information's za maana na kujenga uwezo wa kuzifanyia kazi informations hizo. Imagine wakati ule wa vita baridi jinsi Directorate 16 ya KGB ilivyoweza kufanya kazi ya kununua sensitive navy information za USA na kuweza kutengeneza balance ya navy fleet bila USA kugundua kwa miaka 17 kupitia kwa Johny Walker junior!

Tanzania kwenye balozi zetu kuna majasusi. Lakini ni majasusi wa aina gani? Wale wa kujua kuongea kifaransa na kireno na lugha nyingine za mataifa ya nje bila upeo wowote wa Technologia? Kama kuna sehemu tunakosea basi ndio hapo. Majasusi wengi wa Tanzania au tunaoambiwa kuwa ni watu wa system wengi katika tafsiri ya kijasusi ni "informers". Ujasusu kama ujasusi hapa Tanzania ni kama hakuna. Usalama wa Taifa au TISS/UWT msingi wao uliounda chombo hiki ni "power defensive", yaani wajibu mkubwa unaelekezwa kwenye kumonitor mwelekeo wa kisiasa Tanzania hasa kuwadhibiti oppositions na elements zote za upinzani na assasinations za elements zozote zinazoonekana kuwa against na himaya ya CCM.

Idara ya Usalama wa Taifa hii tuliyonayo leo ilianzishwa na CCM 1997 kutoka katika muundo wa kijamaa wa chama kimoja, hii ni baada ya kuanzishwa mfumo wa vyama vingi, kwa hiyo bado unaiserve CCM kwanza kisha Taifa linatafsiriwa salama kupitia matokeo ya uimara wa ccm, kama yakifanyika mageuzi ya kimuundo, kisheria, kikanuni na kisera, uimara wa Taifa hautatafsiriwa kupitia uimara wa ccm madarakani, na mambo mengi tunayolalamikia sasa juu ya taifa hayatakuwepo tena. In simple words, taswira kubwa inayoonekana yauhakika ni kazi yao ya kulinda viongozi, kusafiri na viongozi na kuilinda CCM.

Nje ya mambo ya Ujasusi wa Kiuchumi ambao mimi ndio ninaoupigania siku zote uongoze nchi, Naweza kusema Tanzania tuko vizuri katika Ujasusi wa kidola kuliko nchi yoyote pengine Afrika nzima, Hili limefanya kuimeza idara na kuonekana siasa ambazo ndio zinabeba taswira kubwa ya ubora ama udhaifu wa ujasusi Tanzania, Eneo la Ujasusi wa Kidola Tanzania kuna vitengo vya wachapakazi hasa kiko jeshini.., kitengo cha ujasusi ambacho kilikuwa kiko free from politics party ni CMI (central military intelligence). Lakini bahati mbaya muundo na aina ya uongozi wa Magufuli ulikiingiza katika siasa pale kilipofanywa kuwa decision maker wa nchi, lakini upande wa foreign assets ndio wazuri sana wako bize kukusanya taarifa hatarishi dhidi ya nchi...

Kwa undani zaidi Soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.
IMG_20210408_230306_873.jpg
 
Huo mradi wa Bagamoyo as long as yupo Mchina, sisi wabongo tunapaswa kuutazama mkataba kwa upya neno hadi neno...wale wapumbavu macho madogo wana hila kuliko mwanadamu yoyote juu ya uso wa nchi...
 
SIKUWA MJINGA, NILIAMINI NIKO SAHIHI, LEO NDUGAI AMEJIBU.

Na Yericko Nyerere

Job Ndugai mfuasi kindakindaki wa hayati John Magufuli aliyeapa kumuongeza muda wa kutawala Tanzania, ananirejesha nyuma miaka miwili iliyopita 22 December 2019 nilipoandika Makala nikipinga hotuba ya Rais Magufuli akikataa kuendelea na ujenzi wa Mradi ya Bandari ya Bagamoyo, nilipinga hoja alizozijenga Rais ili kuualalisha katazo lake juu ya mradi husika...
Si waseme hili ni dili lao la kuuza nchi na kupewa pipi kana kwamba hawatakufa. Hapa naona unafiki, woga na upumbavu wa kupita kiasi.
 
