Ni kweli nako kuko vizuri nilifika kule kuna hawa jamaa wa gesi, nikafika kuna halmashauri mpya nimeisahau jina iko huko mbele ya Rungwe milimaniKuna pahala Mbeya panaitwa Rungwe broo, mwaka mzima ni kijani. Vyanzo vya maji kibao
Hahahaha waliniuzia viazi Ulaya bei chee mpaka nikavikataa kwa kukosa pa kuviwekahaha wapo wengi na ndo wapigakura wengi wa ccm
Kama ukiwa na dhahabu kisha hauna akili bado ni ufukara tuUkanda huo umebarikiwa sana, ujue kuna sehemu zina Ardhi nzr kiasi kwamba zikitumika vzr lazma mafanikio yawepo, unaaenda sehem kipindi kama hiki cha kiangazi unakuta mimea yote ya Kijani but wazawa ni masikini
Nabaki na maswali mengi sana
Hivi mpaka leo duniani kuna sehemu ni mbali?! Nadhani ni uwezo tu mdogo ila hakuna mbali. Wazungu wasingekuja huku kutubanabananimekumiss Lasway.Jr !yeah huko njombe nchi ya asali nami nimefika jaman ni kuzuri maparachichi na mazaga zaga kibao yanastawi vizuri mnooooo ! safi sana kwa kazi yako aisee !sema mbali duh
tunaendelea na utaratibu wetu wa kuwafahamu....Vipi ulifanikiwa kuwaunganisha?
Sure...kuna la kujifunza kwenye mijadala ya namna hii.hayo ndo mambo ya msingi asee!! sio kila siku vijana kujadili mambo ambayo hayana hata faida kwetu, bado tuna ardhi kubwa ambayo ni idle, tutafuteni fursa popote ndani ya ardhi ya Tanzania yetu yenye amani na upendo.
Tembelea Makete uone jinsi tulivyobarikiwa kuku wanakula Apple's maana hakuna wakuzila,tunaomba mwekezaji atujengee kiwanda ili tusindikeVery innocent and genuine comment.
Nahisi umewahi kujihusisha na uwekezaji ktk kilimo kwa jinsi ulivyo changia maoni yako.
Sasa mkuu kwanini usiweke kwenye maboksi, pakiza kwenye fuso uyalete huku Dar?Tembelea Makete uone jinsi tulivyobarikiwa kuku wanakula Apple's maana hakuna wakuzila,tunaomba mwekezaji atujengee kiwanda ili tusindike
Shida yenu njombaa ukimwi ndio nyumbani kwao hukooo
Wewe uko makete? Apples mnalima varieties gani? Mimi nahitaji miche, naweza kupata huko?Tembelea Makete uone jinsi tulivyobarikiwa kuku wanakula Apple's maana hakuna wakuzila,tunaomba mwekezaji atujengee kiwanda ili tusindike
Bwana wee nilitembelea tu,sielewi chochote aina ya apples nilijua kutafuna tuWewe uko makete? Apples mnalima varieties gani? Mimi nahitaji miche, naweza kupata huko?
Kwa kweli huku nilitembelea tu ila changamoto ni barabara ina bodi ziboreshwe ili at least wafanyabiashara waweze kukusanyaSasa mkuu kwanini usiweke kwenye maboksi, pakiza kwenye fuso uyalete huku Dar?
Utajiri huo mkuu.
Mkuu salama,Katika mizunguko yangu ya kazi nilitoka Morogoro nikaenda Mbeya kufanya shughuli zangu za kilimo hasa umwagiliaji, basi nikiwa Mbeya pale kwa kuwa mimi ni mdadisi nitampigia jamaa yangu mmoja ambae ni mwenyeji wa Mbeya pia ni Mkulima, duh jamaa mcheshi sana na ni mshikaji sana japokuwa ni msomi mkubwa na mfanyabiashara
Basi akanambia njoo huku Njombe,jioni ile nikapanda gari kuelekea huko, nilipofika nikakutana na jamaa ang mmoja niliesoma nae chuo akanipokea na akawa mwenyeji wangu.
Nilipompigia jamaa angu huyu Mkulima akanambia bado hajafika mjini ndio anatoka shamba, kumbuka hapo ni saa nne usiku.
Kesho yapo ikawa asubh , baridi ilikuwa kiasi japokuwa mwenyeji wangu alinambia ni wakati wa joto kwa sasa haaa haaaa Njombe kama ulaya vile
Kama saa moja hivi jamaa angu alikuja akanichukua , tukampitia na mshikaji wake mmoja , na safari ikaanza ya kuelekea nisikokujua kwenye nchi ya maziwa na Asali kama Mwendo wa 80km tukaanza kukwepana na milima ya Lupembe na baada ya muda mshikaji wangu akanambia hapa ndio tunaingia shamba, kwa kuwa lilikuwa shamba jipya lenye milima na milima , na lilikuwa Shamba kubwa kiasi , haaa haaa sio kubwa kama unavyofikiria ww ila ni zaidi ya hekari 400+ Virgin land , hapo hapo nikaanza udadisi wangu na kuanza kukumbuka nilivyokuwa nafundishwa na Maprofesa wangu enzi hizo nasoma pale SUA ,
Nilichoshangaa ni nn?
Katika udadisi wangu niligundua kuwa ile Ardhi haikuwahi kulimwa , mimea iliyoota maeneo Yale iliashiria rutuba ya ajabu iliyoko katika udongo ule , hali ya hewa na baadhi ya vitu vilionyesha kuwa eneo lile linapata mvua kubwa sana kwa mwaka tatribani 2300mm per yr
Organic matter layer ya Ardhi ile ni zaidi 40cm,
Nilichoshangaa zaidi ni pale nilipoenda ndani ya Shamba zaidi na kuona kuwa kuna chanzo kizuri cha maji , nilitamani niende kwetu Rombo niwachukue wale wazee niwalete pale kwa sababu kule sijawahi kuona kitu kama kile .
Bhasi nikaendelea na utafiti wangu nikagundua vitu vingi zaidi katika Ardhi ile na baada ya kukaa na kuangalia milima ikishangaa ujio wetu na muda ulikuwa umeenda , tukafanya baadhi ya kazi pale na kuanza kurudi
Ninachotaka kusema ni kwamba
Don't limit your mind to think
Seed and not diamond will make Africa great
Wekeza vzr kwenye kilimo
Uzi utakao fuata nitawaeleza katika hyo Ardhi ni nini kimepandwa na kinawezaje kumlipa Mkulima tena bila stress , najua utafikiri ni miti ya mbao lakini sio kweli ....stay tuned
Jumapili njema wana jamvi
Wazee wa kulwenda kwao.mara mija kwa mwaka hata akae njimbe miaka mia atakwambia baridi lipo moshi huku hamna kitu,pesa ipo moshi huku hamna kitu ila ukimuuliza mbona hukubaki moshi atakwambia huku nimekuja kutafutaHali ya hewa ya njombe ni zaidi ya ulaya!ukanda ule wamebarikiwa sana