Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,895
- 30,234
Azaria C. Mbughuni
December 31, 2019 at 10:05 PM ·
''One thing that Mwalimu Nyerere did every December between 1953 and 1959.
December 1953 Mwalimu Nyerere visited Bukoba to investigate an incident at Kamachumu where the police used teargas to disperse a crowd.''
Hayo hapo juu nimenyambua kutoka kwa Prof. Mbughuni.
Naomba nishereheshe kidogo ili safari hii ya Mwalimu Nyerere kwenda Bukoba kuhusu wananchi kupigwa mabomu ieleweke vyema:
''Katika mambo ya kusikitisha sana wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika ni kisa cha wananchi waliokuwa katika mkutano wakimsikiliza kiongozi wao Ali Migeyo, kupigwa mabomu ya machozi huko Kamachumu.
Lakini jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa shujaa huyu wa uhuru wa Tanganyika historia imemsahau.
Hakuna popote pale ambapo utalisikia jina lake likitajwa.
Nimekutana na Ali Migeyo wakati natafiti kitabu cha Abdul Sykes.
Bahati nzuri Mutahaba ameandika kitabu cha maisha ya Ali Migeyo, ''The Portrait of a Nationalist,'' na ndani ya kitabu hiki kuna mengi kiasi yamenifanya mimi kuamini na nikaandika katika kitabu cha Sykes kuwa kama si kwa Ali Migeyo kufungwa kufuatia kesi ya mabomu ya machozi kwa hiyo kuasisiwa kwa TANU mwaka 1954 kumkuta akiwa jela ya Butimba akitumika kifungo cha miaka mitatu, Ali Migeyo angekuwa mmoja wa wale waasisi 17 wa TANU.
Baada ya uhuru Ali Migeyo aliwekwa kuzuizini Ukonga Prison kwa tuhuma ya ''kuchanganya dini na siasa'' lakini akaja kutolewa baada ya kuteuliwa na Rais Nyerere kuwa Mbunge.
Inspector General of Police (IGP) Hamza Aziz alinihadithia kuwa alipopewa amri ya kwenda kumtoa jela Ali Migeyo alishtuka jinsi alivyomkuta.
Migeyo alikuwa ndani ya selo yake hana nguo.
Ilibidi arudi mjini amnunulie nguo na viatu ndipo aliporejea jela na kujanae mjini akampangia International Hotel akae wakati anasubiri kwenda bungeni, Karimjee kuapishwa.
Napenda kuhitimisha kwa kusema kuwa baada ya Migeyo kufungwa mwaka wa 1954, Abdul Sykes, Julius Nyerere alikwenda kijijini kwake Bugandika kuijulia hali familia yake.
tatizo kubwa ambalo nimeliona katika kumwandika Mwalimu Nyerere ni kuwa huwa ahusishwi na mtu mwingine hata kama alikuwa bega kwa bega na yeye.
Hii inatoa ladha historia yake.
Mifano iko mingi sana.
Sijui kwa nini Mwalimu alikuwa kimya kuhusu wenzake.
Mfano pale Makao Makuu ya TAA New Street alikuwapo Dr. Michael Lugazia yeye 1953 katika harakati za kuunda TANU ndiye alikuwa kiungò baina ya Makao Makuu na TAA Bukoba akiwatia hima viongozi wa Bukoba kutorudi nyuma kwa ajili ya kufungwa Migeyo waendelee na mapambano.
Dr. Lugazia hatajwi popote katika historia ya TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika.
Dr. Lugazia alimaliza udaktari wake Ocean Road Hospital Dar es Salaam na amekufa akiwa na kinyongo kuhusu historia ya TANU.
Dr. Lugazia katika miaka yake ya mwisho alifungua kinywa chake kwa yeyote aliyekuwa tayari kumsikiliza akawa anaeleza historia ya kweli ya kuasisiwa kwa TANU.''
December 31, 2019 at 10:05 PM ·
''One thing that Mwalimu Nyerere did every December between 1953 and 1959.
December 1953 Mwalimu Nyerere visited Bukoba to investigate an incident at Kamachumu where the police used teargas to disperse a crowd.''
Hayo hapo juu nimenyambua kutoka kwa Prof. Mbughuni.
Naomba nishereheshe kidogo ili safari hii ya Mwalimu Nyerere kwenda Bukoba kuhusu wananchi kupigwa mabomu ieleweke vyema:
''Katika mambo ya kusikitisha sana wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika ni kisa cha wananchi waliokuwa katika mkutano wakimsikiliza kiongozi wao Ali Migeyo, kupigwa mabomu ya machozi huko Kamachumu.
Lakini jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa shujaa huyu wa uhuru wa Tanganyika historia imemsahau.
Hakuna popote pale ambapo utalisikia jina lake likitajwa.
Nimekutana na Ali Migeyo wakati natafiti kitabu cha Abdul Sykes.
Bahati nzuri Mutahaba ameandika kitabu cha maisha ya Ali Migeyo, ''The Portrait of a Nationalist,'' na ndani ya kitabu hiki kuna mengi kiasi yamenifanya mimi kuamini na nikaandika katika kitabu cha Sykes kuwa kama si kwa Ali Migeyo kufungwa kufuatia kesi ya mabomu ya machozi kwa hiyo kuasisiwa kwa TANU mwaka 1954 kumkuta akiwa jela ya Butimba akitumika kifungo cha miaka mitatu, Ali Migeyo angekuwa mmoja wa wale waasisi 17 wa TANU.
Baada ya uhuru Ali Migeyo aliwekwa kuzuizini Ukonga Prison kwa tuhuma ya ''kuchanganya dini na siasa'' lakini akaja kutolewa baada ya kuteuliwa na Rais Nyerere kuwa Mbunge.
Inspector General of Police (IGP) Hamza Aziz alinihadithia kuwa alipopewa amri ya kwenda kumtoa jela Ali Migeyo alishtuka jinsi alivyomkuta.
Migeyo alikuwa ndani ya selo yake hana nguo.
Ilibidi arudi mjini amnunulie nguo na viatu ndipo aliporejea jela na kujanae mjini akampangia International Hotel akae wakati anasubiri kwenda bungeni, Karimjee kuapishwa.
Napenda kuhitimisha kwa kusema kuwa baada ya Migeyo kufungwa mwaka wa 1954, Abdul Sykes, Julius Nyerere alikwenda kijijini kwake Bugandika kuijulia hali familia yake.
tatizo kubwa ambalo nimeliona katika kumwandika Mwalimu Nyerere ni kuwa huwa ahusishwi na mtu mwingine hata kama alikuwa bega kwa bega na yeye.
Hii inatoa ladha historia yake.
Mifano iko mingi sana.
Sijui kwa nini Mwalimu alikuwa kimya kuhusu wenzake.
Mfano pale Makao Makuu ya TAA New Street alikuwapo Dr. Michael Lugazia yeye 1953 katika harakati za kuunda TANU ndiye alikuwa kiungò baina ya Makao Makuu na TAA Bukoba akiwatia hima viongozi wa Bukoba kutorudi nyuma kwa ajili ya kufungwa Migeyo waendelee na mapambano.
Dr. Lugazia hatajwi popote katika historia ya TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika.
Dr. Lugazia alimaliza udaktari wake Ocean Road Hospital Dar es Salaam na amekufa akiwa na kinyongo kuhusu historia ya TANU.
Dr. Lugazia katika miaka yake ya mwisho alifungua kinywa chake kwa yeyote aliyekuwa tayari kumsikiliza akawa anaeleza historia ya kweli ya kuasisiwa kwa TANU.''