SIKUWA MJINGA, NILIAMINI NIKO SAHIHI, LEO NDUGAI AMEJIBU.

Na Yericko Nyerere

Job Ndugai mfuasi kindakindaki wa hayati John Magufuli aliyeapa kumuongeza muda wa kutawala Tanzania, ananirejesha nyuma miaka miwili iliyopita 22 December 2019 nilipoandika Makala nikipinga hotuba ya Rais Magufuli akikataa kuendelea na ujenzi wa Mradi ya Bandari ya Bagamoyo, nilipinga hoja alizozijenga Rais ili kuualalisha katazo lake juu ya mradi husika...
Huu mradi tunajua ni wa kipumbafu!
 
SIKUWA MJINGA, NILIAMINI NIKO SAHIHI, LEO NDUGAI AMEJIBU.

Na Yericko Nyerere

Job Ndugai mfuasi kindakindaki wa hayati John Magufuli aliyeapa kumuongeza muda wa kutawala Tanzania, ananirejesha nyuma miaka miwili iliyopita 22 December 2019 nilipoandika Makala nikipinga hotuba ya Rais Magufuli akikataa kuendelea na ujenzi wa Mradi ya Bandari ya Bagamoyo, nilipinga hoja alizozijenga Rais ili kuualalisha katazo lake juu ya mradi husika...
Kwanini wa Msumbiji uwe 5m na wetu use 10.

Pili kwanini sisi wenyewe tusi fiance hata ikiwa kwa kukopa ili tuwe hutu kukusanya kodi yetu, kama mtu wa nje anaweza kuwejeza fedha zote hizo na atapata faida licha ya sisi kutupatia kiasi .

Tatu ikiwa mradi utafeli kama wa Sirilanka nini madhara yake kwa Taifa, tutaweka waziri wa Fedha wa kichina au Raisi tutakodi from China
 
Huu mradi uwekwe wazi sio kwamba Hayati alikuwa mbaya completely hapana kuna vitu visipowekwa wazi vitaleta UTATA huko mbeleni.

Hatukatai maendeleo lakini yaje yale tutakayokubaliana nayo na kwasasa ni vyema Mh. Rais akurudisha vichwa ndani ya bunge kutoka upinzani ili vikapeane changamoto na wasomi wetu wa CCM ndani ya bunge tusonge mbele.
 
Kauli hii ya Ndugai ni tosha kumuundia tume ya kumchunguza; kubadirika kwa msimamo wake kunatia shaka sio bure!!! Kama alivyosema mwendazake ule mradi wa bandari ya Bagamoyo ni wa KIJINGA; hakuna mtu mwenye akili timamu na mzalendo ambale angekubaliana na yale masharti!!! Pengine uwe mgogo kama Ndugai.
 
Nakipataje hicho kitabu na kinauzwaje
Karibu mkuu

OFA YA KARUME DAY inaisha saa sita usiku

Kitabu cha "MTU BAADA YA MTU" 20,000/= Badala ya 80,000

Kitabu cha UJASUSI kwa 20,000/= Badala ya 80,000

Lpia kwa:

TigoPesa 0715865544
M-Pesa 0755865544
Airtel Money 0788887887
HaloPesa 0624452045
(Yericko Nyerere)

Tuma majina yako na ulipo

Kwa Dar ni free delivery

Nje ya Dar nauli ni 8,000/=
 
Karibu mkuu

OFA YA KARUME DAY inaisha saa sita usiku

Kitabu cha "MTU BAADA YA MTU" 20,000/= Badala ya 80,000

Kitabu cha UJASUSI kwa 20,000/= Badala ya 80,000

Lpia kwa:

