Sikuamini nilivyofika Njombe, kumbe Tanzania hii kuna sehemu kama hizi?

Challenge hiyo hasa KUCHOMEWA MAENEO ya hizo TAASISI waisemeaje kiongozi
Inadaiwa kwamba wao ndiyo walikuwa wanaratibu hiyo michezo kwa ajili ya kuwaandalia maeneo hao wawekezaji.
Kule ardhi inakuwa ni ya kijiji sasa kuna watu wanamili ardhi kimila na ukiomba wakuuzie wanakataa kwasababu ni eneo la vizazi na vizazi; Kuondoa hiyo changamoto ya kunyang'anya ardhi viongozi wanaamua kuchoma moto tu ili kesho uliueze kwa bei mbaya. Utakula hasara pale unapokuwa umepanda miti.

Kinachofanya watu wastuke ni kwamba viongozi wengi wakubwa wa awamu ya nne wana mashamba makubwa sana eneo lile lakini moto huwa haufiki kwenye mashamba yao hata siku moja.

Kuja siku Mzee moja kiongozi wa kijiji kile ndiyo akanisumulia ambavyo watu huwa wanatumwa kuratibu huo uharibifu. Nikaishia kusikitika tu....Wao ndiyo wahusika hivyo sidhani kama wanaweza kusaidia chochote kile
 
Kwa kweli umenishawishi niangalie kwa ukaribu yaani ni neema tupu
Ila acha niweke na tupicha maana watu tunapenda uhalisia zaidi kuliko maandishi pekee
Na shingopana waliishi huko miaka mingi iliyopita
Yaani huko umenishawishi niende likizo
c2b0662a20908b70bc9c5d246238217b.jpg
4183c1cad008bf99d6162966981ff20c.jpg
b4182dec1c3a475e37a0ce58c5f07236.jpg
2e9f4a06735c022bf00ccc06222f5361.jpg
a59d8933cc0f98c56e711f7163f513c2.jpg
 
Mkuu Njombe cha mtoto sana mimi nafanya kilimo sehemu moja inaitwa Kidabaga iko Iringa huko. Ni balaa sana na hali ya hewa ni kama Ulaya, zamani Mahindi walikuwa hawapandii mbolea.

Sema tunapana vikumbo na makampuni makubwa kama New Forest na wale wa One Acre Fund. Wanamiliki maeneo makubwa sana na Raisi Kikwete aliwapa tu; Inafika kipindi wananyanyasa wazawa na kuchoma mashamba yao ya miti kwa maksudi pindi ukikataa kuwauzia.

Nawashauri vijana watembee na kuwekeza huko. It is a nice place to invest: jaribu kwenda kufanya utafiti mkuu

NB: Kuna vibarua wengi sana wa bei nafuu na Wahehe wengi ni watu waaminifu sana endapo utawapa stahiki zao kwa wakati.
Ukanda huo umebarikiwa sana, ujue kuna sehemu zina Ardhi nzr kiasi kwamba zikitumika vzr lazma mafanikio yawepo, unaaenda sehem kipindi kama hiki cha kiangazi unakuta mimea yote ya Kijani but wazawa ni masikini

Nabaki na maswali mengi sana
 
Kwa kweli umenishawishi niangalie kwa ukaribu yaani ni neema tupu
Ila acha niweke na tupicha maana watu tunapenda uhalisia zaidi kuliko maandishi pekee
Na shingopana waliishi huko miaka mingi iliyopita
Yaani huko umenishawishi niende likizo
c2b0662a20908b70bc9c5d246238217b.jpg
4183c1cad008bf99d6162966981ff20c.jpg
b4182dec1c3a475e37a0ce58c5f07236.jpg
2e9f4a06735c022bf00ccc06222f5361.jpg
a59d8933cc0f98c56e711f7163f513c2.jpg
Nenda mkuu , najua hutarudi iv iv unaweza kufanya kitu kwa ajili ya watoto wako
 
Tuna kawimbo ketu watu wa njombe na upangwa. Kanaenda


Upangwa\njombe nchii nzuri kuliko Zote,mashamba na bustaani twalima soote twachunga ngombe zeetu huu mlimani,ni nani ajuaaye uzuri wake huo huooo huooo huko huooo njombe\upangwa nitakaa

Karibu khinyumba kaka
 
nimekumiss Lasway.Jr !yeah huko njombe nchi ya asali nami nimefika jaman ni kuzuri maparachichi na mazaga zaga kibao yanastawi vizuri mnooooo ! safi sana kwa kazi yako aisee !sema mbali duh
Asante, mbali mbinguni, uwekezaji ni popote , tamani siku moja watoto wako waje waseme baba/mama aliona mbali sana haaa haaa you must have your children brain for bow for them
 
