Siku sita za mwandishi kuuza baa (7): Wapi nitapata toleo la kwanza to 6 please

Mavindozii

JF-Expert Member
Oct 20, 2012
2,111
2,759
HABARI

Siku sita za mwandishi kuuza baa (7)

Wafanyakazi wa baa wakisubiri kuwahudumia wateja.

By Jacline Masinde, Mwananchi jmasinde@mwananchi.co.tzIN SUMMARY

Nilipozunguka nyuma ya gheto nilimkuta Neema anatapika na jitihada zangu kumdadisi kilichomsibu, hazikufanikiwa kwa kuwa hakutaka kuongea. Lakini wakati wateja wanaanza kuja, Neema anaonekana kuwahudumia muda wote bila ya matatizo na baadaye wakati anapumzika, akaamua kutumia muda huo kuongea na rafiki yake Jane kwa lugha ya Kilugulu.

Jana simulizi hii iliisha wakati nilipoamua kuzunguka nyuma na kumkuta Neema akitapika. Ilikuwa ni baada ya kuambiwa tupange viti muda wa saa tisa alasiri kwa kuwa ndiyo wateja walikuwa wanaanza kufika. Sasa endelea...

Nilipozunguka nyuma ya gheto nilimkuta Neema anatapika na jitihada zangu kumdadisi kilichomsibu, hazikufanikiwa kwa kuwa hakutaka kuongea. Lakini wakati wateja wanaanza kuja, Neema anaonekana kuwahudumia muda wote bila ya matatizo na baadaye wakati anapumzika, akaamua kutumia muda huo kuongea na rafiki yake Jane kwa lugha ya Kilugulu.

Japo Kilugulu si lugha yangu, nakielewa kwa kuwa nimewahi kukaa Uluguluni kwa zaidi ya miaka 10.

Neema anamwambia Janeth kuwa anahisi kama ni mjamzito na amempigia simu aliyempa mimba lakini anakataa kwa kuwa mtu huyo ana mke na mtoto.

“Nimempigia simu kasema nisimsumbue kwa kuwa ni mume wa mtu. Nilipomuuliza kwanini, hakuniambia. Hakunijibu zaidi ya kunikatia simu,” anasema kwa Kilugulu.

Wanapogundua kuwa nawasikiliza, wanaamua kutoka eneo hilo na kusogea mbali zaidi na mimi naachana nao na kuendelea kuhudumia wateja.

Baadaye wanakuja wanaume wawili ambao wanahudumiwa na Sharifa na mmoja wao anamtongoza akimshawishi waondoke naye wakati baa itakapokuwa inafungwa.

Nikiwa napita karibu na meza ya wanaume hao, mmoja ananiita na kunitongoza. Ananiambia kuwa leo niondoke naye.

“Nimekupenda sana binti. Unafaa kuwa na mimi usiku wa leo. Vipi uko tayari tuondoke wote?” ananiuliza.

Nikamjibu siko tayari.

“Acha hizo wewe au unamwogopa bosi wako? Usijali, mimi naenda kuongea naye. Si huwa mnalipiwa hela pale kaunta?” anauliza na mimi nikamjibu ndiyo akasema ataenda kulipa.

Kuona hivyo, nikamfuata rafiki yangu Sharifa nikamweleza kilichotokea naye akashangaa.

“Na wewe wanakutaka? Mimi mwenyewe yule mwingine kasema ananitaka niondoke naye na ameshazungumza na bosi akakubali. Hapa nasubiri tu nimalize kazi tuondoke,” anasema Sharifa.

“Kubali uondoke naye, lakini hakikisha kabla ya yote anakupa fedha yako kabisa.”

Nikataka kujua kwa siku Sharifa huwa anatoka na wanaume wangapi, akaniambia kuwa hali ikiwa nzuri anaweza kutoka na watatu hadi wanne.

Nikamuuliza huwa anajigawa vipi kiasi cha kuweza pia kufanya kazi yake ya uhudumu kwa wakati mmoja.

“Wengine tunamalizana nao hapahapa. Tunaweza kuingia kule chooni au gheto, tunapiga shortime tu. Mi’ nachukua changu,” ananiambia.

