Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 56,326
- 92,507
3ANAANDIKA Mchao Tv
KWA MFANO TU
Mechi ya Azam dhidi ya Yanga ilipigwa Septemba 6, 2022 (zaidi ya wiki mbili zilizopita, ni siku 16 zilizopita) ambapo mchezaji wa Yanga Bernard Morrison alifanya utovu wa nidhamu kwa kumkanyaga Lusajo Mwaikenda wa Azam kwa makusudi.
Kwa mfano Bodi ya Ligi wangekaa na kamati yao ya saa 72 na kutoa maamuzi kungekuwa na ubaya gani???
Na kama maamuzi yangekuwa kama jinsi walivyoamua, maana yake Morrison angeikosa michezo ya Yanga dhidi ya Mtibwa Sugar uliochezwa Septemba 13, angeukosa pia mchezo dhidi ya Ihefu (ambao ulipangwa kuchezwa Septemba 29 kabla ya kusogezwa mbele) na angeukosa pia mchezo dhidi ya Ruvu Shooting ambao unatarajiwa kuchezwa Oktoba 3.
Tuna-assume mchezo kati ya Yanga dhidi ya Ihefu ungeahirishwa kama ilivyo hivi sasa, maana yake ni kwamba Morrison angeikosa michezo ya Yanga dhidi ya Mtibwa Sugar (Septemba 13), dhidi ya Ruvu (Oktoba 3) na adhabu yake angeimalizia kwa kuukosa mchezo dhidi ya Namungo ambao kwa mujibu wa ratiba utachezwa Oktoba 13... halafu kwenye Kariakoo Derby dhidi ya Simba (Oktoba 23) mtoto mtukutu angekuwa ndani ya nyumba.
Jana Bodi ya Ligi walitoa taarifa ya kuusogeza mbele mchezo kati ya Yanga na Ihefu (kutoka Septemba 29 hadi Novemba 29, yaan miezi miwili mbele) halafu leo Bodi ya Ligi hao hao wanatoa taarifa za kumfungia Morrison michezo mitatu kutoka sasa ambapo mchezo dhidi ya Simba unakuwa mmojawapo kwa kosa la siku 16 nyuma.
KWA MFANO TU lakini.....Yanga wakihoji uhalali wa adhabu ya BM33 kutoka leo Shirikisho la TFF na Bodi ya Ligi watajitetea kwa lipi??
KWA MFANO TU lakini.....Yanga wakiituhumu TFF kuwa inawahujumu, ni utetezi upi utakaotolewa na wenye mamlaka kupinga hoja hiyo??
KWA MFANO TU.....Yanga ikilalamika kuwa kuna bingwa anaandaliwa na Shirikisho la soka (TFF) kama jinsi Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangungu alivyowahi kulituhumu Shirikisho, ni nani atakayekuwa na mamlaka ya kuchukua hatua za kinidhamu juu ya kauli hiyo.
KWA MFANO TU......yaan ni mfano tu, ni mfano ambao........
KWA MFANO TU
Mechi ya Azam dhidi ya Yanga ilipigwa Septemba 6, 2022 (zaidi ya wiki mbili zilizopita, ni siku 16 zilizopita) ambapo mchezaji wa Yanga Bernard Morrison alifanya utovu wa nidhamu kwa kumkanyaga Lusajo Mwaikenda wa Azam kwa makusudi.
Kwa mfano Bodi ya Ligi wangekaa na kamati yao ya saa 72 na kutoa maamuzi kungekuwa na ubaya gani???
Na kama maamuzi yangekuwa kama jinsi walivyoamua, maana yake Morrison angeikosa michezo ya Yanga dhidi ya Mtibwa Sugar uliochezwa Septemba 13, angeukosa pia mchezo dhidi ya Ihefu (ambao ulipangwa kuchezwa Septemba 29 kabla ya kusogezwa mbele) na angeukosa pia mchezo dhidi ya Ruvu Shooting ambao unatarajiwa kuchezwa Oktoba 3.
Tuna-assume mchezo kati ya Yanga dhidi ya Ihefu ungeahirishwa kama ilivyo hivi sasa, maana yake ni kwamba Morrison angeikosa michezo ya Yanga dhidi ya Mtibwa Sugar (Septemba 13), dhidi ya Ruvu (Oktoba 3) na adhabu yake angeimalizia kwa kuukosa mchezo dhidi ya Namungo ambao kwa mujibu wa ratiba utachezwa Oktoba 13... halafu kwenye Kariakoo Derby dhidi ya Simba (Oktoba 23) mtoto mtukutu angekuwa ndani ya nyumba.
Jana Bodi ya Ligi walitoa taarifa ya kuusogeza mbele mchezo kati ya Yanga na Ihefu (kutoka Septemba 29 hadi Novemba 29, yaan miezi miwili mbele) halafu leo Bodi ya Ligi hao hao wanatoa taarifa za kumfungia Morrison michezo mitatu kutoka sasa ambapo mchezo dhidi ya Simba unakuwa mmojawapo kwa kosa la siku 16 nyuma.
KWA MFANO TU lakini.....Yanga wakihoji uhalali wa adhabu ya BM33 kutoka leo Shirikisho la TFF na Bodi ya Ligi watajitetea kwa lipi??
KWA MFANO TU lakini.....Yanga wakiituhumu TFF kuwa inawahujumu, ni utetezi upi utakaotolewa na wenye mamlaka kupinga hoja hiyo??
KWA MFANO TU.....Yanga ikilalamika kuwa kuna bingwa anaandaliwa na Shirikisho la soka (TFF) kama jinsi Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangungu alivyowahi kulituhumu Shirikisho, ni nani atakayekuwa na mamlaka ya kuchukua hatua za kinidhamu juu ya kauli hiyo.
KWA MFANO TU......yaan ni mfano tu, ni mfano ambao........