MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Naomba kuuliza maswali mawili tu!
1) Leo ni kilele cha Siku ya Kimataifa ya Wanawake (International Women's Day). Je, Siku ya Kimataifa ya Wanaume ipo? Na kama ipo inaadhimishwa lini? Na kama haipo ni kwa sababu gani?
2) Nchini Tanzania kuna sheria inayoitwa Sexual Offences Special Provisions Act (SOSPA), ambayo inahusiana na masuala yote ya udhalilishwaji, unyanyasaji na makosa mengine yanayotokea, hususan wanapoathirika ni wanawake. Ni nadra sana kusikia wanaume wakiathirika na unyanyasaji au udhalilishwaji wa kijinsia.
Mara nyingi wanaoathirika huwa katika ndoa, lakini inapotokea anayeathirika ni msichana ambaye ananyanyaswa na mwenza (boyfriend) wake, na haswa kama mwenza huyo ni mtu mwenye uwezo kifedha, mara nyingi anayenyanyaswa huwa na hofu kiasi cha kumkimbia na hata kuhama nchi.
Kimenitokea kisa ambacho nimekutana na binti mdogo, miaka 24, ambaye hata chuo kikuu amesitisha masomo yake kwa sababu ya unyanyaswaji anaokutana nao kutoka kwa boyfriend wake huyo, ambaye analazimisha mapenzi... anatamba kwamba ana uwezo mkubwa, amewaweka maofisa wa polisi mfukoni, na kadhalika!
Je, kuna sheria gani ya kuwabana watu kama hawa? Au nini kifanyike kuwasaidia dada zetu wasinyanyasike?
./mwana wa haki
1) Leo ni kilele cha Siku ya Kimataifa ya Wanawake (International Women's Day). Je, Siku ya Kimataifa ya Wanaume ipo? Na kama ipo inaadhimishwa lini? Na kama haipo ni kwa sababu gani?
2) Nchini Tanzania kuna sheria inayoitwa Sexual Offences Special Provisions Act (SOSPA), ambayo inahusiana na masuala yote ya udhalilishwaji, unyanyasaji na makosa mengine yanayotokea, hususan wanapoathirika ni wanawake. Ni nadra sana kusikia wanaume wakiathirika na unyanyasaji au udhalilishwaji wa kijinsia.
Mara nyingi wanaoathirika huwa katika ndoa, lakini inapotokea anayeathirika ni msichana ambaye ananyanyaswa na mwenza (boyfriend) wake, na haswa kama mwenza huyo ni mtu mwenye uwezo kifedha, mara nyingi anayenyanyaswa huwa na hofu kiasi cha kumkimbia na hata kuhama nchi.
Kimenitokea kisa ambacho nimekutana na binti mdogo, miaka 24, ambaye hata chuo kikuu amesitisha masomo yake kwa sababu ya unyanyaswaji anaokutana nao kutoka kwa boyfriend wake huyo, ambaye analazimisha mapenzi... anatamba kwamba ana uwezo mkubwa, amewaweka maofisa wa polisi mfukoni, na kadhalika!
Je, kuna sheria gani ya kuwabana watu kama hawa? Au nini kifanyike kuwasaidia dada zetu wasinyanyasike?
./mwana wa haki