TigoPesa 0715865544
M-Pesa 0755865544
Airtel Money 0788887887
HaloPesa 0624452045
(Yericko Nyerere)

Tuma majina yako na ulipo

Kwa Dar ni free delivery

Nje ya Dar nauli ni 8,000/=
Lipia tangazo
 
Kama ambavyo awamu ya tano ilificha ficha taarifa na ninyi ndivyo mnavyokazana kuficha ficha mikataba ya huo mradi, mkataba upelekwe sehemu husika, upitiwe upya na wananchi tuambiwe ABC, ili siku yakianza kwenda ndivyo sivyo tujue wakumshika shati.

Msitumie hizi kelele za kukosolewa kwa awamu ya tano kupitisha mambo yenu binafsi. Hii nchi ni yetu sote.
 
Mkuu umeusoma huo mkataba? Kama umeusoma uweke hapa.
La sivyo hakuna maneno yatakayoshawishi kwamba mkataba ni mzuri au hapana bila watu kuusoma na kufanya tathmini.
 
SIKUWA MJINGA, NILIAMINI NIKO SAHIHI, LEO NDUGAI AMEJIBU.

Na Yericko Nyerere

Job Ndugai mfuasi kindakindaki wa hayati John Magufuli aliyeapa kumuongeza muda wa kutawala Tanzania, ananirejesha nyuma miaka miwili iliyopita 22 December 2019 nilipoandika Makala nikipinga hotuba ya Rais Magufuli akikataa kuendelea na ujenzi wa Mradi ya Bandari ya Bagamoyo, nilipinga hoja alizozijenga Rais ili kuualalisha katazo lake juu ya mradi husika.

Nilieleza wazi kwamba, Kuna mambo katika nchi yanahitaji uchunguzi kubaini pengine kuna hujuma katika taifa, hii inatokana na michakato mingi muhimu ya kichumi na kijamii imekuwa ikiishia njiani na kuliacha taifa katika hasara kubwa. Hii ni hujuma inahitaji mwarobaini kulitibu.

Mifano ya michakato ambayo kwamiaka mingi imeikuwa ikiishia njiani ni kama vile sekta ya nishati ambapo uzalishaji wa umeme limekuwa jambo linalotumiwa kama mchakato wakuzuka na kufa kwa miaka mingi sana tangu mwaka 1994 ilipokuja kitu kinaitwa umeme wa dharula kuokoa taifa (IPTL), ikafata michakato mingi yenye kuumiza taifa na haikufanikiwa hadi tukafika kuchimba Gesi mtwara tukapoteza mabilioni, gesi hadi Kinyerezi, kufumba na kufumbua mradi umetelekezwa sasa tunaimba mradi wa Bonde la Rufiji. Twende tuendelee..

Serikali ya awamu ya nne ilianzisha mradi wa kimkakati kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara duniani, mradi huu ilikuwa ni kujenga bandari ya Bagamoyo kwa ubia kati ya China na Omani wenye thamani ya dola bilioni 10, Serikali ya Tanzania katika mradi huu ilikuwa haiweki pesa yoyote isipokuwa ardhi na raslimali zingine, huku Uchina na Omani wakiweka mtaji na utaalamu.

Kwamjibu wa mapendekezo ya mkataba wa awali wa mradi huo, ni kwamba kungeundwa chombo maalumu cha nchi zote tatu ambacho kingekusanya mapato ya mradi huu na kusimamia gawio la pande zote, hii inamaana kwamba TRA ya Tanzania isingekuwa na haki ya kukusanya mapato moja kwa moja kutoka katika mradi badala yake ingekusanya gawio toka kwa chombo cha wabia kinachokusanya mapato ya mradi wa nchi zote tatu.

