Intellect
Member
- Apr 1, 2011
- 34
- 20
Ni dhahiri kwamba siku za muungano kati ya Tanzania Bara na Visiwani (Zanzibar) siku zake zina hesabika kwa maana hata hao wanaoutetea ukiwaambia wakupe faida zake utasikia " huu muungano wetu tumerithishwa na waasisi wa taifa hili" mara "amani" mara "watu wameoana" ili mradi wao waendelee kula matunda na wananchi wanaambulia kero tu.
Ukitizama kwa undani faida za muungano ni chache na nyingi hazina tija. Karume Angekua hai angeufutilia mbali na kama hoja ni kuoana mbona watu wameoa ulaya na sisi hatuna muungano na nchi za ulaya! Wazanzibari wanafikiri wananchi wa bara wanafaidi, wa bara wanafikiri waunguja wanafaidi kumbe ni watu wachache tu wanaoshikilia uongozi serikalini ndio wanafaidi na ndio maana ukiwahoji wananchi wa zanzibar watasema hawautaki, baraza la wawakilishi haliutaki ila viongozi wenye nyadhifa katika derikali ya muungano kama wabunge na mawaziri kutoka zanzibar pamoja na wana CCM wenye fikra mgando wao ndio kama wana hati ya muungano!
Binafsi sina tatizo na uvunjika kwa muungano, uvunjike tu, tatizo lango ni baada ya kuvunjika, je tanzania bara italirudia jina la tanganyika au itaitwa vipi?
Ukitizama kwa undani faida za muungano ni chache na nyingi hazina tija. Karume Angekua hai angeufutilia mbali na kama hoja ni kuoana mbona watu wameoa ulaya na sisi hatuna muungano na nchi za ulaya! Wazanzibari wanafikiri wananchi wa bara wanafaidi, wa bara wanafikiri waunguja wanafaidi kumbe ni watu wachache tu wanaoshikilia uongozi serikalini ndio wanafaidi na ndio maana ukiwahoji wananchi wa zanzibar watasema hawautaki, baraza la wawakilishi haliutaki ila viongozi wenye nyadhifa katika derikali ya muungano kama wabunge na mawaziri kutoka zanzibar pamoja na wana CCM wenye fikra mgando wao ndio kama wana hati ya muungano!
Binafsi sina tatizo na uvunjika kwa muungano, uvunjike tu, tatizo lango ni baada ya kuvunjika, je tanzania bara italirudia jina la tanganyika au itaitwa vipi?