Siku wananchi wakichoka kunyanyaswa nani atalinda usalama wa Askari Polisi?

STEIN

JF-Expert Member
Aug 29, 2010
1,770
553
Ndugu zangu wanaJF, ninavyofahamu mimi polisi wanatakiwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni zilizopo. Lakini cha kushangaza jeshi hilo limekuwa likitetea maslahi ya CCM na Mafisadi hata kama ni kwa gharama ya kuwapiga risasi wananchi.

Mfano mzuri ni wakati wa uchaguzi ambapo jeshi la polisi na askari wake wamekuwa wakitimiza majukumu yao kwa kuipendelea CCM hata hata kama ni kutofuata sheria na kanuni kama vile kukataa kulinda helicopter aliyokuwa akiitumia Dr. Slaa wakati wa kampeni na kuwaachia wanaCCM wakifanya vurugu kwenye mikutano ya CDM.

Ni jambo la kusikitisha hasa pale unapokuta polisi wanahatarisha usalama na maisha ya mwananchi badala ya kulinda usalama.

Swali langu kubwa ni kwa jinsi tunavyofahamu idadi ndogo ya jeshi hilo ukilinganisha na idadi ya wananchi, Siku wananchi wakichoka kuvumilia je ni nani atalinda usalama wa polisi mitaani? maana tuko tunakaa nao mtaani.

Ushauri wangu kwa jeshi la polisi ni kwamba wafanye kazi zao kwa kufuata sheria na si maagizo ya CCM na serikali yao. Mfano wa jeshi hilo kutotosha hata kuwathibiti wananchi wa mkoa moja upo wazi hata pamoja na silaha zote.

Tumeona juzi tu Arusha ilibidi wachukue askari kutoka mikoa ya Kilimanjaro na Dar na vurugu zilikuwa Arusha mjini tu je ingekuwa mkoa wa arusha wote watu wameandama ingekuwaje.

Askari najua mko humu JF hasa WAKUBWA tafadhali msifanye kazi kwa maagizo ya CCM mtapata matatizo ya kutokaa mtaani vizuri na watoto wenu watanyanyasika.
 
Nawaonea huruma. Siku zao ziko tu karibu

Kama Congresswoman kala shaba, hawa nao watakula beto one day.

Na hivyo tunakaa nao vibanda umiza huku na wengine jioni tunagongana nao mitaani wamepiga ulabu hadi wanaangukia mitaroni, we ngoja ni kuwafanuyia kitu cha mande


Watalipa damu za ndugu zetu wanaowaua bila msingi wowote
 
NewDawnTz said:
we ngoja tutalipa vijana wawapige kitu cha mande
No more, talking actions please. Kwanini utume vijana? Do it urself! Acha maneno matupu,sasa ni muda wa vitendo tu. Tumeongea sana toka 1961,na hakuna faida tuliyoipata. Sasa tuanze vitendo ili tuone matokeo yake.
 
NewDawnTz said:
we ngoja tutalipa vijana wawapige kitu cha mande
No more, talking actions please. Kwanini utume vijana? Do it urself! Acha maneno matupu,sasa ni muda wa vitendo tu. Tumeongea sana toka 1961,na hakuna faida tuliyoipata. Sasa tuanze vitendo ili tuone matokeo yake.

You are right hatutaki kuendela kufanya propaganda, issue ni kama haya ya Arusha yataendelea wajue nchi hii haitakalika.
 
avatar25721_1.gif

avatar28900_2.gif


Hizi avatar zote ni za kimapinduzi lakini je, zinaendana na dhamira na nia zenu??
 
Gharibu bilal yupo serengeti na wanawake wawili katika mapumuziko na gharama zake ni 10m kwa siku . Sasa kaenda na waker wawili hii hatari kwa matumizi makubwa ya fedha wakati wahadhari wanamtaka akajibu maswali udom
 
Wananch msiwe na Hasira sana na Polisi, kwanza nao ni wananchi wenzetu, wanachofanya ni kutekeleza maaigizo ya watawala kama walivyoapa kuwa watii kwa Rais.

