STEIN
JF-Expert Member
- Aug 29, 2010
- 1,770
- 553
Ndugu zangu wanaJF, ninavyofahamu mimi polisi wanatakiwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni zilizopo. Lakini cha kushangaza jeshi hilo limekuwa likitetea maslahi ya CCM na Mafisadi hata kama ni kwa gharama ya kuwapiga risasi wananchi.
Mfano mzuri ni wakati wa uchaguzi ambapo jeshi la polisi na askari wake wamekuwa wakitimiza majukumu yao kwa kuipendelea CCM hata hata kama ni kutofuata sheria na kanuni kama vile kukataa kulinda helicopter aliyokuwa akiitumia Dr. Slaa wakati wa kampeni na kuwaachia wanaCCM wakifanya vurugu kwenye mikutano ya CDM.
Ni jambo la kusikitisha hasa pale unapokuta polisi wanahatarisha usalama na maisha ya mwananchi badala ya kulinda usalama.
Swali langu kubwa ni kwa jinsi tunavyofahamu idadi ndogo ya jeshi hilo ukilinganisha na idadi ya wananchi, Siku wananchi wakichoka kuvumilia je ni nani atalinda usalama wa polisi mitaani? maana tuko tunakaa nao mtaani.
Ushauri wangu kwa jeshi la polisi ni kwamba wafanye kazi zao kwa kufuata sheria na si maagizo ya CCM na serikali yao. Mfano wa jeshi hilo kutotosha hata kuwathibiti wananchi wa mkoa moja upo wazi hata pamoja na silaha zote.
Tumeona juzi tu Arusha ilibidi wachukue askari kutoka mikoa ya Kilimanjaro na Dar na vurugu zilikuwa Arusha mjini tu je ingekuwa mkoa wa arusha wote watu wameandama ingekuwaje.
Askari najua mko humu JF hasa WAKUBWA tafadhali msifanye kazi kwa maagizo ya CCM mtapata matatizo ya kutokaa mtaani vizuri na watoto wenu watanyanyasika.
Mfano mzuri ni wakati wa uchaguzi ambapo jeshi la polisi na askari wake wamekuwa wakitimiza majukumu yao kwa kuipendelea CCM hata hata kama ni kutofuata sheria na kanuni kama vile kukataa kulinda helicopter aliyokuwa akiitumia Dr. Slaa wakati wa kampeni na kuwaachia wanaCCM wakifanya vurugu kwenye mikutano ya CDM.
Ni jambo la kusikitisha hasa pale unapokuta polisi wanahatarisha usalama na maisha ya mwananchi badala ya kulinda usalama.
Swali langu kubwa ni kwa jinsi tunavyofahamu idadi ndogo ya jeshi hilo ukilinganisha na idadi ya wananchi, Siku wananchi wakichoka kuvumilia je ni nani atalinda usalama wa polisi mitaani? maana tuko tunakaa nao mtaani.
Ushauri wangu kwa jeshi la polisi ni kwamba wafanye kazi zao kwa kufuata sheria na si maagizo ya CCM na serikali yao. Mfano wa jeshi hilo kutotosha hata kuwathibiti wananchi wa mkoa moja upo wazi hata pamoja na silaha zote.
Tumeona juzi tu Arusha ilibidi wachukue askari kutoka mikoa ya Kilimanjaro na Dar na vurugu zilikuwa Arusha mjini tu je ingekuwa mkoa wa arusha wote watu wameandama ingekuwaje.
Askari najua mko humu JF hasa WAKUBWA tafadhali msifanye kazi kwa maagizo ya CCM mtapata matatizo ya kutokaa mtaani vizuri na watoto wenu watanyanyasika.