Nikiwa naendelea kuzungumza na Sharifa, yule baba anarejea kwenye meza yake na kuniita. Ananiambia kuwa ameshaongea na bosi wangu na amekataa.

“Lakini ninachotaka ufanye, naomba utoroke,” anashauri huyo baba.

Ninamkubalia kwamba nitatoroka. Baadaye naamua kuondoka eneo hilo na kwenda kukaa pamoja na Sharifa na Teddy, mfanyakazi mwingine wa baa hiyo. Nikatamani wanieleze changamoto wanazozipata kazini. “Shoga wewe acha tu. Hizi kazi ni ngumu sana asikwambie mtu. Wewe mwenyewe unaona, kwanza mahali pa kulala ukitembea baa nyingi wahudumu wanalala sehemu mbaya,” anasema Teddy.

Teddy anasema usalama wao ni mdogo.

“Kubakwa ni njenje, kupigwa ndo usiseme. Kutukanwa matusi ya nguoni mpaka unaona aibu,” anasema .

Wananiambia kuwa wanaume wengine wanaotembea nao ni wale wanaokuja kunywa kwenye baa hii. Wanasema wanaume hao wakilewa, huwatukana na kuwadhalilisha mbele za watu, wakielezea maumbile yao ya siri yalivyo.

“Kwenye baa niliyokuwa nafanya kazi kabla ya kuja hapa kuna mwanaume nilitoka naye. Alipokuja mara ya pili nikaenda kumhudumia, lakini baada ya kulewa pombe alianza kunitukana na kunidhalilisha mpaka nikaona aibu,” anasema.

“Alikuwa anataka anishike sehemu za siri mbele za watu au anakwambia uvue nguo mbele za watu mfanye mapenzi,”anasema Teddy.

Sharifa naye anasema hivi karibuni kabla sijaja, alipigwa vibao na wanaume waliokuwa wanakunywa pombe kwa bili.

“Ni Wakurya. Nilipowapelekea bili, waliniambia bili ni kubwa kwa hiyo nikapewa kipigo. Niliokolewa na bosi lakini wakati tayari nimeshaumia,” anasema.

“Ikifikia mteja anakupiga au anaondoka na bili, wewe unakatwa kwenye mshahara wako. Ukimuhudumia mteja akalewa, akavunja chupa ama akaondoka nayo bila wewe kujua, unakatwa kwenye mshahara.”

Sharifa anasema mwezi uliopita alipokea mshahara wa Sh50,000 baada ya kukakatwa Sh20,000 nzima.

“Dada hizi kazi tunafanya tu, ila si kazi. Si upo utayaona tu,” anasema.

Kupima Ukimwi

Tukiwa tunaendelea na maongezi, Fred anatuita wafanyakazi wote na kututaka tukapime Ukimwi. Anasema kulikuwa na gari linapita kwenye mitaa na maeneo ya baa na kuwataka wananchi wapime Ukimwi.

“Mjipange kwa zamu mkapime Ukimwi kila mhudumu. Hiyo ni lazima siyo ombi,” anasema meneja Fredy, taarifa inayoonekana kuwashtua wafanyakazi wote.

Hata hivyo, kazi hiyo inamalizika vizuri na wote tunapewa majibu yetu. Tedy ananikimbilia kunikumbatia kwa furaha akiwa haamini kama hana Ukimwi. Tunaendelea na kazi.

Wakati tukiendelea na kazi, wakaja vijana wawili; mmoja mweupe na mwingine mweusi. Walikuwa wananitazama kwa jicho la kunitamani, huku mmoja aliyekuwa akivuta kiti ili akae karibu na nilipokaa, akisema “jamani huyu binti mzuri hivi katoka wapi tena? Hii ni rangi ninayoizimia”.

Wakati wakiendelea kunywa, anaanza kunitongoza huku akinitomasa.

“Wewe sikuachi, lazima nifanye mambo. Bosi wako yupo?” anasema na nikamjibu kuwa yupo. Akanyanyuka kwenda kaunta kuonana na meneja.

