Asante ni kweli nimenusurika kwa msaada wa Mungu wetu wa huruma.
Kwa kweli hayo namuachia yeye na Mungu wake mwaya,
kama alikusudia kuniambukiza kwa makusudi au la mimi sitaki kuchuma dhambi kwa kukisia,
mradi nimenusurika acha niendelee kuamini kuwa ni bahati mbaya japo mama yangu anasisitiza nikae mbali naye.
Mungu pekee ndiye anayejua ukweli Lizy 11
Usifikiri kwamba umenisurika.......,,upo hatarini kuliko unavyofikiri. Kwanza napata wasiwasi kwamba wewe ni mwathirika na unakuja kujinadi hapa kwamba wewe ni HIV negative ili upate wa kumwambukiza. Halafu eti uneweka slogan ya "YESU NAKUPENDA NITUMIE UPENDAVYO", hivyi ndivyo Yesu anavyokutumia, kuja kuleta unyanyapaa na kujiona wewe ni bora na kuthamini zaidi uhai wako, siku ukikutana na Yesu muulize yeye aliwezaje kuutoa uhai wake kwa ajili ya wengine.