Sikuamini nilivyofika Njombe, kumbe Tanzania hii kuna sehemu kama hizi?

Lasway.Jr

JF-Expert Member
Jul 25, 2015
230
402
Katika mizunguko yangu ya kazi nilitoka Morogoro nikaenda Mbeya kufanya shughuli zangu za kilimo hasa umwagiliaji, basi nikiwa Mbeya pale kwa kuwa mimi ni mdadisi nitampigia jamaa yangu mmoja ambae ni mwenyeji wa Mbeya pia ni Mkulima, duh jamaa mcheshi sana na ni mshikaji sana japokuwa ni msomi mkubwa na mfanyabiashara

Basi akanambia njoo huku Njombe,jioni ile nikapanda gari kuelekea huko, nilipofika nikakutana na jamaa ang mmoja niliesoma nae chuo akanipokea na akawa mwenyeji wangu.
Nilipompigia jamaa angu huyu Mkulima akanambia bado hajafika mjini ndio anatoka shamba, kumbuka hapo ni saa nne usiku.

Kesho yapo ikawa asubh , baridi ilikuwa kiasi japokuwa mwenyeji wangu alinambia ni wakati wa joto kwa sasa haaa haaaa Njombe kama ulaya vile

Kama saa moja hivi jamaa angu alikuja akanichukua , tukampitia na mshikaji wake mmoja , na safari ikaanza ya kuelekea nisikokujua kwenye nchi ya maziwa na Asali kama Mwendo wa 80km tukaanza kukwepana na milima ya Lupembe na baada ya muda mshikaji wangu akanambia hapa ndio tunaingia shamba, kwa kuwa lilikuwa shamba jipya lenye milima na milima , na lilikuwa Shamba kubwa kiasi , haaa haaa sio kubwa kama unavyofikiria ww ila ni zaidi ya hekari 400+ Virgin land , hapo hapo nikaanza udadisi wangu na kuanza kukumbuka nilivyokuwa nafundishwa na Maprofesa wangu enzi hizo nasoma pale SUA ,

Nilichoshangaa ni nn?
Katika udadisi wangu niligundua kuwa ile Ardhi haikuwahi kulimwa , mimea iliyoota maeneo Yale iliashiria rutuba ya ajabu iliyoko katika udongo ule , hali ya hewa na baadhi ya vitu vilionyesha kuwa eneo lile linapata mvua kubwa sana kwa mwaka tatribani 2300mm per yr
f8e30fe5a8f17a71a09ce3f3cca203a6.jpg


Organic matter layer ya Ardhi ile ni zaidi 40cm,
Nilichoshangaa zaidi ni pale nilipoenda ndani ya Shamba zaidi na kuona kuwa kuna chanzo kizuri cha maji , nilitamani niende kwetu Rombo niwachukue wale wazee niwalete pale kwa sababu kule sijawahi kuona kitu kama kile .
Bhasi nikaendelea na utafiti wangu nikagundua vitu vingi zaidi katika Ardhi ile na baada ya kukaa na kuangalia milima ikishangaa ujio wetu na muda ulikuwa umeenda , tukafanya baadhi ya kazi pale na kuanza kurudi

Ninachotaka kusema ni kwamba
Don't limit your mind to think
Seed and not diamond will make Africa great
Wekeza vzr kwenye kilimo
Uzi utakao fuata nitawaeleza katika hyo Ardhi ni nini kimepandwa na kinawezaje kumlipa Mkulima tena bila stress , najua utafikiri ni miti ya mbao lakini sio kweli ....stay tuned
Jumapili njema wana jamvi
 
hayo ndo mambo ya msingi asee!! sio kila siku vijana kujadili mambo ambayo hayana hata faida kwetu, bado tuna ardhi kubwa ambayo ni idle, tutafuteni fursa popote ndani ya ardhi ya Tanzania yetu yenye amani na upendo.
 
Katika mizunguko yangu ya kazi nilitoka Morogoro nikaenda Mbeya kufanya shughuli zangu za kilimo hasa umwagiliaji, basi nikiwa Mbeya pale kwa kuwa mimi ni mdadisi nitampigia jamaa yangu mmoja ambae ni mwenyeji wa Mbeya pia ni Mkulima, duh jamaa mcheshi sana na ni mshikaji sana japokuwa ni msomi mkubwa na mfanyabiashara

Basi akanambia njoo huku Njombe,jioni ile nikapanda gari kuelekea huko, nilipofika nikakutana na jamaa ang mmoja niliesoma nae chuo akanipokea na akawa mwenyeji wangu.
Nilipompigia jamaa angu huyu Mkulima akanambia bado hajafika mjini ndio anatoka shamba, kumbuka hapo ni saa nne usiku.