Huu ni moja ya mradi ambo kimsingi ulikuwa umeitangazia dunia vita vya kiuchumi toka kwa washindani wetu ambao ni nchi jirani na zinazotuzunguka. Kwakuwa Afrika yote ingepokelea bidhaa zake toka ulimwenguni hadi Bagamoyo, sawa na ilivyo Dubai ambayo ndio mlango wa Afrika kupokelea bidhaa zake.

Afrika inaingiza bidhaa toka Uchina kwa 88.8% na kiwango cha 98% ya bidhaa hizo zinapita Dubai. Hivyo kujengwa kwa Bandari ya Bagamoyo kungefunga nyia ya Dubai na bidhaa zote za Afrika kutoka China kupita Bagamoyo. Hii inamaana kwamba uchumi wa Dubai na Marekani ambayo ndio mdau mkuu ungemegwa. Mradi huu ulikuwa ndio msingi halisi wa kuanzisha mradi wa reli ya kisasa ya SGR, bila Bandari itakayozalisha mizigo kwa wingi SGR itakuwa ni kwakubeba abiria tu badala ya mizigo.

Serikali ya awamu ya tano katika hali ya kustaajabisha imeutupilia mbali mradi huo kwakutoa sababu ambazo hazina nguvu na zingine za kushangaza sana, mimi naitafsiri kama ni hujuma kwa taifa, izingatiwe kuwa tayari taifa lilishaingia gharama kubwa kuanzia kwenye upembuzi yakinifu, na kusaini mikataba ya awali. Kitendo cha kusitisha katika hatua hii ni kulitia hasara taifa. Moja ya hoja zilizotolewa na rais kama sababu ni kwamba masharti ya wabia nikuwa TRA hairuhusiwi kukusanya mapato, hoja hii ya Rais alikuwa sahihi lakini bahati mbaya alishindwa kufafanua wazi sababu za TRA kutokuwa miusanya mapato ya ubia. Pengine hili Rais alidanganywa.

Pili rais alisema kuwa masharti ya wabia nikuwa Tanzania hairuhusiwi kuendeleza bandari zake zingine. Hoja hii nayo inautata mwingi sana, Bandari zingine zote ziko kwaajili ya ndani, na mradi huu ulikuwa kwa shughuli za kimataifa. Sasa hoja ya kuwa tusikarabati bandari zetu zilizopo ni hoja isiyo na mashiko, Hili inawezekana kabisa Rais hakuambiwa ukweli.

Hoja ya Tatu aliyoitumia Rais Magufuli kukataa mradi ule, ilikuwa kwamba, wabia wanataka wapewe umiliki wa ardhi kwa miaka 99. Hili si la mwekezaji bali la sheria zetu ambazo zinatoa uwekezaji katika ardhi kwa miaka 33 hadi 99. Sasa hoja hii haiwezi kuwa kwa wabia wawili tu kati ya watatu ikiwemo Tanzania yenyewe. Hili nalo kuna uwezekano watu waliamua kumpotosha rais wetu.

Chakusikitisha kwa nchi yangu, Katikati ya mvutano wetu na wabia hadi Rais Magufuli kusitisha mradi, Rais wa Msumbiji Philip Nyusi kwakutumia majasusi wake waliotanda kila pembe ya Afrika na kwingineko, amefanya mageuzi makubwa, amechukua wazo lilelile ambalo limekataliwa Dar es Salaam na wajuvi, amekwenda kulisimika katika Bandari ya Nacala kwakuingia ubia na Wachina kwa Dola bilioni 5 za Kimarekani, hii ni Bandari inayotarajiwa kuwa lango kuu la kiuchumi Afrika.