Baada ya dakika kumi anarejea na kuniambia nimeshaongea na bosi wako, kakubali na nimempa fedha. Naomba twende tukamalize mambo,” anasema.

Nikamwambia utanipa shilingi ngapi, akaniuliza wewe unataka Shilingi ngapi? nikamtajia Sh50,000 akasema “hapana mimi Sh10,000 inakutosha kumbuka nalipia chumba Sh10,000, fedha ya bosi wako Sh 5,000 ukisema fedha kubwa hivyo utakuwa unaniua,” anasema.

Nikamjibu kuwa akitaka kizuri lazima agharamie. Bila hata haya, kijana huyo anasema nisubiri akatafute hiyo fedha. Akaondoka zake na baada ya nusu saa anarudi akiwa na noti tatu za Sh10,000 kwa maana ya Sh30,000. Ananionyesha kuwa ana hamu sana ya kufanya tendo la ndoa nami na anazidi kunishawishi niondoke naye.

Lakini nakataa kupokea fedha. Kuona hivyo anabadili wazo na kunitaka twende gheto tunakolala wahudumu ili Sh10,000 ya chumba anipe.

Wakati tukiendelea na mazungumzo akaja yule baba aliyetaka niondoke naye siku ya pili tangu nianze kazi, lakini wenzangu wakanizuia kwamba hana fedha. Yule baba akaanza kuimba ule wimbo wake, akionekana amejipanga vizuri zaidi. Aliweka oda mapema kwa Fredy, akiwa amemtaka asiniruhusu niondoke na mwanaume wa aina yeyote siku hiyo isipokuwa yeye.

Saa tatu usiku, ananiita na kunipa Sh5,000 anayodai kuwa ameambiwa na Fredy niipeleke kwake. Namkatalia na kumwambia badala yake yeye aipeleke kwa bosi.

Pia, nikatumia muda huo kumweleza kiasi cha fedha anachotakiwa kunilipa endapo anataka kufanya tendo la ngono na mimi.

“Unataka shilingi ngapi?” ananiuliza.

“Nataka Sh100,000,” namjibu na anaonekana kushtuka. “Pesa yote hiyo? Wewe utakuwa hunipendi,” anasema.

Nikamjibu nakupenda ila huwezi kunitoa kazini na kwenda kufanya mapenzi na mimi, halafu unilipe fedha kidogo.

“Wewe kubali nitakulipa, lakini siyo fedha hiyo,” anasema.

Ananipa tena Sh5,000 ili nimpelekee bosi.

“Chukua hii mpelekee bosi wako. Mwambie kuna mtu kaniambia nikuletee, yeye atajua na atakupa maelekezo,” anasema.

Nikachukua fedha hiyo ambayo ni malipo kwa bosi Fredy ili aniruhusu kwenda kulala na mwanaume huyo.

“Akishakuruhus
 
HABARI

Siku sita za mwandishi kuuza baa (7)

Wafanyakazi wa baa wakisubiri kuwahudumia wateja.

By Jacline Masinde, Mwananchi jmasinde@mwananchi.co.tzIN SUMMARY

Nilipozunguka nyuma ya gheto nilimkuta Neema anatapika na jitihada zangu kumdadisi kilichomsibu, hazikufanikiwa kwa kuwa hakutaka kuongea. Lakini wakati wateja wanaanza kuja, Neema anaonekana kuwahudumia muda wote bila ya matatizo na baadaye wakati anapumzika, akaamua kutumia muda huo kuongea na rafiki yake Jane kwa lugha ya Kilugulu.

Jana simulizi hii iliisha wakati nilipoamua kuzunguka nyuma na kumkuta Neema akitapika. Ilikuwa ni baada ya kuambiwa tupange viti muda wa saa tisa alasiri kwa kuwa ndiyo wateja walikuwa wanaanza kufika. Sasa endelea...

Nilipozunguka nyuma ya gheto nilimkuta Neema anatapika na jitihada zangu kumdadisi kilichomsibu, hazikufanikiwa kwa kuwa hakutaka kuongea. Lakini wakati wateja wanaanza kuja, Neema anaonekana kuwahudumia muda wote bila ya matatizo na baadaye wakati anapumzika, akaamua kutumia muda huo kuongea na rafiki yake Jane kwa lugha ya Kilugulu.

