Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,062
- 79,089
kwa kuangalia harakaharaka migomo ya wanafunzi Tumaini na SAUT inaweza kuwa na maana lakini tukiangalia gharama za uendeshaji sidhani kama kutoa ada ya milioni 2.5 ni kubwa namna hiyo kama hawa wakuu wanavyotaka kutusadikisha! Hivi vyuo ni vya taasisi binafsi zenye malengo ya kutoa elimu bora wakati huo huo kuboresha huduma na kupanua uwezo wao! Na ninaamini kila centi inayoongezwa kwenye ada zao ina mipango maalum katika bajeti ya hivi vyuo ikiwemo kuajiri waalimu wapya (CAG anaweza kuhakikisha hilo)! Ikumbukwe bado kuna uhaba mkubwa wa waalimu kwenye hivi vyuo!
Sasa ningewashauri hawa wanafunzi waelekeze maandamano yao kwa serikali ya JK kwa kuwa ndiyo sababu a kupanda kwa gharama za uendeshaji kuanzia umeme, chakula hata mafuta ambavyo vinaadhiri uendeshaji na hata kiasi anachopata mwalimu ambaye naye mwishowe anadai mshahara upande. Vilevile hizi taasisi za vyuo wana mipango yao yaani kuboresha na kuongeza uwezo wa kufundisha na sidhani kama itakuwa ustaarabu kushusha tu kwa vile watu fulani wanataka kusoma dezo je wadogo zenu wanaofuata hawana haki ya kukuta hizo huduma hapo? na je hawana haki ya kupata nafasi zaidi katika hivyo vyuo?
Tutumie busara kwenye hili millioni 2.5 si kiasi cha kulalamika namna hiyo mpaka migomo ukizingatia zinalenga katika kuboresha huduma katika hivyo vyuo!
Sasa ningewashauri hawa wanafunzi waelekeze maandamano yao kwa serikali ya JK kwa kuwa ndiyo sababu a kupanda kwa gharama za uendeshaji kuanzia umeme, chakula hata mafuta ambavyo vinaadhiri uendeshaji na hata kiasi anachopata mwalimu ambaye naye mwishowe anadai mshahara upande. Vilevile hizi taasisi za vyuo wana mipango yao yaani kuboresha na kuongeza uwezo wa kufundisha na sidhani kama itakuwa ustaarabu kushusha tu kwa vile watu fulani wanataka kusoma dezo je wadogo zenu wanaofuata hawana haki ya kukuta hizo huduma hapo? na je hawana haki ya kupata nafasi zaidi katika hivyo vyuo?
Tutumie busara kwenye hili millioni 2.5 si kiasi cha kulalamika namna hiyo mpaka migomo ukizingatia zinalenga katika kuboresha huduma katika hivyo vyuo!