Siku Nilipomsikia Nyerere Akilitangazia Taifa Kifo Cha Edward Moringe Sokoine

M M Mwanakijiji, hujajua hiyo ni mawazo ya majambazi? Huwa wana usemi "dead people dont talk" ukiona mtu anachangia hivyo jua ana element za kijambazi!

Na wewe ambae si jambazi unasema "dead people do talk"?

Kwi kwi kwi teh teh teh!
 
Yeah, it depends! Ila dead people talks, but for majambazi dead people dont talk! Matendo ya dead people talks! Dont you know that?
 
jambo jema hili,,,mjengwa umetenda,,,,,nakumbuka nilikuwa darasa la nne nulu shule ya msingi kule kwakoa wilayani mwanga k,njaro,wilaya yetu ilikuwa mpya,,,kuna mzee marehem sasa,hatib mwaluma baba temanyike,ndio alikua na radio mkulima anatembea nayo,,,,alisikia habari hiyo,,then,,tukakusanyika karibu kitongoji kizima,,,saa mbili usiku kwenye taarifa ya habari,,,,betri ziliuzwa duka la kijiji pekee,,,r.i.p. erdward moringe sokoine,,,,,,,,miaka ishirin baadae nilibahatika ksoma na kufanya kazi monduli,,,,nikajua nyumbani kake,jamii yake,,jimbo lake,,,,,nataman kuwa kama yeye,,japo kwa asilimia ishirin,,,,,,,
 
Kivipi wameigaragaza Tanzania? Ina maana hata baada ya miaka yote hii ambayo hawa watu wawili wamekuwa nje ya uongozi hatujapata dawa ya kutibu matatizo tuliyonayo? Kwani Nyerere ndio aliuza na kugawa bure rasilimali za nchi na akaleta siasa uchwara za kujuana na kulindana hata kama ni wahalifu? Inatusaidia nini tunapojaribu kusukumia matatizo yetu sisi watanzania wa leo kwa wakoloni, na Nyerere wakati tunaofanya maamuzi na kuendesha nchi ni sisi tena bila ushawishi wao?
Mkubwa tupende tusipende nyinyi mnaojiiita "system at work" ndio mnatugaragaza watanzania. Mko kimaslahi zaidi kuliko kikazi. Mna njaa za kupitiliza! Mnataka kuvuna msipopanda! Mnalea hata yasiyolelewa popote pale ulimwenguni. Hayo ni matatizo ya Nyerere na Sokoine au ni ya kwetu?


Ahsante sana Mkuu kwa maneno yaliyotulia na yenye hekima na busara tele.
 
Yes, Nyerere ndio alioitia Tanzania umaskini kwa kutokuweka misingi mizuri kwa miaka 24 aliyukuwa Rais. Kwa miaka 24 kila alichofanya kimekufa kabla ya yeye hajafa, kwa sababu alikuwa hajui akifanyacho.

Alidhulumu kwa kutaifisha mali za wanyonge wachche lakini magwiji walioijuwa dunia aliwashindwa, kesi nzuri ni ya LONRHO na Tiny Rowlands, alijaribu kumtaifisha huyu, akkakikwaa kisiki, ilibidi mwenyewe arudishe mali zake bila kupenda.

Tanganyika ilikuwa ni mchi ya kwanza katika Afrika kuuuza mazao nje, baada ya kuja Nyerere na siasa zake mbovu ikawa nchi maskini duniani na ikawa inaomba omba nje hata kula ikawa shida. Kaachia madaraka, mchi hii haina hata senti mbovu ya kigeni, viwanda vinakufa kwa kuliwa, ukabila idara zote za Serikali na Umma. Kila kitu hohehahe. Ardhi kubwa ya Tanzania kaigawia kanisa katoliki.

Unajuwa kuwa mmiliki mkubwa wa Ardhi Tanzania baada ya Serikali ni kanisa katoliki? Kwanini?