Japo Kilugulu si lugha yangu, nakielewa kwa kuwa nimewahi kukaa Uluguluni kwa zaidi ya miaka 10.

Neema anamwambia Janeth kuwa anahisi kama ni mjamzito na amempigia simu aliyempa mimba lakini anakataa kwa kuwa mtu huyo ana mke na mtoto.

“Nimempigia simu kasema nisimsumbue kwa kuwa ni mume wa mtu. Nilipomuuliza kwanini, hakuniambia. Hakunijibu zaidi ya kunikatia simu,” anasema kwa Kilugulu.

Wanapogundua kuwa nawasikiliza, wanaamua kutoka eneo hilo na kusogea mbali zaidi na mimi naachana nao na kuendelea kuhudumia wateja.

Baadaye wanakuja wanaume wawili ambao wanahudumiwa na Sharifa na mmoja wao anamtongoza akimshawishi waondoke naye wakati baa itakapokuwa inafungwa.

Nikiwa napita karibu na meza ya wanaume hao, mmoja ananiita na kunitongoza. Ananiambia kuwa leo niondoke naye.

“Nimekupenda sana binti. Unafaa kuwa na mimi usiku wa leo. Vipi uko tayari tuondoke wote?” ananiuliza.

Nikamjibu siko tayari.

“Acha hizo wewe au unamwogopa bosi wako? Usijali, mimi naenda kuongea naye. Si huwa mnalipiwa hela pale kaunta?” anauliza na mimi nikamjibu ndiyo akasema ataenda kulipa.

Kuona hivyo, nikamfuata rafiki yangu Sharifa nikamweleza kilichotokea naye akashangaa.

“Na wewe wanakutaka? Mimi mwenyewe yule mwingine kasema ananitaka niondoke naye na ameshazungumza na bosi akakubali. Hapa nasubiri tu nimalize kazi tuondoke,” anasema Sharifa.

“Kubali uondoke naye, lakini hakikisha kabla ya yote anakupa fedha yako kabisa.”

Nikataka kujua kwa siku Sharifa huwa anatoka na wanaume wangapi, akaniambia kuwa hali ikiwa nzuri anaweza kutoka na watatu hadi wanne.

Nikamuuliza huwa anajigawa vipi kiasi cha kuweza pia kufanya kazi yake ya uhudumu kwa wakati mmoja.

“Wengine tunamalizana nao hapahapa. Tunaweza kuingia kule chooni au gheto, tunapiga shortime tu. Mi’ nachukua changu,” ananiambia.

Nikiwa naendelea kuzungumza na Sharifa, yule baba anarejea kwenye meza yake na kuniita. Ananiambia kuwa ameshaongea na bosi wangu na amekataa.

“Lakini ninachotaka ufanye, naomba utoroke,” anashauri huyo baba.

Ninamkubalia kwamba nitatoroka. Baadaye naamua kuondoka eneo hilo na kwenda kukaa pamoja na Sharifa na Teddy, mfanyakazi mwingine wa baa hiyo. Nikatamani wanieleze changamoto wanazozipata kazini. “Shoga wewe acha tu. Hizi kazi ni ngumu sana asikwambie mtu. Wewe mwenyewe unaona, kwanza mahali pa kulala ukitembea baa nyingi wahudumu wanalala sehemu mbaya,” anasema Teddy.

Teddy anasema usalama wao ni mdogo.

“Kubakwa ni njenje, kupigwa ndo usiseme. Kutukanwa matusi ya nguoni mpaka unaona aibu,” anasema .

Wananiambia kuwa wanaume wengine wanaotembea nao ni wale wanaokuja kunywa kwenye baa hii. Wanasema wanaume hao wakilewa, huwatukana na kuwadhalilisha mbele za watu, wakielezea maumbile yao ya siri yalivyo.