Juzi Rais alisema, kuzaliwa Tanzania ni fursa. Watu wakaanza kumponda
Ilinikera siku moja nikiwa kwa hao ndugu zetu, kijana mmoja akaniuliza "kwa nini Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini sana duniani wakati mna raslimali nyingi" nilikereka sana! Nikamwambia kuwa Madini ya Tanzanite kwa mfano huwa yanapatikana Tanzania tu! Nikafungua site hii: http://allafrica.com/stories/201405120444.html na hii Tanzanite Gemstone in Jaipur, Rajasthan | tanzanite stone Suppliers, Dealers & Retailers in Jaipur hakunighasi tena
 
Katika mizunguko yangu ya kazi nilitoka Morogoro nikaenda Mbeya kufanya shughuli zangu za kilimo hasa umwagiliaji, basi nikiwa Mbeya pale kwa kuwa mimi ni mdadisi nitampigia jamaa yangu mmoja ambae ni mwenyeji wa Mbeya pia ni Mkulima, duh jamaa mcheshi sana na ni mshikaji sana japokuwa ni msomi mkubwa na mfanyabiashara

Basi akanambia njoo huku Njombe,jioni ile nikapanda gari kuelekea huko, nilipofika nikakutana na jamaa ang mmoja niliesoma nae chuo akanipokea na akawa mwenyeji wangu.
Nilipompigia jamaa angu huyu Mkulima akanambia bado hajafika mjini ndio anatoka shamba, kumbuka hapo ni saa nne usiku.

Kesho yapo ikawa asubh , baridi ilikuwa kiasi japokuwa mwenyeji wangu alinambia ni wakati wa joto kwa sasa haaa haaaa Njombe kama ulaya vile

Kama saa moja hivi jamaa angu alikuja akanichukua , tukampitia na mshikaji wake mmoja , na safari ikaanza ya kuelekea nisikokujua kwenye nchi ya maziwa na Asali kama Mwendo wa 80km tukaanza kukwepana na milima ya Lupembe na baada ya muda mshikaji wangu akanambia hapa ndio tunaingia shamba, kwa kuwa lilikuwa shamba jipya lenye milima na milima , na lilikuwa Shamba kubwa kiasi , haaa haaa sio kubwa kama unavyofikiria ww ila ni zaidi ya hekari 400+ Virgin land , hapo hapo nikaanza udadisi wangu na kuanza kukumbuka nilivyokuwa nafundishwa na Maprofesa wangu enzi hizo nasoma pale SUA ,

Nilichoshangaa ni nn?
Katika udadisi wangu niligundua kuwa ile Ardhi haikuwahi kulimwa , mimea iliyoota maeneo Yale iliashiria rutuba ya ajabu iliyoko katika udongo ule , hali ya hewa na baadhi ya vitu vilionyesha kuwa eneo lile linapata mvua kubwa sana kwa mwaka tatribani 2300mm per yr
f8e30fe5a8f17a71a09ce3f3cca203a6.jpg


Organic matter layer ya Ardhi ile ni zaidi 40cm,
Nilichoshangaa zaidi ni pale nilipoenda ndani ya Shamba zaidi na kuona kuwa kuna chanzo kizuri cha maji , nilitamani niende kwetu Rombo niwachukue wale wazee niwalete pale kwa sababu kule sijawahi kuona kitu kama kile .
Bhasi nikaendelea na utafiti wangu nikagundua vitu vingi zaidi katika Ardhi ile na baada ya kukaa na kuangalia milima ikishangaa ujio wetu na muda ulikuwa umeenda , tukafanya baadhi ya kazi pale na kuanza kurudi

Ninachotaka kusema ni kwamba
Don't limit your mind to think
Seed and not diamond will make Africa great
Wekeza vzr kwenye kilimo
Uzi utakao fuata nitawaeleza katika hyo Ardhi ni nini kimepandwa na kinawezaje kumlipa Mkulima tena bila stress , najua utafikiri ni miti ya mbao lakini sio kweli ....stay tuned
Jumapili njema wana jamvi
Mkuu lupembe nmetoka juzi tu kijiji kinaitwa mfiriga so mchezo ardhi kule ina rutuba so mchezo mi nlienda kutafuta mashamba ya kupanda miti ya mbao
 
Back
Top Bottom