Kama wewe kweli uko kwenye system ambayo katika nchi yoyote inakuwa ndio moyo wa kusukuma "agenda" za nchi hiyo basi Tanzania kwishinei. Ina sikitisha kama Tanzania hii inaingiza kwenye system watu wasio na uwezo wala maarifa ya kutafuta majawabu ya matatizo yanayotuzunguka. Ina watu wenye kutafuta sifa na ukubwa bila kujua wataifanyia nini Tanzania. Kwasababu ya kukosa uwezo na maarifa, tunapotaka kuzungumzia tatizo lolote wao kwa kuhamaki wanatafuta jawabu rahisi ambalo ni udini na kumlaumu Nyerere. Bahati mbaya hata kama tunaendekeza udini na ulalamishi, time haitusubiri. Tuna nafasi ya kurekebisha mambo...maana Nyerere au Sokoine sio wanaokula kwa wizi fedha za walipa kodi wa leo wa Tanzania. Hawaendeshi serikali isiyojari hata bajeti yake na kufanya matumizi kinyume na taratibu. Hawaendeshi nchi ambayo waziri anaweza kutembea kama "warrior" na kuibiwa bunduki uchochoroni bunduki ambayo inapatikana jeshini tu na bado akaendelea kuachwa kwenye madaraka.
Kikulacho ki nguoni mwako. The way I see this life is different...ukombozi wangu unatokana na choices zangu. Simlaumu yoyote kwa kufika hapa nilipofikia maaana it my own choices that have led me into the destine I have been now. Nyinyi wazee wa system at work muendelee kwa mwendo huo huo...soon or later mtachukua nafasi zenu pale mnapostahili maana times change...na system nayo inachange.
 
Jambo la ajabu sana ni kuwa mavuvuzela ya CCM ya sasa hayataki kabisa sifa za uadilifu za Nyerere na Sokoine ziwe zinatajwa.Lakini hao viongozi wao wakiwa kwenye public wanajidai kusema viongozi hao wazamani ni mfano wa kuiga.Unafiki mtupu.

Naona wanasahau folosofia yenye kusema " Ufalme unaojaribu kusimama kwenye misingi ya uongo lazima utaanguka". Unafiki ndio utawaangusha wengi wa viongozi wetu wa leo siku zijazo. Maana tunayofanya gizani, with time yatakuja kujulikana nuruni. Kama mema, we will be covered...kama maovu, ndio hivyo tena!!!
 
Asante mjengwa kwa historia hiyo,mimi wakati huo nilikuwa darasa la sita,nakumbuka taarifa za kifo chake nilizisikia kutoka kwa mama yangu mzazi ambaye alisikiliza tangazo lililotolewa na rais wa wakati huo hayati nyerere.nakumbuka siku ya pili yake nikiwa shuleni tulijadili na wanafunzi wenzangu juu umakini aliokuwa nao sokoine katika uongozi.kweli tulimpoteza kiongozi mahiri.
 
Ni miongoni mwa viongoz wachache sana Tanzania hii na Afrika kwa ujumla kupata kuwepo, tusubir miaka 100 mingine labda anaweza tokea tena
 
kuna watu katika nchi hii wa ajabu sana.Ukimtaja Mwl Nyerere wanasema ni mfano wa kuigwa ukisema tuyafuate yale aliyoyaamini na ambayo ni mema kwa nchi wanaanza kumponda. Na cha ajabu wnasema ameua viwanda, kilimo nk lakini hawtaji mfano wa kiwanda kilichokufa wakati wa enzi ya Mwl. Nyerere. Na sishangai sn maana ni haohao waliozunguka nchi nzima wakiongozwa na nani yule sasa hivi ni marehemu yule aliyekuwa anahamasisha wenzake wawaue viongozi wa dini ya Kikristo hapa Tanzania, wakimlaani Mwl. Nyerere.