“Kwenye baa niliyokuwa nafanya kazi kabla ya kuja hapa kuna mwanaume nilitoka naye. Alipokuja mara ya pili nikaenda kumhudumia, lakini baada ya kulewa pombe alianza kunitukana na kunidhalilisha mpaka nikaona aibu,” anasema.

“Alikuwa anataka anishike sehemu za siri mbele za watu au anakwambia uvue nguo mbele za watu mfanye mapenzi,”anasema Teddy.

Sharifa naye anasema hivi karibuni kabla sijaja, alipigwa vibao na wanaume waliokuwa wanakunywa pombe kwa bili.

“Ni Wakurya. Nilipowapelekea bili, waliniambia bili ni kubwa kwa hiyo nikapewa kipigo. Niliokolewa na bosi lakini wakati tayari nimeshaumia,” anasema.

“Ikifikia mteja anakupiga au anaondoka na bili, wewe unakatwa kwenye mshahara wako. Ukimuhudumia mteja akalewa, akavunja chupa ama akaondoka nayo bila wewe kujua, unakatwa kwenye mshahara.”

Sharifa anasema mwezi uliopita alipokea mshahara wa Sh50,000 baada ya kukakatwa Sh20,000 nzima.

“Dada hizi kazi tunafanya tu, ila si kazi. Si upo utayaona tu,” anasema.

Kupima Ukimwi

Tukiwa tunaendelea na maongezi, Fred anatuita wafanyakazi wote na kututaka tukapime Ukimwi. Anasema kulikuwa na gari linapita kwenye mitaa na maeneo ya baa na kuwataka wananchi wapime Ukimwi.

“Mjipange kwa zamu mkapime Ukimwi kila mhudumu. Hiyo ni lazima siyo ombi,” anasema meneja Fredy, taarifa inayoonekana kuwashtua wafanyakazi wote.

Hata hivyo, kazi hiyo inamalizika vizuri na wote tunapewa majibu yetu. Tedy ananikimbilia kunikumbatia kwa furaha akiwa haamini kama hana Ukimwi. Tunaendelea na kazi.

Wakati tukiendelea na kazi, wakaja vijana wawili; mmoja mweupe na mwingine mweusi. Walikuwa wananitazama kwa jicho la kunitamani, huku mmoja aliyekuwa akivuta kiti ili akae karibu na nilipokaa, akisema “jamani huyu binti mzuri hivi katoka wapi tena? Hii ni rangi ninayoizimia”.

Wakati wakiendelea kunywa, anaanza kunitongoza huku akinitomasa.

“Wewe sikuachi, lazima nifanye mambo. Bosi wako yupo?” anasema na nikamjibu kuwa yupo. Akanyanyuka kwenda kaunta kuonana na meneja.

Baada ya dakika kumi anarejea na kuniambia nimeshaongea na bosi wako, kakubali na nimempa fedha. Naomba twende tukamalize mambo,” anasema.

Nikamwambia utanipa shilingi ngapi, akaniuliza wewe unataka Shilingi ngapi? nikamtajia Sh50,000 akasema “hapana mimi Sh10,000 inakutosha kumbuka nalipia chumba Sh10,000, fedha ya bosi wako Sh 5,000 ukisema fedha kubwa hivyo utakuwa unaniua,” anasema.

Nikamjibu kuwa akitaka kizuri lazima agharamie. Bila hata haya, kijana huyo anasema nisubiri akatafute hiyo fedha. Akaondoka zake na baada ya nusu saa anarudi akiwa na noti tatu za Sh10,000 kwa maana ya Sh30,000. Ananionyesha kuwa ana hamu sana ya kufanya tendo la ndoa nami na anazidi kunishawishi niondoke naye.

Lakini nakataa kupokea fedha. Kuona hivyo anabadili wazo na kunitaka twende gheto tunakolala wahudumu ili Sh10,000 ya chumba anipe.

Wakati tukiendelea na mazungumzo akaja yule baba aliyetaka niondoke naye siku ya pili tangu nianze kazi, lakini wenzangu wakanizuia kwamba hana fedha. Yule baba akaanza kuimba ule wimbo wake, akionekana amejipanga vizuri zaidi. Aliweka oda mapema kwa Fredy, akiwa amemtaka asiniruhusu niondoke na mwanaume wa aina yeyote siku hiyo isipokuwa yeye.