Wakati hili halijapoa, Mwaka 2017 tu juzi Tanzania tulipowazuia wazungu wasisafirishe madini ghafi na makinikia yao, tuliimba nyimbo kwamba Tanzania itajenga vinu vya kuchenjulia madini hapahapa, na nyimbo ziliimbwa kisiasa zikaitikiwa kishabiki kwa beti za kinafiki kwelikweli. Leo nyimbo haziimbwi, hakuna anayejua kama viwanda vimeshajengwa au laa na hakuna anayehoji hilo kwakuwa ukihojihoji tu basi ukinusurika sana utaenda mochwari au Ubelgiji, tulishazoe vimbunga kwamba vitavuma na kutulia.

Lakini huku sisi tukiwa tumebadili nyimbo sasa tunaimba nyimbo za Standard Gauge nk, Rwanda kwakutumia majasusi wao waliotanda kila pembe ya Dunia, imelichukua wazo lilelile la Tanzania imejenga vinu vya kuchenjulia madini na inatarajiwa kwamba hadi 2024 Rwanda iwe ndio nchi ya kwanza barani Afrika inayosafirisha madini kwa wingi nje ya Afrika. Kumbuka na elewa Rwanda sio mzalishaji wa Dhabu, Almasi wala chochote kiitwacho madini isipokuwa kwenye kilimo cha chai na kahawa huko. Hivyo anategemea viwanda vyake vipokee madini ghafi toka Tanzania, Kongo, Zambia akusanye kodi yake na kugonga muhuri wa madini unaotambulisha kuwa ni madini toka Rwanda nk. Sisi tumelala. Siasa inanguvu bana.

Kwa maoni yangu ninafiki kuna tatizo kubwa kwenye eneo la Ujasusi katika nchi yetu, hasa ujasusi wa Kiuchumi, na hili ndilo lilikuwa msingi wa mimi kuandika Kitabu changu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi. Michakato mingi ya kiuchumi katika nchi hii imekuwa haina mafaa ama inaliacha taifa katika makovu makubwa yasiyozibika. Hii inazaa uhalali wa kuhitaji mageuzi makubwa katika Idara ya Ujasusi nchini kuanzia kwenye ideology, sheria, misingi, kanuni, na mambo anuai ndani ya idara ya ujasusi nchini.

Ujasusi kwa nchi zilizoendelea kama China, Israel, Urusi na Marekani, unafanywa na watu ambao ni smart na wanajengwa kuwa smart ili kuweza kumudu ugumu wa kazi hiyo na kuifanya kazi hiyo kwa mafanikio makubwa. Majasusi katika nchi hizo hawapewi kazi kwasababu ya ujomba ujomba na kujuana.
Ni kweli asilimia kubwa ya information's zenye thamani katika kazi ya ujasusi huwa zinaletwa na "human intelligence" badala ya magazeti, TV na source nyingine za habari.

Kwa maana hiyo basi ni lazima kuwe na watu competent ambao wana uwezo wa kukusanya habari za kijasusi ili tuweze kupata information's za maana na kujenga uwezo wa kuzifanyia kazi informations hizo. Imagine wakati ule wa vita baridi jinsi Directorate 16 ya KGB ilivyoweza kufanya kazi ya kununua sensitive navy information za USA na kuweza kutengeneza balance ya navy fleet bila USA kugundua kwa miaka 17 kupitia kwa Johny Walker junior!

Tanzania kwenye balozi zetu kuna majasusi. Lakini ni majasusi wa aina gani? Wale wa kujua kuongea kifaransa na kireno na lugha nyingine za mataifa ya nje bila upeo wowote wa Technologia? Kama kuna sehemu tunakosea basi ndio hapo. Majasusi wengi wa Tanzania au tunaoambiwa kuwa ni watu wa system wengi katika tafsiri ya kijasusi ni "informers". Ujasusu kama ujasusi hapa Tanzania ni kama hakuna. Usalama wa Taifa au TISS/UWT msingi wao uliounda chombo hiki ni "power defensive", yaani wajibu mkubwa unaelekezwa kwenye kumonitor mwelekeo wa kisiasa Tanzania hasa kuwadhibiti oppositions na elements zote za upinzani na assasinations za elements zozote zinazoonekana kuwa against na himaya ya CCM.

