Sikubaliani na kauli hii ya Baba wa Taifa NYERERE

Ombeni Mbise

Member
Nov 2, 2012
40
9
Nikiwa kama mtanzania ninayefikiri ninaamini kuwa hakuna aliyekamilika na wa kuaminiwa asilimia 100 zaidi ya Mungu peke yake. Mengi aliyosema mzee wetu mpendwa hayati baba wa taifa yanatufaa na yako relevant kwetu na hata kwa kizazi kijacho kisichomjua kitaendelea kunufaika na hotuba zake nzuri.
Lakini ninapingana asilimia 100 na kauli ya mwalimu pale aliposema ''Kiongozi bora hawezi toka nje ya CCM''. Kwa kweli hapo alisahau au alipitiwa kidogo jambo ambalo angerudi Duniani leo kwa hakika angekanusha kauli yake andapo angeona viongozi wa CCM na vyama vya upinzani ambapo tumejionea wabunge wadogo wenye uongozi makini na dhabiti ikilinanishwa na CCM aliyoiamini Baba wa Taifa.
 
Jana nilikuwa nasikiliza hotuba ya Baba wa Taifa hii mwal. nyerere. niligundua kuwa angerudi Duniani leo angekanusha kauli yake kuwa kiongozi bora hawezi toka nje ya CCM.Angebadilisha na kusema kiongozi bora hawezi toka ndani ya CCM kutokana na hali tete ya Rushwa ndani ya chama hicho tena akifufuka leo kwa jinsi alivyokuwa hapendi rushwa atakufa presha kwa jinsi machalii walimchafulia chama
 
Rejea kauli ya Mwl Nyerere wakati wa mchakato wa kupitisha majina ya wagombea Urais kupitia CCM mwaka 1995 baada ya kuona majina ya Edward Lowassa na John Malecela baba WILLE LE MUTUZ alisema kama hao hawatatolewa atawarudishia kadi yao ya chama kwani "CCM SI BABA YAKE WALA MAMA YAKE" kauli hiyo iliashiria kwamba angeweza kukihama chama hicho wakati wowote,lakini pia umesahau kuwa kuna UHURU WA KUFANYA MAAMUZI,kwa mfano wewe unaweza ukaamua kuwa CDM hadi kufa lakini hakuna mtu atakayefikiri kuwa hauko sahihi labda awe yeye anashindwa KUFIKIRI VIZURI,h.....
BY THE WAY HOJA YAKO HAINA MASHIKO NA NI DHAIFU SANA KULIKO KUMSUKUMA MLEVI AU MGONJWA WA KIPINDUPINDU
Nikiwa kama mtanzania ninayefikiri ninaamini kuwa hakuna aliyekamilika na wa kuaminiwa asilimia 100 zaidi ya Mungu peke yake. Mengi aliyosema mzee wetu mpendwa hayati baba wa taifa yanatufaa na yako relevant kwetu na hata kwa kizazi kijacho kisichomjua kitaendelea kunufaika na hotuba zake nzuri.
Lakini ninapingana asilimia 100 na kauli ya mwalimu pale aliposema Kiongozi bora hawezi toka nje ya CCM. Kwa kweli hapo alisahau au alipitiwa kidogo jambo ambalo angerudi Duniani leo kwa hakina angekanusha kauli yake andapo angeona viongozi wa CCM na vyama vya upinzani ambapo tumejionea wabunge wadogo wenye uongozi makini na dhabiti ikilinanishwa na CCM aliyoiamini Baba wa Taifa.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kauli ipi ndugu yangu? mbona Mwl. alisema yote...maani kipindi hicho sisiem kulikuwa na viongozi lakini siku hizi kuna watawala.. so kuna tofauti kubwa kati ya watawala na Viongozi...
 
Bwana Mbise, kwa kweli hata mimi napingana kabisa na ile kauli tena inanichefua kila ninaposikiliza ile hotuba (bado ninayo DVD yake) na kama isingekuwa busara zingine nyingi zilizo kwenye hotuba ile ile, ile DVD ningeichoma. Baada ya kutafakari sana kuhusu kauli ile nilifikia hitimisho kuwa ilikuwa ni kauli ya kisiasa mwana TANU/CCM ambaye anatamani au anaamini kuwa CCM itatawala milele. Faraja ninayopata moyoni ni kwamba, kama angefufuka leo (jambo ambalo haliwezekani) angekiri kutoa kauli ile lakini ange-justify kwa muktadha wa wakati ule na ukweli ni kuwa kwa hali ilivyo sasa asingeweza kuirudia kwa ushupavu ule ule; Baba wa Taifa alikuwa ni mkweli katika mazingira husika na asingeweza kuvumilia uozo uliopo sasa.
Mungu atusaidie, tuishi maisha safi ili hatimaye siku moja tuonane na Baba wa Taifa kama ni mapenzi YAKE.
Amen!
 
Jana nilikuwa nasikiliza hotuba ya Baba wa Taifa hii mwal. nyerere. niligundua kuwa angerudi Duniani leo angekanusha kauli yake kuwa kiongozi bora hawezi toka nje ya CCM.Angebadilisha na kusema kiongozi bora hawezi toka ndani ya CCM kutokana na hali tete ya Rushwa ndani ya chama hicho tena akifufuka leo kwa jinsi alivyokuwa hapendi rushwa atakufa presha kwa jinsi machalii walimchafulia chama
Ni kweli kabisa kiongozi bora atatoka ndani ya CCM,Dr. Slaa ametoka ndani ya ccm,hivyo tutashuhudia kiongozi bora kutoka ndani ya ccm kupitia cdm.
 
