Chinga One
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 11,433
- 12,282
===================
Leo nimeona nitumie haki yangu ya kikatiba ya uhuru wa kutoa maoni.
Nitangulie kwa kukumbusha kama tujuavyo mapenzi ya kweli ni ngumu sana kuyahamisha toka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine hivyo basi inapotokea watu wakapendana kwa dhati ni kuwaombea wafike hatua ya kuoana na kuishi pamoja, yaani ni kama shabiki wa timu ya mpira ambapo hata akisema naihama timu lakini bado moyo wake utakuwa kwenye timu yake ya mwanzo.
Vijana Diamond & Wema ni majina makubwa na brands kali sana hapa nchini. Hawa walipendana kwa dhati lakini hawakufanikiwa kufika mbali kutokana na sababu mbalimbali lakini sababu inayotajwa zaidi ni tabia zisizofaa kati yao. Kila mmoja alikuwa macho juu.
Alicho-post Diamond Siku wa Wanawake Duniani
View attachment 1381859
Nimeamua niseme sio vibaya wakiona inafaa wasione haya kurudiana na waanzie pale walipoishia.
Hawa vijana kiukweli wanateseka nafsini kila mmoja kwa style yake. Post ya leo ya diamond kwa siku ya wanawake ni ushahidi usiotia shaka kwamba wawili hawa bado nafsi zao hazijatengana. Ninyi mna maoni gani?