Idara ya Usalama wa Taifa hii tuliyonayo leo ilianzishwa na CCM 1997 kutoka katika muundo wa kijamaa wa chama kimoja, hii ni baada ya kuanzishwa mfumo wa vyama vingi, kwa hiyo bado unaiserve CCM kwanza kisha Taifa linatafsiriwa salama kupitia matokeo ya uimara wa ccm, kama yakifanyika mageuzi ya kimuundo, kisheria, kikanuni na kisera, uimara wa Taifa hautatafsiriwa kupitia uimara wa ccm madarakani, na mambo mengi tunayolalamikia sasa juu ya taifa hayatakuwepo tena. In simple words, taswira kubwa inayoonekana yauhakika ni kazi yao ya kulinda viongozi, kusafiri na viongozi na kuilinda CCM.

Nje ya mambo ya Ujasusi wa Kiuchumi ambao mimi ndio ninaoupigania siku zote uongoze nchi, Naweza kusema Tanzania tuko vizuri katika Ujasusi wa kidola kuliko nchi yoyote pengine Afrika nzima, Hili limefanya kuimeza idara na kuonekana siasa ambazo ndio zinabeba taswira kubwa ya ubora ama udhaifu wa ujasusi Tanzania, Eneo la Ujasusi wa Kidola Tanzania kuna vitengo vya wachapakazi hasa kiko jeshini.., kitengo cha ujasusi ambacho kilikuwa kiko free from politics party ni CMI (central military intelligence). Lakini bahati mbaya muundo na aina ya uongozi wa Magufuli ulikiingiza katika siasa pale kilipofanywa kuwa decision maker wa nchi, lakini upande wa foreign assets ndio wazuri sana wako bize kukusanya taarifa hatarishi dhidi ya nchi...

Kwa undani zaidi Soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.
View attachment 1747076

Ulinikera tu pale ulipotuaminisha kuwa ni Jasusi na una Maisha mazuri ( huna njaa kama Sisi ) na una Network Kubwa ila ukakosa Tsh 5,000,000/ za Faini pale Mahakamani Kisutu hadi Bakuli lilipopitishwa ndiyo ikapatikana na ukasalimika kwenda kuyaanza Maisha yako mapya Segerea.

Katika Uzi wako huu nimegundua mengi hasa juu yako na kwa Serikali na nchi yetu kwa Ujumla. Nianze kwa Kukupongeza kwa Uwasilishaji wako mzuri na makini hapa.

Unaonekana una Thinking Capacity kubwa mno na Laiti Wapuuzi fulani fulani wangechukua muda Kusoma yale uliyokuwa ukiwaandikia huko nyuma huenda leo Tanzania tungefaidika na mengi ya Kimaendeleo kupitia hizi Critical Analysis zako Ndugu.

Hiki ulichokiandika hapa kama kingekuwa ni Majibu ya Swali la Mtihani kuhusu Changamoto za Kiutawala na Uchumi kwa nchi ya Tanzania ningekupa Alama 85% ambayo Kitaaluma ni A ya Ufaulu wa juu kabisa.

Japo kuna maeneo mengine uliyogusia yanahitaji Mjadala zaidi kwa Maslahi mapana na Ustawi na Usalama wetu kama Watanzania na Taifa letu kwa Ujumla ila Bandiko lako hili ( Uzi wako huu ) una Faida nyingi kuliko Hasara kama Wahusika wakiusoma na Kuujadili Kiumakini na haraka sana Kurekebisha na Kufanyia Kazi mapungufu yetu kama nchi nikiamini kuwa hata kama tumetanguliwa ila bado hatujachelewa na tusikate tamaa kwani Tanzania ya Rais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan ( ya sasa ) ni makini na sikivu pia tofauti na iliyokuwepo iliyojaa Uwongo, Majungu, Ubishi, Kiburi, Dharau na iliyobobea katika Ufisadi uliovunja rekodi katika Historia ya Tanzania.