Kauli ya Mwalimu Nyerere ni valid kabisa. Upinzani utakuwa mkubwa kama wale walio CCM wataamua kuiacha na kuunda chama kipya. Mfano mzuri ni pale akina Mpendazoe walipojaribu kuanzisha CCJ, kama isingekuwa hujuma leo hii CCM ingekuwa pengine nje kama chama pinzanani maana CCJ na CDM wangepunguza idadi wa wanachama wa CCM na hata wapiga kura kwa ujumla. Kile kinachosemwa ushindi wa kishindo usingekuwepo hata kidogo. Na hili ndilo linalosubiriwa 2015 kama nguvu za upinzani zitaongezeka hasa katika mikoa yenye ushawishi.
 
Jana nilikuwa nasikiliza hotuba ya Baba wa Taifa hii mwal. nyerere. niligundua kuwa angerudi Duniani leo angekanusha kauli yake kuwa kiongozi bora hawezi toka nje ya CCM.Angebadilisha na kusema kiongozi bora hawezi toka ndani ya CCM kutokana na hali tete ya Rushwa ndani ya chama hicho tena akifufuka leo kwa jinsi alivyokuwa hapendi rushwa atakufa presha kwa jinsi machalii walimchafulia chama

Mkuu ili umwelewe unapaswa kuzingatia muktadha na wakati/Kairos alipolizungumza hilo jambo! Kumbuka nyakati zake ni tofauti na nyakati hizi za sasa! Hivyo hutakuwa unamtendea haki kwa kumhukumu kwa kutumia kigezo cha wakati wa sasa!!
 
Ni vizuri Umeiona na kuisema wazi kwani kuna wengine awafikir kwa vichwa vyao kila alichoongea mwalimu ukimeza bila kutafuna, Kama kiongoz wetu wa Mwanzo tunawajibu wa kumuenzi kwa mazuri yote aliyotufanyia pamoja na Huu usia wake but Tuchukue yale mazuri na mabaya tuyaache SI KWELI CCM PEKEE NDO INAWEZA KUTOA RAIS BORA HUU NI MFUMO HURU WA KIDEMOKRASIA WANANCHI WAKIPENDA WAKIRIDHIKA WATACHAGUA UPINZANI AU NJE YA CCM SO wasifungwe na mawazo ya propaganda
 
Bwana Mbise, kwa kweli hata mimi napingana kabisa na ile kauli tena inanichefua kila ninaposikiliza ile hotuba (bado ninayo DVD yake) na kama isingekuwa busara zingine nyingi zilizo kwenye hotuba ile ile, ile DVD ningeichoma. Baada ya kutafakari sana kuhusu kauli ile nilifikia hitimisho kuwa ilikuwa ni kauli ya kisiasa mwana TANU/CCM ambaye anatamani au anaamini kuwa CCM itatawala milele. Faraja ninayopata moyoni ni kwamba, kama angefufuka leo (jambo ambalo haliwezekani) angekiri kutoa kauli ile lakini ange-justify kwa muktadha wa wakati ule na ukweli ni kuwa kwa hali ilivyo sasa asingeweza kuirudia kwa ushupavu ule ule; Baba wa Taifa alikuwa ni mkweli katika mazingira husika na asingeweza kuvumilia uozo uliopo sasa.
Mungu atusaidie, tuishi maisha safi ili hatimaye siku moja tuonane na Baba wa Taifa kama ni mapenzi YAKE.
Amen!
Bwana Msengepavi,ni kweli kabisa,nami nakubaliana na kauli hii 100% kwamba Rais bora atatoka ndani ya CCM,ni kauri isiyo na mashaka kabisa,leo hii wana cdm tunaamini kuwa Rais bora angekuwa Dr.Slaa,ambaye alitoka ndani ya CCM.Hakusema agombee kupitia chama gani isipokuwa atatoka ndani ya CCM.Hiyo ni dhana namba moja,dhani ya pili ni kwamba "Ukitaka kuwa Rais bora lazima utoke ndani ya CCM". Kwamba huwezi kuwa rais bora huku ukiwa ndani ya CCM,wakati mwingine waliokusanyika wanaweza kushangilia kauli hii bila kujua maana yake.

Lakini mwisho kabisa anaweza kusema CCM kwa maana ya CCM,kwani alikuwa miongoni mwa waasisi wa chama,na hadi anafariki hakuwahi kukabidhi kadi ya CCM.Lakini yote kwa yote,hoja mbili za juu kwangu zina mashiko sana
.
 
Mkuu ili umwelewe unapaswa kuzingatia muktadha na wakati/Kairos alipolizungumza hilo jambo! Kumbuka nyakati zake ni tofauti na nyakati hizi za sasa! Hivyo hutakuwa unamtendea haki kwa kumhukumu kwa kutumia kigezo cha wakati wa sasa!!
Kiongozi mwenye vision hazungumzii kauli za hapo kwa hapo! anaingalia kauli yake itakuwa na athari gani baadaye!
Jamaa alikosa maono ya mbali.
 
sio hilo tuu hata aliposema kuwa wachaga hawafai kuwa marais hiyo ilikuwa kauli ya kibaguzi kwa watu wa tanzania...na ilikuwa doa kubwa sana kwake kwa hili.....
 
Kiongozi mwenye vision hazungumzii kauli za hapo kwa hapo! anaingalia kauli yake itakuwa na athari gani baadaye!
Jamaa alikosa maono ya mbali.

Mkuu, yeye hakuwa Nabii na alichosema hakukiita Unabii! Alizungumzia hadhara ya wakati wake, hivyo sio sahihi kuhukumu kauli yake hiyo kwa kutumia vigezo vya sasa! Nina uhakika angalikuwapo leo kauli yake ingalikuwa nyingine kabisa, na nafikiri isingalikuwa njema sana masikioni na mioyoni mwa wana-CCM!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom