balibabambonahi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2015
- 14,425
- 12,530
Vitu vingine tuwe tunatafiti kidogo,Maalim Seif hakuwahi kuwa na uadui na Nyerere na mpaka Nyerere anamliza uongozi wake 1985 kama rais wa nchi na mwenyekiti wa ccm 1987,maalim Seif alikuwa ccm kindakindaki.Seif aliwekwa kizuizini Nyerere akiwa tayari ameng'atuka.Ahmed Rajab siku zote nikihisi ni "kijana" wa Nyerere. Katika system aliyoitengeneza Mwalimu kuna watu ambao wengine unaweza dhani labda ni mahasimu wake kumbe kwa makusudi amepanga iwe hivyo
Miongoni mwao ni pamoja na marehemu Seif Sharif Hamad. Maalif Seif aliwahi kuwekwa kizuizini wakati wa utawala wa awamu ya kwanza hadi alipotolewa na Mwinyi 1988 lakini kwa wanaomfahamu ni kwamba alikua ni mtu wa mfumo na very loyal kwa Mwalimu Nyerere
Ahmed Rajab halikadhalika. Usuhuba(ukaribu) wake na Mwalimu ulikua ni zaidi ya Mwanasiasa na Mwanahabari. Hawa walikua marafiki na wandani(wasiri)
Rajab ni kati ya watu wachache sana ambao waliweza kumuandika(critically) Mwalimu na Nyerere akakaa kimya. Ni miongoni mwa watu walioweza kumtania kama alivyoonyesha mwenyewe kwenye hiyo makala yake hii na wakacheka
Ahmed Rajab na wengine wengi walikua ni wasiri wa Mwalimu Nyerere(na mfumo?). Aliwajenga, akawakuza na kisha akawasambaza kila mahali ndani na nje ya nchi.
Alifanya hivyo sio kwa maslahi ya yeye kubakia madarakani daima bali kuweka uwiano wa mamlaka ya nchi na taasisi zingine ikiwemo wanahabari ili kutengeneza watu na taifa alilolikusudia