Siku ya Sheria: No mention of Tundu Lissu!, Je ni amesahaulika tu kutajwa, amepuuzwa au ameepukwa?!.

Huu mkasa wa Tundu Lissu sio bure inaonesha inasumbua watu sana hasa wale watuhumiwa wakuu kwani kutuhumiwa ni kutuhumiwa tu hata uwe na cheo kikubwa namna gani.
 
Wewe ni ng'inyang'inya
Ptro Petro:
Naona umetegwa na mtego dhaifu nawe umetegeka kweli kweli.
Hukupaswa kufikia kujibizana vibaya na wakosoaji wako, ungeomba radhi kwa kueleweka vibaya au hata kunyamaza ili kutetea hadhi yako.
Nilijizuia kusema lolote juu yako hadi nilipoona uvumilivu umaniishia.
Kitabu cha Yakobo kinasema, mtu akipungukiwa na hekima na amwombe Mungu.
Petro omba hekima
 
Pascal Mayalla Bila shaka ameepukwa. Na kumuepuka Mhe. Tundu Lissu ni kazi ngumu sana. Waliomchagua wanamtambua na ni kuhakikishie watamchagua tena hata bila kuwepo. Mhe. Tundu Lissu ni nguzo muhimu kwa demokrasia ya kweli ya nchii. Get well soon brother, Hon. Tundu Lissu.
 
Wanasheria wakiongea huwa wana quote vifungu vya sheria ulitaka wamu quote Lisu kwani yeye ni kifungu cha sheria
Wewe M TAG ni Yuda Iskarioti.
Hufai hata kuitwa Mkristo, kwa kifupi wewe u mnafiki na kilaza.
Tofauti za kiitikadi zina ukomo.
Nje ya siasa Watanzania ni ndugu, lkn ninyi mmegeuza siasa kuwa ni uadui hadi kufikia kutakiana mabaya hadi vifo.

Mnaharibu nchi yetu nzuri kwa midingi mibovu ya chuki.
 
Mimi nilitegemea kuwa wewe ni Jasiri kumbe BOGA kabisa, Taja aliyehusika kwenye tukio la Lisu. Mbona umefyata mkia ? Mbilinyi yeye alimgonga na gari mtoto Yatima tena kwenye Zebra Crossing na kumuua, mbona hili hauliongelei ?, badala yake unashupalia la Lisu kupigwa risasi, Je huyo mtoto tena Yatima kugongwa na gari kwenye Zebra crossing na kumuua lenyewe mbona huongelei ?
Mimi nilitegemea kuwa wewe ni Jasiri kumbe BOGA kabisa, Taja aliyehusika kwenye tukio la Lisu. Mbona umefyata mkia ? Mbilinyi yeye alimgonga na gari mtoto Yatima tena kwenye Zebra Crossing na kumuua, mbona hili hauliongelei ?, badala yake unashupalia la Lisu kupigwa risasi, Je huyo mtoto tena Yatima kugongwa na gari kwenye Zebra crossing na kumuua lenyewe mbona huongelei ?
Nadhani aliyemgonga yule mtoto na kumuua ni dereva Wa mbilinyi wala sio mbilinyi mwenyewe.
 
Wanabodi,

Leo nimepata fursa kuangalia sherehe za maadhimisho wa siku ya sheria zilizokuwa zikitangazwa live na TBC. Chama cha wanasheria ni mdau muhimu wa maadhimisho haya ambayo huhutubiwa na rais wa chama hicho. Kwa vile rais wa TLS ni Tundu Lissu, na ameshindwa kuhudhuria kutokana na kuwa mgonjwa, jina la Tundu Lissu, halikutajwa popote!. Swali la kujiuliza, ni kutotajwa huku kutokana na kusahaulika tuu, Lissu amepuuzwa as if he doesn't exist, or ameepukwa kutajwa kwa makusudi?.

