Sikuamini nilivyofika Njombe, kumbe Tanzania hii kuna sehemu kama hizi?

Kuna pahala Mbeya panaitwa Rungwe broo, mwaka mzima ni kijani. Vyanzo vya maji kibao
Ni kweli nako kuko vizuri nilifika kule kuna hawa jamaa wa gesi, nikafika kuna halmashauri mpya nimeisahau jina iko huko mbele ya Rungwe milimani
 
Umenikumbusha Kate, huko Sumbawanga , kuna watawa wa Benedictine wanakaa Abasia ya Mvimwa , wale jamaa wamewekeza kwenye kilimo hakuna mfano , maji ya kutosha , ardhi nzuri etc . Nilijifunza mengi sana kwa wale watawa aisee.
 
Ukanda huo umebarikiwa sana, ujue kuna sehemu zina Ardhi nzr kiasi kwamba zikitumika vzr lazma mafanikio yawepo, unaaenda sehem kipindi kama hiki cha kiangazi unakuta mimea yote ya Kijani but wazawa ni masikini

Nabaki na maswali mengi sana
Kama ukiwa na dhahabu kisha hauna akili bado ni ufukara tu
 
nimekumiss Lasway.Jr !yeah huko njombe nchi ya asali nami nimefika jaman ni kuzuri maparachichi na mazaga zaga kibao yanastawi vizuri mnooooo ! safi sana kwa kazi yako aisee !sema mbali duh
Hivi mpaka leo duniani kuna sehemu ni mbali?! Nadhani ni uwezo tu mdogo ila hakuna mbali. Wazungu wasingekuja huku kutubanabana
 
hayo ndo mambo ya msingi asee!! sio kila siku vijana kujadili mambo ambayo hayana hata faida kwetu, bado tuna ardhi kubwa ambayo ni idle, tutafuteni fursa popote ndani ya ardhi ya Tanzania yetu yenye amani na upendo.
Sure...kuna la kujifunza kwenye mijadala ya namna hii.
 
Very innocent and genuine comment.
Nahisi umewahi kujihusisha na uwekezaji ktk kilimo kwa jinsi ulivyo changia maoni yako.
Tembelea Makete uone jinsi tulivyobarikiwa kuku wanakula Apple's maana hakuna wakuzila,tunaomba mwekezaji atujengee kiwanda ili tusindike
 
Tembelea Makete uone jinsi tulivyobarikiwa kuku wanakula Apple's maana hakuna wakuzila,tunaomba mwekezaji atujengee kiwanda ili tusindike
Sasa mkuu kwanini usiweke kwenye maboksi, pakiza kwenye fuso uyalete huku Dar?
Utajiri huo mkuu.
 
Tembelea Makete uone jinsi tulivyobarikiwa kuku wanakula Apple's maana hakuna wakuzila,tunaomba mwekezaji atujengee kiwanda ili tusindike
Wewe uko makete? Apples mnalima varieties gani? Mimi nahitaji miche, naweza kupata huko?
 
Kwa mikoa niliyopita nadhani hakuna sehemu isiyofaa kwa kilimo

Kwa mfano watu wanasema singida kuna Ukame ila kuna maeneo kuanzia kinampanda kuelekea barabara inayokwenda hydom
Kuna ardhi kule siyo mchezo

Ukirudi Iringa nako ni balaa tupu

Njombe ndiyo usiulize,
Mbeya nako balaa kabisa

Pwani nayo japokuwa maeneo mengi yana maji ila bado panalimika

Morogoro huko ukipita mbingu katikati huko mpaka mgololo ni neema tupu.

Ukihitaji uwekezaji tenga bajeti ya kutembea
 
theoretical kilimo ni rahis na kinalipa mno
practical kilimo ni gamble nilikaa njombe nikaamua kujiingiza kwenye kilimo cha viazi aisee kama unategemea maisha yako yote mule utakufa na stress nashukuru nilikua mfanyakaz so nilikua nalima kutengeneza extra income misimu kama miwili nilikula hasara mpaka nikaja kukimudu haikua rahisi kama watu wanabohisi
pia nilikua na lecture wangu wa agriculture UD wa economics third watanielewa
alichukua heka za kutosha 100+ aliambulia hasara mpaka leo hana hamu na kilimo ingawa anafundisha hilo somo
 