Saa tatu usiku, ananiita na kunipa Sh5,000 anayodai kuwa ameambiwa na Fredy niipeleke kwake. Namkatalia na kumwambia badala yake yeye aipeleke kwa bosi.

Pia, nikatumia muda huo kumweleza kiasi cha fedha anachotakiwa kunilipa endapo anataka kufanya tendo la ngono na mimi.

“Unataka shilingi ngapi?” ananiuliza.

“Nataka Sh100,000,” namjibu na anaonekana kushtuka. “Pesa yote hiyo? Wewe utakuwa hunipendi,” anasema.

Nikamjibu nakupenda ila huwezi kunitoa kazini na kwenda kufanya mapenzi na mimi, halafu unilipe fedha kidogo.

“Wewe kubali nitakulipa, lakini siyo fedha hiyo,” anasema.

Ananipa tena Sh5,000 ili nimpelekee bosi.

“Chukua hii mpelekee bosi wako. Mwambie kuna mtu kaniambia nikuletee, yeye atajua na atakupa maelekezo,” anasema.

Nikachukua fedha hiyo ambayo ni malipo kwa bosi Fredy ili aniruhusu kwenda....... kulala na mwanaume huyo.

“Akishakuruhusu [HAPA PAMEKAA VIBAYA]

HABARI

Siku sita za mwandishi kuuza baa (7)

Wafanyakazi wa baa wakisubiri kuwahudumia wateja.

By Jacline Masinde, Mwananchi jmasinde@mwananchi.co.tzIN SUMMARY

Nilipozunguka nyuma ya gheto nilimkuta Neema anatapika na jitihada zangu kumdadisi kilichomsibu, hazikufanikiwa kwa kuwa hakutaka kuongea. Lakini wakati wateja wanaanza kuja, Neema anaonekana kuwahudumia muda wote bila ya matatizo na baadaye wakati anapumzika, akaamua kutumia muda huo kuongea na rafiki yake Jane kwa lugha ya Kilugulu.

Jana simulizi hii iliisha wakati nilipoamua kuzunguka nyuma na kumkuta Neema akitapika. Ilikuwa ni baada ya kuambiwa tupange viti muda wa saa tisa alasiri kwa kuwa ndiyo wateja walikuwa wanaanza kufika. Sasa endelea...

Nilipozunguka nyuma ya gheto nilimkuta Neema anatapika na jitihada zangu kumdadisi kilichomsibu, hazikufanikiwa kwa kuwa hakutaka kuongea. Lakini wakati wateja wanaanza kuja, Neema anaonekana kuwahudumia muda wote bila ya matatizo na baadaye wakati anapumzika, akaamua kutumia muda huo kuongea na rafiki yake Jane kwa lugha ya Kilugulu.

Japo Kilugulu si lugha yangu, nakielewa kwa kuwa nimewahi kukaa Uluguluni kwa zaidi ya miaka 10.

Neema anamwambia Janeth kuwa anahisi kama ni mjamzito na amempigia simu aliyempa mimba lakini anakataa kwa kuwa mtu huyo ana mke na mtoto.

“Nimempigia simu kasema nisimsumbue kwa kuwa ni mume wa mtu. Nilipomuuliza kwanini, hakuniambia. Hakunijibu zaidi ya kunikatia simu,” anasema kwa Kilugulu.

Wanapogundua kuwa nawasikiliza, wanaamua kutoka eneo hilo na kusogea mbali zaidi na mimi naachana nao na kuendelea kuhudumia wateja.

Baadaye wanakuja wanaume wawili ambao wanahudumiwa na Sharifa na mmoja wao anamtongoza akimshawishi waondoke naye wakati baa itakapokuwa inafungwa.

Nikiwa napita karibu na meza ya wanaume hao, mmoja ananiita na kunitongoza. Ananiambia kuwa leo niondoke naye.

“Nimekupenda sana binti. Unafaa kuwa na mimi usiku wa leo. Vipi uko tayari tuondoke wote?” ananiuliza.

