EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,091
Hii ni siku moja ambayo naamini kwa wale ambao wamekwishapitia siku hii wanaweza kutupa uzoefu wao kidogo wa namna inavyokuwa. Kwa mfano, siku hizi ndoa nyingi zinafanyika wakati binti ni mjamzito so inakuwa kama jamaa kalazimishwa vile.....so wanawake huwa wanahisi vipi hasa ikitokea kwa bahati mbaya bwana harusi akachelewa kufika kanisani, au wanaume huwa mnajihisi vipi pale bi harusi anapochelewa kufika kanisani au hata kuwa na mawazo ya je kama asipotokea au akitokea akasema "hapana"
Nimezungumzia makanisani kwasababu mfumo wa ndoa za kiislam uko tofauti kidogo na huu wa kikristo wa kusubiriana church. Lakini hata zile za kiislam huwa unahisi vipi pale anapokuwa kaenda kuulizwa mwenzio na we kusubiri jibu kama amesema ndio au hapana?
Kwenye reception party huwa mnakuwa na feelings gani? Maana kuna wakati kama ni mwanaume wanakuja vidumu vyako au kama ni mwanamke the same, huwa inakuwaje katika kipindi kile cha masaa machache ya reception party?
Wale ambao hawajaoa/kuolewa mnapenda siku yenu hii iweje?
Nimezungumzia makanisani kwasababu mfumo wa ndoa za kiislam uko tofauti kidogo na huu wa kikristo wa kusubiriana church. Lakini hata zile za kiislam huwa unahisi vipi pale anapokuwa kaenda kuulizwa mwenzio na we kusubiri jibu kama amesema ndio au hapana?
Kwenye reception party huwa mnakuwa na feelings gani? Maana kuna wakati kama ni mwanaume wanakuja vidumu vyako au kama ni mwanamke the same, huwa inakuwaje katika kipindi kile cha masaa machache ya reception party?
Wale ambao hawajaoa/kuolewa mnapenda siku yenu hii iweje?