Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 44
Kauli ya waziri mkuu Pinda aliyoitoa jana kupitia Star Tv kwamba serikali itafuata msingi wa utawala wa sheria wa dhana ya utawala bora kuilipa dowans sikubaliani nayo. Kwanza nampinga Pinda kwa kuangalia utawala bora katika ngazi ya juu tu kuhusu kesi inayoamuliwa na taasisi ya kimataifa ya biashara kati ya Dowans na Tanesco. Pili nampinga Pinda kwa mtazamo wake kuwa anayetarajiwa kulipa ufisadi wa Dowans siyo serikali bali ni sisi wananchi- raia wa Tanzania. Tatu, Pinda anakwepa ukweli kwamba rushwa si mojawapo ya misingi ya utawala bora.
Pinda amepotoka kwa sababu haiwezekani auone utawala wa sheria katika taasisi ya kimataifa inayoamua kesi wakati huohuo anakwepa ukweli kwamba kimsingi mkataba kati ya Dowans na Tanesco au wananchi wa Tanzania si halali kisheria- ni wa kifisadi. Dowans ilirithishwa mkataba feki na kampuni hewa ya Richmond. Utawala bora wa sheria unatoka wapi katika hali hii? Pinda pia anatundanganya watanzania eti serikali ndiyo inayotarajiwa kulipa ufisadi wa Dowans hali akijua pesa za serikali zinakamuliwa kutoka kwetu wananchi, hatutaki ufisadi huu. Mwisho, Pinda hawezi kuzungumzia utawala bora katika mkataba anaojua fika kuwa ni wa rushwa. Rushwa ni kipimo cha kukosekana kwa utawala bora. Lowasa, Msabaha na karamagi walijiuzuru baada ya bunge kubaini rushwa ilitumika katika kuipa Richmond kazi ya kuzalisha umeme. Pinda anajua kuwa Richmond haipo katika mafaili ya kampuni zilizowahi kusajiliwa na Brela hapa Tanzania. Uhalali wa kisheria na utawala bora katika mkataba wa Dowans unatoka wapi mzee Pinda?
Pinda asitufanya wananchi hatuelewi. Anataka kuhalalisha ufisadi wa Dowans na kutubebesha wananchi madeni ya kifisadi kwa manufaa ya kuwalinda mafisadi wa serikali ya CCM katika mkataba wa Richmond na Dowans. CCM ikihalalisha mzigo huu kwa wananchi itaendelea kukabiliana na hasira kali za wananchi, wananchi tumechoka kunyonywa na kunyanyaswa na CCM.
Pinda amepotoka kwa sababu haiwezekani auone utawala wa sheria katika taasisi ya kimataifa inayoamua kesi wakati huohuo anakwepa ukweli kwamba kimsingi mkataba kati ya Dowans na Tanesco au wananchi wa Tanzania si halali kisheria- ni wa kifisadi. Dowans ilirithishwa mkataba feki na kampuni hewa ya Richmond. Utawala bora wa sheria unatoka wapi katika hali hii? Pinda pia anatundanganya watanzania eti serikali ndiyo inayotarajiwa kulipa ufisadi wa Dowans hali akijua pesa za serikali zinakamuliwa kutoka kwetu wananchi, hatutaki ufisadi huu. Mwisho, Pinda hawezi kuzungumzia utawala bora katika mkataba anaojua fika kuwa ni wa rushwa. Rushwa ni kipimo cha kukosekana kwa utawala bora. Lowasa, Msabaha na karamagi walijiuzuru baada ya bunge kubaini rushwa ilitumika katika kuipa Richmond kazi ya kuzalisha umeme. Pinda anajua kuwa Richmond haipo katika mafaili ya kampuni zilizowahi kusajiliwa na Brela hapa Tanzania. Uhalali wa kisheria na utawala bora katika mkataba wa Dowans unatoka wapi mzee Pinda?
Pinda asitufanya wananchi hatuelewi. Anataka kuhalalisha ufisadi wa Dowans na kutubebesha wananchi madeni ya kifisadi kwa manufaa ya kuwalinda mafisadi wa serikali ya CCM katika mkataba wa Richmond na Dowans. CCM ikihalalisha mzigo huu kwa wananchi itaendelea kukabiliana na hasira kali za wananchi, wananchi tumechoka kunyonywa na kunyanyaswa na CCM.