Nikamjibu siko tayari.

“Acha hizo wewe au unamwogopa bosi wako? Usijali, mimi naenda kuongea naye. Si huwa mnalipiwa hela pale kaunta?” anauliza na mimi nikamjibu ndiyo akasema ataenda kulipa.

Kuona hivyo, nikamfuata rafiki yangu Sharifa nikamweleza kilichotokea naye akashangaa.

“Na wewe wanakutaka? Mimi mwenyewe yule mwingine kasema ananitaka niondoke naye na ameshazungumza na bosi akakubali. Hapa nasubiri tu nimalize kazi tuondoke,” anasema Sharifa.

“Kubali uondoke naye, lakini hakikisha kabla ya yote anakupa fedha yako kabisa.”

Nikataka kujua kwa siku Sharifa huwa anatoka na wanaume wangapi, akaniambia kuwa hali ikiwa nzuri anaweza kutoka na watatu hadi wanne.

Nikamuuliza huwa anajigawa vipi kiasi cha kuweza pia kufanya kazi yake ya uhudumu kwa wakati mmoja.

“Wengine tunamalizana nao hapahapa. Tunaweza kuingia kule chooni au gheto, tunapiga shortime tu. Mi’ nachukua changu,” ananiambia.

Nikiwa naendelea kuzungumza na Sharifa, yule baba anarejea kwenye meza yake na kuniita. Ananiambia kuwa ameshaongea na bosi wangu na amekataa.

“Lakini ninachotaka ufanye, naomba utoroke,” anashauri huyo baba.

Ninamkubalia kwamba nitatoroka. Baadaye naamua kuondoka eneo hilo na kwenda kukaa pamoja na Sharifa na Teddy, mfanyakazi mwingine wa baa hiyo. Nikatamani wanieleze changamoto wanazozipata kazini. “Shoga wewe acha tu. Hizi kazi ni ngumu sana asikwambie mtu. Wewe mwenyewe unaona, kwanza mahali pa kulala ukitembea baa nyingi wahudumu wanalala sehemu mbaya,” anasema Teddy.

Teddy anasema usalama wao ni mdogo.

“Kubakwa ni njenje, kupigwa ndo usiseme. Kutukanwa matusi ya nguoni mpaka unaona aibu,” anasema .

Wananiambia kuwa wanaume wengine wanaotembea nao ni wale wanaokuja kunywa kwenye baa hii. Wanasema wanaume hao wakilewa, huwatukana na kuwadhalilisha mbele za watu, wakielezea maumbile yao ya siri yalivyo.

“Kwenye baa niliyokuwa nafanya kazi kabla ya kuja hapa kuna mwanaume nilitoka naye. Alipokuja mara ya pili nikaenda kumhudumia, lakini baada ya kulewa pombe alianza kunitukana na kunidhalilisha mpaka nikaona aibu,” anasema.

“Alikuwa anataka anishike sehemu za siri mbele za watu au anakwambia uvue nguo mbele za watu mfanye mapenzi,”anasema Teddy.

Sharifa naye anasema hivi karibuni kabla sijaja, alipigwa vibao na wanaume waliokuwa wanakunywa pombe kwa bili.

“Ni Wakurya. Nilipowapelekea bili, waliniambia bili ni kubwa kwa hiyo nikapewa kipigo. Niliokolewa na bosi lakini wakati tayari nimeshaumia,” anasema.

“Ikifikia mteja anakupiga au anaondoka na bili, wewe unakatwa kwenye mshahara wako. Ukimuhudumia mteja akalewa, akavunja chupa ama akaondoka nayo bila wewe kujua, unakatwa kwenye mshahara.”

Sharifa anasema mwezi uliopita alipokea mshahara wa Sh50,000 baada ya kukakatwa Sh20,000 nzima.

“Dada hizi kazi tunafanya tu, ila si kazi. Si upo utayaona tu,” anasema.

Kupima Ukimwi

Tukiwa tunaendelea na maongezi, Fred anatuita wafanyakazi wote na kututaka tukapime Ukimwi. Anasema kulikuwa na gari linapita kwenye mitaa na maeneo ya baa na kuwataka wananchi wapime Ukimwi.

