Its Pancho
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 14,176
- 22,577
SIKU NITAKAPOKUFA ..01
AUTHOR: NEXT LEVEL.
Katika kila maisha ya binadamu kuna sehemu tunapitia na kukutana na majaribu ya kila aina mbalimbali, lakini kuna kuzaliwa kuishi na kufa, lakini Mimi siku nitakayokufa ...!siku nitakayokufa!..
Asubuhi na mapema jogoo anawika kuashiria kuwa watu waamke na kuanza shughuli zao za utafutaji, japo waliokereka na taarifa ya jogoo huyo kuwika kuashiria kuwa ni asubuhi kumekucha.
Mmojawapo alikuwa ni kijana mdogo Mussa matalu, alikuwa ni kijana wa miaka 16 tu, damu bado changa, mwili uliojengeka vizuri kutokana na kazi za suruba nyumbani kwao kwani yeye pekee ndiyo alikuwa kijana pekee wa kiume hapo kwao. "Wee mtoto utaendelea kulala mpaka saa ngapi?"
Huyo alikuwa ni baba wa damu wa mussa aliyejulikana kama mzee matalu, alikuwa mkali asiyependa mzaha kabisa wala utani wa kipuuzi.
Mussa aliamka harakaharaka kwani alielewa akiendelea kulala atachelewa shule na baba yake pia atamuadhibu.. Haraka akajiandaa na kutoka katika kibanda chake haraka kuelekea shule iliyojulikana kama WELLA SECONDARY.. Ilikuwa ni shule pekee kijijini hapo .
Oyaa mussa..!
Alikuwa na rafiki ake wa damu kabisa aliyejulikana kama Emanuel chigoni mwenyewe alijiita Emma uzo..Oya damu yangu nimepita kwenu bi mkubwa wako kasema umeshatangulia skuli nikaona nikufukuzie ..!
Mussa: aah we kila siku unachelewaa?
Imma uzo: aah mwanangu nilisahau kukuchana Jana si nilikuwa na mtoto Lydia?
Mussa: acha uzushi mtu mwenyewe utamuwezea wapi wewe?Ukweli ni kuwa mussa alipinga kwa nje lakini moyoni aliumia sana kwani hakuwahi kuwa na mpenzi tofauti na wanafunzi wenzake kama alivyo imma uzo angefanyaje na anawaogopa?
Alichoamua ni kubadilisha story maana imma hakuchelewa kuanza kumkandia kwamba kwanini hana demu..(mpenzi)
Well wanafika shuleni vijana hao wawili wa kidato cha NNE shuleni hapo . Baada ya mambo mengine kama usafi wanaenda mstarini (paredi) na kumkuta mwalimu mkuu amefura kwa hasira mithili ya chura mwenye mimba ..!
Kikawaida akiwa amekasirika basi huwa kunaKikawaida akiwa amekasirika basi huwa kuna jambo kubwa limemkasirisha ...alikuwa ni mwalimu DANIEL SHENDU.. Mkali mithili ya mbogo, ngozi yake nyeusi ya kung'aa, miwani yake ya macho aliyoining'iniza machoni pake ..hakuwa na utani hata kidogo.
Vijana kuna baadhi ya wanafunzi wanafanya shule kama ya wazazi wao, kwamba wanatenda wanavyojiskia "alianza mwalimu huyo"
Sasa basi ili kuonyesha mfano na onyo kwa wengine lazima sheria ifuatwe.
Erick mazinde..!, noel machemba.! Piteni mbele upesi.
AUTHOR: NEXT LEVEL.
Katika kila maisha ya binadamu kuna sehemu tunapitia na kukutana na majaribu ya kila aina mbalimbali, lakini kuna kuzaliwa kuishi na kufa, lakini Mimi siku nitakayokufa ...!siku nitakayokufa!..
Asubuhi na mapema jogoo anawika kuashiria kuwa watu waamke na kuanza shughuli zao za utafutaji, japo waliokereka na taarifa ya jogoo huyo kuwika kuashiria kuwa ni asubuhi kumekucha.
Mmojawapo alikuwa ni kijana mdogo Mussa matalu, alikuwa ni kijana wa miaka 16 tu, damu bado changa, mwili uliojengeka vizuri kutokana na kazi za suruba nyumbani kwao kwani yeye pekee ndiyo alikuwa kijana pekee wa kiume hapo kwao. "Wee mtoto utaendelea kulala mpaka saa ngapi?"
Huyo alikuwa ni baba wa damu wa mussa aliyejulikana kama mzee matalu, alikuwa mkali asiyependa mzaha kabisa wala utani wa kipuuzi.
Mussa aliamka harakaharaka kwani alielewa akiendelea kulala atachelewa shule na baba yake pia atamuadhibu.. Haraka akajiandaa na kutoka katika kibanda chake haraka kuelekea shule iliyojulikana kama WELLA SECONDARY.. Ilikuwa ni shule pekee kijijini hapo .
Oyaa mussa..!
Alikuwa na rafiki ake wa damu kabisa aliyejulikana kama Emanuel chigoni mwenyewe alijiita Emma uzo..Oya damu yangu nimepita kwenu bi mkubwa wako kasema umeshatangulia skuli nikaona nikufukuzie ..!
Mussa: aah we kila siku unachelewaa?
Imma uzo: aah mwanangu nilisahau kukuchana Jana si nilikuwa na mtoto Lydia?
Mussa: acha uzushi mtu mwenyewe utamuwezea wapi wewe?Ukweli ni kuwa mussa alipinga kwa nje lakini moyoni aliumia sana kwani hakuwahi kuwa na mpenzi tofauti na wanafunzi wenzake kama alivyo imma uzo angefanyaje na anawaogopa?
Alichoamua ni kubadilisha story maana imma hakuchelewa kuanza kumkandia kwamba kwanini hana demu..(mpenzi)
Well wanafika shuleni vijana hao wawili wa kidato cha NNE shuleni hapo . Baada ya mambo mengine kama usafi wanaenda mstarini (paredi) na kumkuta mwalimu mkuu amefura kwa hasira mithili ya chura mwenye mimba ..!
Kikawaida akiwa amekasirika basi huwa kunaKikawaida akiwa amekasirika basi huwa kuna jambo kubwa limemkasirisha ...alikuwa ni mwalimu DANIEL SHENDU.. Mkali mithili ya mbogo, ngozi yake nyeusi ya kung'aa, miwani yake ya macho aliyoining'iniza machoni pake ..hakuwa na utani hata kidogo.
Vijana kuna baadhi ya wanafunzi wanafanya shule kama ya wazazi wao, kwamba wanatenda wanavyojiskia "alianza mwalimu huyo"
Sasa basi ili kuonyesha mfano na onyo kwa wengine lazima sheria ifuatwe.
Erick mazinde..!, noel machemba.! Piteni mbele upesi.