Kwenye ratiba ya maadhimisho hayo, kulionyesha kuna mahali rais wa TLS, angepaswa kutoa salamu. Kwa vile rais wa TLS, Mhe. Tundu Lissu, ni mgonjwa kwa shambulio la risasi, aliyekuja kuzungumza nafasi ya rais wa TLS, ni Makamo rais wa TLS, nikitegemea, alipoanza kuzungumza, kwa vile aliyepaswa kuzungumza sii yeye ni rais wa TLS, hivyo anaongea kwa niaba ya rais wa TLS, then, kistaarabu tuu, alipaswa kusema anazungumza kwa niaba ya rais wa TLS ambaye ni mgojwa. Huyu Makamo rais wa TLS, aliposimama kuzungumza, alisimama na kujitaja kuwa anazungumza kwa niaba yake!. Ratiba inasema mzungumzaji ni rais wa TLS, wewe sio rais wa TLS, unasimama kuzungumza badala ya rais wa TLS, ilibidi kumtaja rais wa TLS as an excuse ndipo uendelee!.

Naibu Spika, Tulia Akson, amemuwakilisha Spika ametajwa kuwa yupo anamuwakilisha spika. Naibu DPP ametajwa kumwakilsha DPP, Naibu Mwanasheria Mkuu ametajwa kumwakilisha Mwanasheria Mkuu, kwa nini huyu Makamo rais wa TLS akajitaja yeye ili hali kwenye ratiba aliyeandikwa ni rais wa TLS.

Aliposimama mgeni rasmi, Rais wa Jamhuri ya Muungano, naye katika maelezo yake, akamtaja rais wa TLS na kujikwaa, akamtaja Makomo rais wa TLS.

Huku kutotajwa kabisa kwa rais wa TLS, Tundu Lissu. ni oversight tuu ya kusahaulika, au ni omission kuwa Tundu Lissu asitajwe popote.

Rais katika hotuba yake, akatoa pole kwa mhimiliwa mahakama kwa kifo cha Jaji Robert Kisanga ambaye aliishastaafu siku nyingi, kama mtu aliishastaafu siku nyingi na kufariki, mhimili huu unapewa pole, vipi kuhusu shambulio la rais wa TLS ambaye hadi sasa anauguza majereha ya shambulizi, hatajwi popote, wala hata kumtakia uponywaji wa haraka!.

Amini usiamini, kama Tundu Lissu, angekufa kwa shambulio lile, hotuba ya TLS ingemtaja, na kile aliyehutubia, angetoa pole kwa TLS kwa kuondokewa na rais wake, lakini kwa vile Lissu yuko hai, amenusurika, hadi marehemu wastaafu wanapewa pole, lakini walio hai wanaohitaji kuombewa tuu uponyaji wa haraka, wamesahaulika, kama sio kuepukwa!.

Kama huku sio kusahaulika, bali ni kuepukwa, then bandiko hili, ndio taarifa ya awali, kuwa urais wa Tundu Lissu kwenye TLS, unaofikia kikomo miezi miwili ijayo, Mwezi April, 2018, wanasheria watakutana na kumfuta rasmi kazi Tundu Lussu kama rais wa TLS, na inawezekana kabisa, jina la Tundu Lissu likaingia kwenye kumbukumbu za TLS kuwa Tundu Lissu ndie rais wa TLS ambaye he did almost nothing, tangu achaguliwe, kwa kudumu kwa miazi mitatu tuu TLS, ba baada ya hapo, akashambuliwa, hivyo kumaliza Kipindi chake chote cha urais akiwa hospitalini.

Pamoja na kwamba Tundu Lissu ni mgonjwa na yuko hospitalini, bado yeye ndie rais halali wa TLS!. Kuumwa hakumfanyi Tundu Lissu asiwe rais wa TLS, hivyo he was worth mentioned, na kutakiwa uponyaji wa haraka!.

Get Well Tundu Lissu, pole sana, umesahaulika mapema!.

Paskali

Was that so important kumtaja Lissu kwenye hiyo hadhira. Hakukuwa na mambo mengine ya msingi kwa taifa zaidi ya kutajwa kwa Lissu? Je yaliyotamkwa pale hayakuwa na uzito uliokamilika kiasi kwamba kutajwa kwa Lissu kungeyakamilisha?

BTW wewe umemtaja ngoja tusubiri tuone italeta tija gani kwenye hii siku ya sheria.
 