“Mjipange kwa zamu mkapime Ukimwi kila mhudumu. Hiyo ni lazima siyo ombi,” anasema meneja Fredy, taarifa inayoonekana kuwashtua wafanyakazi wote.

Hata hivyo, kazi hiyo inamalizika vizuri na wote tunapewa majibu yetu. Tedy ananikimbilia kunikumbatia kwa furaha akiwa haamini kama hana Ukimwi. Tunaendelea na kazi.

Wakati tukiendelea na kazi, wakaja vijana wawili; mmoja mweupe na mwingine mweusi. Walikuwa wananitazama kwa jicho la kunitamani, huku mmoja aliyekuwa akivuta kiti ili akae karibu na nilipokaa, akisema “jamani huyu binti mzuri hivi katoka wapi tena? Hii ni rangi ninayoizimia”.

Wakati wakiendelea kunywa, anaanza kunitongoza huku akinitomasa.

“Wewe sikuachi, lazima nifanye mambo. Bosi wako yupo?” anasema na nikamjibu kuwa yupo. Akanyanyuka kwenda kaunta kuonana na meneja.

Baada ya dakika kumi anarejea na kuniambia nimeshaongea na bosi wako, kakubali na nimempa fedha. Naomba twende tukamalize mambo,” anasema.

Nikamwambia utanipa shilingi ngapi, akaniuliza wewe unataka Shilingi ngapi? nikamtajia Sh50,000 akasema “hapana mimi Sh10,000 inakutosha kumbuka nalipia chumba Sh10,000, fedha ya bosi wako Sh 5,000 ukisema fedha kubwa hivyo utakuwa unaniua,” anasema.

Nikamjibu kuwa akitaka kizuri lazima agharamie. Bila hata haya, kijana huyo anasema nisubiri akatafute hiyo fedha. Akaondoka zake na baada ya nusu saa anarudi akiwa na noti tatu za Sh10,000 kwa maana ya Sh30,000. Ananionyesha kuwa ana hamu sana ya kufanya tendo la ndoa nami na anazidi kunishawishi niondoke naye.

Lakini nakataa kupokea fedha. Kuona hivyo anabadili wazo na kunitaka twende gheto tunakolala wahudumu ili Sh10,000 ya chumba anipe.

Wakati tukiendelea na mazungumzo akaja yule baba aliyetaka niondoke naye siku ya pili tangu nianze kazi, lakini wenzangu wakanizuia kwamba hana fedha. Yule baba akaanza kuimba ule wimbo wake, akionekana amejipanga vizuri zaidi. Aliweka oda mapema kwa Fredy, akiwa amemtaka asiniruhusu niondoke na mwanaume wa aina yeyote siku hiyo isipokuwa yeye.

Saa tatu usiku, ananiita na kunipa Sh5,000 anayodai kuwa ameambiwa na Fredy niipeleke kwake. Namkatalia na kumwambia badala yake yeye aipeleke kwa bosi.

Pia, nikatumia muda huo kumweleza kiasi cha fedha anachotakiwa kunilipa endapo anataka kufanya tendo la ngono na mimi.

“Unataka shilingi ngapi?” ananiuliza.

“Nataka Sh100,000,” namjibu na anaonekana kushtuka. “Pesa yote hiyo? Wewe utakuwa hunipendi,” anasema.

Nikamjibu nakupenda ila huwezi kunitoa kazini na kwenda kufanya mapenzi na mimi, halafu unilipe fedha kidogo.

“Wewe kubali nitakulipa, lakini siyo fedha hiyo,” anasema.

Ananipa tena Sh5,000 ili nimpelekee bosi.

“Chukua hii mpelekee bosi wako. Mwambie kuna mtu kaniambia nikuletee, yeye atajua na atakupa maelekezo,” anasema.

Nikachukua fedha hiyo ambayo ni malipo kwa bosi Fredy ili aniruhusu kwenda kulala na mwanaume huyo.

“Akishakuruhus
 
Back
Top Bottom