Siku ya wanawake duniani - Tanzania: Nani anawajua wapigania uhuru hawa wanawake?

Kipala nimeeleza wapi nimepata picha hii na nyingine labda hukusoma uzi toka mwanzo. Ally Sykes alinikutanisha na Jim Bailey aliyekuwa na mswada wa kitabu cha picha kuhusu Baba wa Taifa. Bailey akaniomba nifanye uhariri wa kitabu chake. Huyu Bailey alikuwa na gazeti lake Drum likichapwa Johannesburg katika miaka ya 1950s. Katika kazi hii ndipo nilipopata picha hii ya 1955. Kulia ni Bi. Chiku Kisusa (Mama Sakina), Bi. Titi Mohamed, huyo wa tatu jina sina wa nne Mwalimu Julius Nyerere wa tano jina sina na wa sita ni Bi. Tatu bint Mzee. Bailey akiniomba pia baada ya kukihariri kitabu nimtafutie publisher. Mimi nikamjulisha Bailey kwa Walter Bgoya wa Mkuki na Nyota ambae ni rafiki yangu wa miaka mingi. Yeye ni publisher wa sifa na kitabu kikachapwa - The Story of Julius Nyerere of Tanzania. Picha hii ni moja picha kutoka Bailey African Collection. Ninazo picha nyingine mkipenda naweza kukuwekeeni hapa pamoja na historia zake.
Mungu akuweke Shekhe wangu,Mwalim wangu wa historia ya kweli ilotukuka.... Allah atakulipa inshaallah Maandsh yko hayatapotea buree
 
Mungu akuweke Shekhe wangu,Mwalim wangu wa historia ya kweli ilotukuka.... Allah atakulipa inshaallah Maandsh yko hayatapotea buree
Alwayz...
Amin.

Ngoja nikupe kisa kidogo cha sahib wangu Jim Bailey.

Mwka wa 2000 niko katika ndege naelekea Johannesburg nimekaa na Mzungu
mmoja tukaanza mazungumzo.

Akaniuliza nakwenda wapi.
Nikamwambia kuwa safari yangu khasa ni Manzini Swaziland na kisha J'burg.

Akaniambia unakwenda Jburg kufanya nini?
NIkamwambia kutembea nina rafiki yangu nataka nikamtembelee.

Nikamtajia jina, ''Jim Baliey.''
Akaniuliza, ''Wewe unafahamiana na Bailey?''

Nikamjibu, ''Naam.''

Akanipa pole kisha akasema, ''Mimi Bailey ni jirani yangu na tumemzika mwezi
uliopita.''
 
Back
Top Bottom