Waliokwapua Richmond umewasahau

Wewe waweke,maana according to CAG hakuna pesa iliyopotea hapo,ila wanajuana wakuu wenyewe.Cha msingi waweza ongezea kama nimesahau kuweka.

Cha msingi msifagie nyumba uchafu mkauweka chini ya kitanda kwa maana uvundo bado utakuwepo tu
 
Unfortunately he has not been mentioned by TLS, but we should all remember that TL is just a drop in the ocean called Tanzania let's not hype him beyond his wothness to the Nation.
 
Tangu nianze kukusoma hakika leo umetoa mchango bora kabisa.

Akhsante kwa pongezi zako ila nadhani utakuwa ni ' Mgeni ' Kwangu kwani nilishasema humu siku nyingi tu kwamba japo Mimi ni Mshabiki na Mpenzi wa CCM ( Ingawaje Kadi ya Chama bado sina ila nipo mbioni kuishughulikia niipate ) ila sitokuwa ' Mnafiki ' kwa Kuisifia CCM hata kama naona ' wamekosea / wamekengeuka ' bali nitawasema ili wajitathmini na wajirekebishe lakini pia nilishasema kwamba japo napenda ' Changamoto ' ambazo Vyama vya Upinzani nchini hasa vya CHADEMA na CUF dhidi ya Chama Tawala cha CCM ila hata wao pia ( CHADEMA na CUF ) nao wakienda ndivyo sivyo basi kama kawaida yangu sitonyamaza ' Kuwananga / Kuwasema '.

Siku zote ' msimamo ' wangu wa Kisiasa hasa hizi za Tanzania nitabakia kuwa ' neutral ' na nadhani siku zote GENTAMYCINE nipo hivyo humu na ndiyo maana unaweza kuona nakubalika na Watu wote wawe wana CCM wenzangu na hata ' Watani ' zangu CHADEMA na CUF. Hata CCM, CHADEMA na CUF wakifanya jambo chanya / jema mbele ya Jamii ya Kitanzania basi nitakuwa wa Kwanza kuwapa Sifa / Kongole zao bila hiyana.

Tanzania Kwanza, Vyama vya Siasa na Siasa baadae na hata ' tugombane ' vipi ila Sisi sote tutabaki kuwa Watanzania tu.
 
Watanzania tunapomwomba Mungu kutupa kiongozi tuwe tunaangalia sana. Tulisema Tanzania inatakiwa kuongozwa na "dikteta"

Tuwe tunasema Tanzania inatakiwa kuongozwa na kiongozi mwenye hekima na mwenye hofu ya Mungu. Inatosha

Haiwezekeni unapenda kusifiwa tu hata kwenye madudu.

Ukiwa na mfumo mzuri vitu vingine vinajipanga yenyewe hata hiyo teua tengue ingepungua

Get well soon Tundu Lissu
 
Andiko lako limenigusa sana.. Zaidi hapo uliposrma kama angekufa basi tungeona jana watu wanagalagala kutoa pole na maombi kede kede Mungu amlaze mahali pema, lakini yupo hai (labda kwa vile baadhi hawakupenda aendelee ku-survive) basi wamemsahau kabisa.
Nasubiria karma ifike kwenye address zao kama ambavyo Paskali umekuwa ukisisitiza kuwa karma has got everyone's address....
 
Ndio maana tuna mashaka sana na shambulio lake jamani, mpinzani sio adui iweje umtaje marehemu wa miaka hiyo ukamwacha kumtaja aliyeko ila tu kashindwa kuhudhuria kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake? Hapana si kawaida there is something behind ila kama huyu Mungu tuliemlilia juu ya shambulio lake na akamnusuru umauti basi ataendelea kumlinda dhidi ya maadui na wenye nia mbaya juu yake!
 
Pascal Mayalla Sitaandika sana katika hili ila ni lazima uelewe ya kuwa watu wanajua kusoma alama za nyakati.Mtu aliye mbele yako ana madaraka makubwa na ana maamuzi ya haraka.Kwa nini uiharibu hiyo shughuli kwa kutaja nguo ya ndani ya mkweo?
TLS hawakuwa wajinga,walijua wako wapi na nani.
 
Back
Top Bottom