Kesho yapo ikawa asubh , baridi ilikuwa kiasi japokuwa mwenyeji wangu alinambia ni wakati wa joto kwa sasa haaa haaaa Njombe kama ulaya vile

Kama saa moja hivi jamaa angu alikuja akanichukua , tukampitia na mshikaji wake mmoja , na safari ikaanza ya kuelekea nisikokujua kwenye nchi ya maziwa na Asali kama Mwendo wa 80km tukaanza kukwepana na milima ya Lupembe na baada ya muda mshikaji wangu akanambia hapa ndio tunaingia shamba, kwa kuwa lilikuwa shamba jipya lenye milima na milima , na lilikuwa Shamba kubwa kiasi , haaa haaa sio kubwa kama unavyofikiria ww ila ni zaidi ya hekari 400+ Virgin land , hapo hapo nikaanza udadisi wangu na kuanza kukumbuka nilivyokuwa nafundishwa na Maprofesa wangu enzi hizo nasoma pale SUA ,

Nilichoshangaa ni nn?
Katika udadisi wangu niligundua kuwa ile Ardhi haikuwahi kulimwa , mimea iliyoota maeneo Yale iliashiria rutuba ya ajabu iliyoko katika udongo ule , hali ya hewa na baadhi ya vitu vilionyesha kuwa eneo lile linapata mvua kubwa sana kwa mwaka tatribani 2300mm per yr
f8e30fe5a8f17a71a09ce3f3cca203a6.jpg


Organic matter layer ya Ardhi ile ni zaidi 40cm,
Nilichoshangaa zaidi ni pale nilipoenda ndani ya Shamba zaidi na kuona kuwa kuna chanzo kizuri cha maji , nilitamani niende kwetu Rombo niwachukue wale wazee niwalete pale kwa sababu kule sijawahi kuona kitu kama kile .
Bhasi nikaendelea na utafiti wangu nikagundua vitu vingi zaidi katika Ardhi ile na baada ya kukaa na kuangalia milima ikishangaa ujio wetu na muda ulikuwa umeenda , tukafanya baadhi ya kazi pale na kuanza kurudi

Ninachotaka kusema ni kwamba
Don't limit your mind to think
Seed and not diamond will make Africa great
Wekeza vzr kwenye kilimo
Uzi utakao fuata nitawaeleza katika hyo Ardhi ni nini kimepandwa na kinawezaje kumlipa Mkulima tena bila stress , najua utafikiri ni miti ya mbao lakini sio kweli ....stay tuned
Jumapili njema wana jamvi

Mkuu Njombe cha mtoto sana mimi nafanya kilimo sehemu moja inaitwa Kidabaga iko Iringa huko. Ni balaa sana na hali ya hewa ni kama Ulaya, zamani Mahindi walikuwa hawapandii mbolea.

Sema tunapana vikumbo na makampuni makubwa kama New Forest na wale wa One Acre Fund. Wanamiliki maeneo makubwa sana na Raisi Kikwete aliwapa tu; Inafika kipindi wananyanyasa wazawa na kuchoma mashamba yao ya miti kwa maksudi pindi ukikataa kuwauzia.

Nawashauri vijana watembee na kuwekeza huko. It is a nice place to invest: jaribu kwenda kufanya utafiti mkuu

NB: Kuna vibarua wengi sana wa bei nafuu na Wahehe wengi ni watu waaminifu sana endapo utawapa stahiki zao kwa wakati.
 
Mkuu Njombe cha mtoto sana mimi nafanya kilimo sehemu moja inaitwa Kidabaga iko Iringa huko. Ni balaa sana na hali ya hewa ni kama Ulaya, zamani Mahindi walikuwa hawapandii mbolea.

Sema tunapana vikumbo na makampuni makubwa kama New Forest na wale wa One Acre Fund. Wanamiliki maeneo makubwa sana na Raisi Kikwete aliwapa tu; Inafika kipindi wananyanyasa wazawa na kuchoma mashamba yao ya miti kwa maksudi pindi ukikataa kuwauzia.

Nawashauri vijana watembee na kuwekeza huko. It is a nice place to invest: jaribu kwenda kufanya utafiti mkuu

NB: Kuna vibarua wengi sana wa bei nafuu na Wahehe wengi ni watu waaminifu sana endapo utawapa stahiki zao kwa wakati.
Challenge hiyo hasa KUCHOMEWA MAENEO ya hizo TAASISI waisemeaje kiongozi
 
Mkuu Njombe cha mtoto sana mimi nafanya kilimo sehemu moja inaitwa Kidabaga iko Iringa huko. Ni balaa sana na hali ya hewa ni kama Ulaya, zamani Mahindi walikuwa hawapandii mbolea.

Sema tunapana vikumbo na makampuni makubwa kama New Forest na wale wa One Acre Fund. Wanamiliki maeneo makubwa sana na Raisi Kikwete aliwapa tu; Inafika kipindi wananyanyasa wazawa na kuchoma mashamba yao ya miti kwa maksudi pindi ukikataa kuwauzia.

Nawashauri vijana watembee na kuwekeza huko. It is a nice place to invest: jaribu kwenda kufanya utafiti mkuu

NB: Kuna vibarua wengi sana wa bei nafuu na Wahehe wengi ni watu waaminifu sana endapo utawapa stahiki zao kwa wakati.
Ni eneo zuri sana mkuu! Kuna ardhi safi sana wilaya ya kilolo
 
Back
Top Bottom