Siku Waafrika wakiwa kama Wazungu au Wajapani itakuwaje

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Huwa najiuliza sana haya maswali kwa maana nimeona kwamba sisi Waafrika ni watu wa midomo sana, hivi siku ikija nchi ya Kiafrika ikawa na Uchumi wa Trilion US Dollars kama vile Wazungu au Wajapani, Wachina &Co itakuwaje?

Kwa maana hapa tu ukiangalia kanchi kama Kenya kana uchumi wa kabilioni kadhaa lkn ukimsikia Mkenya akiongea utafikiri Kenya ina trilion Dollar economy au hata Tanzania ni hivyo hivyo!

Mbona Wajapani au Wazungu hawako hivyo yaani hawana midomo midomo wakati ukingalia mauchumi yao yako kwenye matrilioni, Marekani ina zaidi 15 trilion Dollar economy, Japan ana zaidi ya 4 trilion Dollar economy lkn ukikutana na Mjapani ni watu simpo tu wala wkt mwingine hauwezi kujua kama anatoka nchi yenye Trilion Dollar economy!

Sasa njoo kwa Mwafrika siku ikijengwa shopping mall tu nchini mwake basi matako hulia mbwata, sasa ni kwa nini??
Unakuta Mwafrika siku akienda Ulaya utakuta kazaliwa na kukulia hapa hapa Bongo, akaja kwenda Ulaya miaka 3 tu, akirudi ukienda kumpokea airport anaanza kulalamika mara joto sana, vumbi, mwingine anaogopa kupanda daladala wkt miaka yote kasoma Tambaza alikuwa anapanda chai maharage tena anapanda nyuma kwenye mlangao baada ya kujaa kwanza, kuna mmoja alikuja na mtoto wake tukaenda kijijini akamchukulia mtoto wake uma na kisu ktk Dar, sasa kwanini tuko hiyo? Mbona Wajapani au Wazungu ni watu simpo tu ili hali wao wanatoka kwenye manchi yenye zaidi ya trilion dollars economy??
 
kutokujiamini ndio tatizo. siku wazungu wakawa weusi na Waafrika wakawa weupe nakwambia dada zetu watapaka mkaa ili wawe weusi!
 
Mkuu Ni ulimbukeni tu unajua mtu ambae anakitu kidogo ana limbuka sana tofauti na yule mwenye nacho kingi we angalia hata maofisini wanaosumbua sana elimu zao ni za kuunga au wapo pale kwa kuwekwa Ebu tazama engineers wanavyolilia waitwe engineer au Dk Fastjet ebu njoo kwa hao maprofesa sasa wanavyolilia kutajwa sambamba na title wenzetu wamesogea haswa mwafirika ukimsifia atakupenda ila ukimueleza weakness anakuchukia, mzungu anapenda zaidi umwambie weakness ili ajimalishe mwisho wa yote Debe tupuuu lina kelele mno Hao kenya na hio lugha tu ya malikia wanatunisha misuli ya ma*tako utadhani wana vinu vya nyukilia au satellite angani
 
Huwa najiuliza sana haya maswali kwa maana nimeona kwamba sisi Waafrika ni watu wa midomo sana, hivi siku ikija nchi ya Kiafrika ikawa na Uchumi wa Trilion US Dollars kama vile Wazungu au Wajapani, Wachina &Co itakuwaje?

Kwa maana hapa tu ukiangalia kanchi kama Kenya kana uchumi wa kabilioni kadhaa lkn ukimsikia Mkenya akiongea utafikiri Kenya ina trilion Dollar economy au hata Tanzania ni hivyo hivyo!

Mbona Wajapani au Wazungu hawako hivyo yaani hawana midomo midomo wakati ukingalia mauchumi yao yako kwenye matrilioni, Marekani ina zaidi 15 trilion Dollar economy, Japan ana zaidi ya 4 trilion Dollar economy lkn ukikutana na Mjapani ni watu simpo tu wala wkt mwingine hauwezi kujua kama anatoka nchi yenye Trilion Dollar economy!

Sasa njoo kwa Mwafrika siku ikijengwa shopping mall tu nchini mwake basi matako hulia mbwata, sasa ni kwa nini??
Unakuta Mwafrika siku akienda Ulaya utakuta kazaliwa na kukulia hapa hapa Bongo, akaja kwenda Ulaya miaka 3 tu, akirudi ukienda kumpokea airport anaanza kulalamika mara joto sana, vumbi, mwingine anaogopa kupanda daladala wkt miaka yote kasoma Tambaza alikuwa anapanda chai maharage tena anapanda nyuma kwenye mlangao baada ya kujaa kwanza, kuna mmoja alikuja na mtoto wake tukaenda kijijini akamchukulia mtoto wake uma na kisu ktk Dar, sasa kwanini tuko hiyo? Mbona Wajapani au Wazungu ni watu simpo tu ili hali wao wanatoka kwenye manchi yenye zaidi ya trilion dollars economy??
Hayo yatawezekana endapo mtatoa dhana ya uwepo wa mungu. Hii inamaliza sana akili za utendaji. Maana mnaamini Mtaishi mkifa
 
Hayo yatawezekana endapo mtatoa dhana ya uwepo wa mungu. Hii inamaliza sana akili za utendaji. Maana mnaamini Mtaishi mkifa
Unalipenda hili suala ila lipo juu ya uwezo wako wa kufikiri,usituchanganyie mambo maana mwishowe utakuja kusema waafrika hawataki ndoa za jinsia moja kama wazungu kwa sababu ya ujinga wao wa kuamini mungu.
 
Ulimbukeni mwingi kwa Mwafrika akifanikiwa kidogo, mlio karibu naye mtaipata. Mawazo yake anataka awe kama hao wazungu bila ya kuwaona kuwa licha ya kuwa na uwezo wa kifedha, lakini hawana majisifu yasiyo na kichwa wala miguu.
 
Back
Top Bottom