Mbona mnasahau kwamba Rais wa Tz alisema atawaamuru polisi watumie silaha za moto? hivyo kuwatia vilema yeyote atakaye andamana? kumbukeni alivyo kuwa akitaka wafanyakazi wasiandamane.

Sasa yaliyotokea Arusha ndiyo hayo Rais aliyasema may, 2010, na polisi wametekalaza amri au agizo la amiri jeshi mkuu.

Hivyo naomba tusiwachukie tu Polisi mchukieni anaye watuma.
 
ndugu zangu wanajf, ninavyofahamu mimi polisi wanatakiwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni zilizopo. Lakini cha kushangaza jeshi hilo limekuwa likitetea maslahi ya ccm na mafisadi hata kama ni kwa gharama ya kuwapiga risasi wananchi.

Mfano mzuri ni wakati wa uchaguzi ambapo jeshi la polisi na askari wake wamekuwa wakitimiza majukumu yao kwa kuipendelea ccm hata hata kama ni kutofuata sheria na kanuni kama vile kukataa kulinda helicopter aliyokuwa akiitumia dr. Slaa wakati wa kampeni na kuwaachia wanaccm wakifanya vurugu kwenye mikutano ya cdm.

Ni jambo la kusikitisha hasa pale unapokuta polisi wanahatarisha usalama na maisha ya mwananchi badala ya kulinda usalama.

Swali langu kubwa ni kwa jinsi tunavyofahamu idadi ndogo ya jeshi hilo ukilinganisha na idadi ya wananchi, siku wananchi wakichoka kuvumilia je ni nani atalinda usalama wa polisi mitaani? Maana tuko tunakaa nao mtaani.

Ushauri wangu kwa jeshi la polisi ni kwamba wafanye kazi zao kwa kufuata sheria na si maagizo ya ccm na serikali yao. Mfano wa jeshi hilo kutotosha hata kuwathibiti wananchi wa mkoa moja upo wazi hata pamoja na silaha zote.

Tumeona juzi tu arusha ilibidi wachukue askari kutoka mikoa ya kilimanjaro na dar na vurugu zilikuwa arusha mjini tu je ingekuwa mkoa wa arusha wote watu wameandama ingekuwaje.

askari najua mko humu jf hasa wakubwa tafadhali msifanye kazi kwa maagizo ya ccm mtapata matatizo ya kutokaa mtaani vizuri na watoto wenu watanyanyasika.

mkuu ushauri wako mzuri lakini angalia usijepigwa ban kuwa unatishia watu maisha . Yamenikuta
 
Wananch msiwe na Hasira sana na Polisi, kwanza nao ni wananchi wenzetu, wanachofanya ni kutekeleza maaigizo ya watawala kama walivyoapa kuwa watii kwa Rais.

Mbona mnasahau kwamba Rais wa Tz alisema atawaamuru polisi watumie silaha za moto? hivyo kuwatia vilema yeyote atakaye andamana? kumbukeni alivyo kuwa akitaka wafanyakazi wasiandamane.

Sasa yaliyotokea Arusha ndiyo hayo Rais aliyasema may, 2010, na polisi wametekalaza amri au agizo la amiri jeshi mkuu.

Hivyo naomba tusiwachukie tu Polisi mchukieni anaye watuma.

Si kweli maana unapotumwa kumwuua mtu na wewe unatekeleza ni sheria gani inasema hivyo? Leo hii CCM ndio iliwatuma askari lakini sisi ndio tumepoteza wananchi wenzetu. Ushauri wangu uko pale pale wasifanye kazi kwa maagizo ya CCM.
 
Gharibu bilal yupo serengeti na wanawake wawili katika mapumuziko na gharama zake ni 10m kwa siku . Sasa kaenda na waker wawili hii hatari kwa matumizi makubwa ya fedha wakati wahadhari wanamtaka akajibu maswali udom

Rudi kwenye mada.
 
Back
Top Bottom