Umeandika Kimtizamo nimependa sana. Na pia kupitia huu Uzi wako kuna sehemu fulani hivi umenifungua Macho Kifikra zaidi kwamba huenda haya Machafuko ya Waasi yaliyoko sasa nchini Msumbiji yanachochewa kwa Siri na Mataifa Jirani ( hasa ya SADC ) kwa Kuhofia endapo hiyo Bandari Kubwa inayojengwa huko itaitajirisha mno Msumbiji, Uchumi wake Kukua kwa haraka, Bandari za Mataifa mengine kukosa Soko hivyo wameungana Kimkakati Kuimaliza Msumbiji ili lengo lake hili lisifanikiwe kwa Kuiogopa.
 
Ulinikera tu pale ulipotuaminisha kuwa ni Jasusi na una Maisha mazuri ( huna njaa kama Sisi ) na una Network Kubwa ila ukakosa Tsh 5,000,000/ za Faini pale Mahakamani Kisutu hadi Bakuli lilipopitishwa ndiyo ikapatikana na ukasalimika kwenda kuyaanza Maisha yako mapya Segerea.

Katika Uzi wako huu nimegundua mengi hasa juu yako na kwa Serikali na nchi yetu kwa Ujumla. Nianze kwa Kukupongeza kwa Uwasilishaji wako mzuri na makini hapa.

Unaonekana una Thinking Capacity kubwa mno na Laiti Wapuuzi fulani fulani wangechukua muda Kusoma yale uliyokuwa ukiwaandikia huko nyuma huenda leo Tanzania tungefaidika na mengi ya Kimaendeleo kupitia hizi Critical Analysis zako Ndugu.

Hiki ulichokiandika hapa kama kingekuwa ni Majibu ya Swali la Mtihani kuhusu Changamoto za Kiutawala na Uchumi kwa nchi ya Tanzania ningekupa Alama 85% ambayo Kitaaluma ni A ya Ufaulu wa juu kabisa.

Japo kuna maeneo mengine uliyogusia yanahitaji Mjadala zaidi kwa Maslahi mapana na Ustawi na Usalama wetu kama Watanzania na Taifa letu kwa Ujumla ila Bandiko lako hili ( Uzi wako huu ) una Faida nyingi kuliko Hasara kama Wahusika wakiusoma na Kuujadili Kiumakini na haraka sana Kurekebisha na Kufanyia Kazi mapungufu yetu kama nchi nikiamini kuwa hata kama tumetanguliwa ila bado hatujachelewa na tusikate tamaa kwani Tanzania ya Rais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan ( ya sasa ) ni makini na sikivu pia tofauti na iliyokuwepo iliyojaa Uwongo, Majungu, Ubishi, Kiburi, Dharau na iliyobobea katika Ufisadi uliovunja rekodi katika Historia ya Tanzania.

Umeandika Kimtizamo nimependa sana. Na pia kupitia huu Uzi wako kuna sehemu fulani hivi umenifungua Macho Kifikra zaidi kwamba huenda haya Machafuko ya Waasi yaliyoko sasa nchini Msumbiji yanachochewa kwa Siri na Mataifa Jirani ( hasa ya SADC ) kwa Kuhofia endapo hiyo Bandari Kubwa inayojengwa huko itaitajirisha mno Msumbiji, Uchumi wake Kukua kwa haraka, Bandari za Mataifa mengine kukosa Soko hivyo wameungana Kimkakati Kuimaliza Msumbiji ili lengo lake hili lisifanikiwe kwa Kuiogopa.

Cha ajabu hakuna mwenye mkataba. Rais Magufuli alisema ni mradi hovyo. Iweje leo amekufa mnageuka?
Serikali iweke mikataba wazi
 
Back
Top Bottom