Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Kuna kila dalili kwamba Watanzania wameanza kuchoshwa na hii tabia ya Jeshi la Polisi la kupiga watu mabomu na risasi za moto hata mahali ambapo hakuna ulazima na hivyo kupelekea vifo kwa Watanzania wasio na hatia. Kuna msururu mrefu sana wa Watanzania waliouawa na Polisi wakiwa kwenye maandamano,mikutano ya hadhara,chini ya ulinzi au mahabusu!
Matukio ya hivi karibuni ambayo yemehusishwa na mauaji ya kisiasa yamezidi kuchafua rekodi za Jeshi la Polisi na hasa baada ya kumwua mwandishi wa habari kule Iringa. Watanzania wamechukizwa sana na tabia hii na kuna tetesi kwamba karibu wataanza kujibu mapigo kutokana na unyama huu.
Ikumbukwe kwamba hawa wanaouawa au kujeruhiwa kwenye maandamano au mikutano ya hadhara mara nyingi imetokea kuwa si wanachama wala wafuasi wa vyama au taasisi husika. Kinachoonekana hapa ni mauaji yanayokuwa yamepangwa makusudi ili kuwazuia,kuwatisha au kuwakatisha watu tamaa kufikia malengo ya kile wanachokikusudia kwenye maandamano husika. Mara zote ambazo mauaji yametokea serikali imekuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua madhubuti za kisheria ili kuzuia hali hii isiendelee. Polis wameua na mwisho wa siku wameishia kupandishwa vyeo au kuhamishwa kutoka kituo kimoja kwenda kingine!
Watanzania wamesha anza kuchoka na wanasema wataanza kuchukua hatua wenyewe kwa kuwashughulikia Polisi wanaohusika na mauaji hayo. Kwa vile Polisi wengi wanaishi uraiani pamoja na familia hizi zinazoasiriwa na mauaji haya zitajibu mapigo huko huko uraiani. Hakuna Mtanzania atakubali kuona Polisi ambaye ni jirani yake akiishi kwa amani na huku akituhumiwa kamwua ndugu yake kwenye maandamano ya CHADEMA bila ya sababu za msingi. Lazima atajibu mapigo tu kama dola itaendelea kumlinda! Polisi hawawezi kujifanya miungu watu wa kutoa roho za watu halafu wao wakaendelea kufurahia maisha kana kwamba wako juu ya sheria. Hili halikubaliki na halitakubalika kwa Tanzania ya sasa na itakayokuja.
Hizo ndiyo salamu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mheshimiwa Nchimbi,IGP Mwema na Makamanda wake wote wa Makao makuu na Mikoani.
Matukio ya hivi karibuni ambayo yemehusishwa na mauaji ya kisiasa yamezidi kuchafua rekodi za Jeshi la Polisi na hasa baada ya kumwua mwandishi wa habari kule Iringa. Watanzania wamechukizwa sana na tabia hii na kuna tetesi kwamba karibu wataanza kujibu mapigo kutokana na unyama huu.
Ikumbukwe kwamba hawa wanaouawa au kujeruhiwa kwenye maandamano au mikutano ya hadhara mara nyingi imetokea kuwa si wanachama wala wafuasi wa vyama au taasisi husika. Kinachoonekana hapa ni mauaji yanayokuwa yamepangwa makusudi ili kuwazuia,kuwatisha au kuwakatisha watu tamaa kufikia malengo ya kile wanachokikusudia kwenye maandamano husika. Mara zote ambazo mauaji yametokea serikali imekuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua madhubuti za kisheria ili kuzuia hali hii isiendelee. Polis wameua na mwisho wa siku wameishia kupandishwa vyeo au kuhamishwa kutoka kituo kimoja kwenda kingine!
Watanzania wamesha anza kuchoka na wanasema wataanza kuchukua hatua wenyewe kwa kuwashughulikia Polisi wanaohusika na mauaji hayo. Kwa vile Polisi wengi wanaishi uraiani pamoja na familia hizi zinazoasiriwa na mauaji haya zitajibu mapigo huko huko uraiani. Hakuna Mtanzania atakubali kuona Polisi ambaye ni jirani yake akiishi kwa amani na huku akituhumiwa kamwua ndugu yake kwenye maandamano ya CHADEMA bila ya sababu za msingi. Lazima atajibu mapigo tu kama dola itaendelea kumlinda! Polisi hawawezi kujifanya miungu watu wa kutoa roho za watu halafu wao wakaendelea kufurahia maisha kana kwamba wako juu ya sheria. Hili halikubaliki na halitakubalika kwa Tanzania ya sasa na itakayokuja.
Hizo ndiyo salamu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mheshimiwa Nchimbi,IGP Mwema na Makamanda wake wote wa Makao makuu na Mikoani.