Katika mizunguko yangu ya kazi nilitoka Morogoro nikaenda Mbeya kufanya shughuli zangu za kilimo hasa umwagiliaji, basi nikiwa Mbeya pale kwa kuwa mimi ni mdadisi nitampigia jamaa yangu mmoja ambae ni mwenyeji wa Mbeya pia ni Mkulima, duh jamaa mcheshi sana na ni mshikaji sana japokuwa ni msomi mkubwa na mfanyabiashara

Basi akanambia njoo huku Njombe,jioni ile nikapanda gari kuelekea huko, nilipofika nikakutana na jamaa ang mmoja niliesoma nae chuo akanipokea na akawa mwenyeji wangu.
Nilipompigia jamaa angu huyu Mkulima akanambia bado hajafika mjini ndio anatoka shamba, kumbuka hapo ni saa nne usiku.

Kesho yapo ikawa asubh , baridi ilikuwa kiasi japokuwa mwenyeji wangu alinambia ni wakati wa joto kwa sasa haaa haaaa Njombe kama ulaya vile

Kama saa moja hivi jamaa angu alikuja akanichukua , tukampitia na mshikaji wake mmoja , na safari ikaanza ya kuelekea nisikokujua kwenye nchi ya maziwa na Asali kama Mwendo wa 80km tukaanza kukwepana na milima ya Lupembe na baada ya muda mshikaji wangu akanambia hapa ndio tunaingia shamba, kwa kuwa lilikuwa shamba jipya lenye milima na milima , na lilikuwa Shamba kubwa kiasi , haaa haaa sio kubwa kama unavyofikiria ww ila ni zaidi ya hekari 400+ Virgin land , hapo hapo nikaanza udadisi wangu na kuanza kukumbuka nilivyokuwa nafundishwa na Maprofesa wangu enzi hizo nasoma pale SUA ,

Nilichoshangaa ni nn?
Katika udadisi wangu niligundua kuwa ile Ardhi haikuwahi kulimwa , mimea iliyoota maeneo Yale iliashiria rutuba ya ajabu iliyoko katika udongo ule , hali ya hewa na baadhi ya vitu vilionyesha kuwa eneo lile linapata mvua kubwa sana kwa mwaka tatribani 2300mm per yr
f8e30fe5a8f17a71a09ce3f3cca203a6.jpg


Organic matter layer ya Ardhi ile ni zaidi 40cm,
Nilichoshangaa zaidi ni pale nilipoenda ndani ya Shamba zaidi na kuona kuwa kuna chanzo kizuri cha maji , nilitamani niende kwetu Rombo niwachukue wale wazee niwalete pale kwa sababu kule sijawahi kuona kitu kama kile .
Bhasi nikaendelea na utafiti wangu nikagundua vitu vingi zaidi katika Ardhi ile na baada ya kukaa na kuangalia milima ikishangaa ujio wetu na muda ulikuwa umeenda , tukafanya baadhi ya kazi pale na kuanza kurudi

Ninachotaka kusema ni kwamba
Don't limit your mind to think
Seed and not diamond will make Africa great
Wekeza vzr kwenye kilimo
Uzi utakao fuata nitawaeleza katika hyo Ardhi ni nini kimepandwa na kinawezaje kumlipa Mkulima tena bila stress , najua utafikiri ni miti ya mbao lakini sio kweli ....stay tuned
Jumapili njema wana jamvi
Mkuu salama,

Mbona hapo kama kijijini kwetu Mfiriga Lupembe, na juzi juzi lilipita doser likaangusha mti wangu pale kilimani, mbona kama ndio hapo? Hata hivyo, karibu sana kwetu Mfiriga.
 
Hali ya hewa ya njombe ni zaidi ya ulaya!ukanda ule wamebarikiwa sana
Wazee wa kulwenda kwao.mara mija kwa mwaka hata akae njimbe miaka mia atakwambia baridi lipo moshi huku hamna kitu,pesa ipo moshi huku hamna kitu ila ukimuuliza mbona hukubaki moshi atakwambia huku nimekuja kutafuta
Huwa hawaeleweki hawa
 
Back
Top Bottom