Tuwe wakweli Mwl. Nyerere pamoja na E.Sokoine walikuwa wazalendo wa kweli kwa Taifa lao. waliofuata mmmhhhhh!!!! uzalendo wao ni questionable
 
Hakuna alichodhibiti Sokoine, Nyerere ndio aliokuwa kinara wa kila kitu, Sokoine was just a vuvuzela, mechi wanacheza wengine.

Hakuna anaestahiki sifa, si Nyerere si Sokoine, wao ndio walioigaragaza Tanzania. Ukipenda usipende, hivyo ndivyo ilivyo.
Pls come up with supportive arguments kuonesha kwamba it was really nyerere who made us poor and not our ignorance uje na uthibitisho wa kisayansi na si porojo kama hizi unazopiga ambazo kila anayejisikia anaweza kuja nazo.
 
Maggid

Mimi nilikuwa na miaka saba, nakumbuka bibi yangu alilia sana

Nikamuuliza bibi unalia nini? akasema kiongozi mzuri wa nchi amekufa mjukuu wangu

kutoka hapo nikaanza kusikiliza nyimbo za maombolezo

Yes, I do remember though I was young
 
Nakumbuka nilikuwa naishu na Shangazi yangu mabibo..baada ya taarifa ile alitoa kilio utadhani amepoteza ndugu yake wa karibu
 
Unajuwa maana ya uadilifu au unajisemea tu? Anti Corruption ya Tanzania ilianzia awamu ya kwanza ikendeshwa na Maftah. Viwanda na mashamba alivyodhulumu Nyerere kwa mabepari vilianza kuliwa na kuuliwa wakati wa Nyerere. Viwanda alivyojengewa Nyerere na wachina, vilianza kuliwa na kuuliwa wakati huohuo wake. Mpaka anang'atuka, nchi iko hohehahe kwa uzembe na kutokuwajibika kwake na kwa viongozi aliowaweka madarakani, huo uadilifu unaousema wewe ni upi?

New year 2015! What is the story now??
 
Ndugu zangu watanzania tunahitaji viongozi kama akina Moringe Sokoine,Uongozi tulionao sasa umepoteza Nguvu na Mamlaka ndio maana nchi inakwenda kijingajinga tu,TAIFA letu Leo hii ni shamba LA bibi na tumeshuhudia sote Leo hii kwa macho na masikio yetu watu wanautaka Urais kwa udi na uvumba kana kwamba ni kitu cha mzahamzaha tu hata WAPUMBAVU,WASHENZI,WAHUNI,MALAYA,WEZI,MAFISADI na WAHUJUMU UCHUMI nao wanautaka URAIS na nafasi nyingine za uongozi.Inaumiza na inasikitisha sana kuona TAIFA lenye heshima leo limegeuza UONGOZI KUWA JAMBO LA MZAHAMZAHA TU KWA Sababu ya maslahi binafsi.Inauma sana kuona Tanzania ya leo inakosa Rais na Waziri MKUU makini,nguvu na mamlaka ya nchi vyote vimecolapse,vimepalalize. MUNGU AMPE PUMZIKO TAKATIFU KIONGOZI WETU MPENDWA EDWARD MORINGE SOKOINE.APUMZIKE KWA AMANI.
 
Kweli ni huzuni sana. NA kama ulivyosema kuwa akifufuka leo anaweza kuzimia tena ndani ya siku saba kutokana na hali ilivyo na aliyoiacha 1984.

Nakumbuka siku ile nilikuwa Shuleni pia, na majira ya saa SABA KASORO; tulikusanyika wote na Mwalimu Mkuu kwa huzuni alitangaza taarifa ya Kifo cha PM mpendwa Sokoine.

Nakumbuka wakati ule magazeti yalikuwa ni ya Chama na Serikali tu (Uhuru, Mzalendo, Daily News, Sunday News) KWa jinsi wananchi walivyoguswa na ule msiba nakumbuka kulikuwa na Foleni kubwa sana kila asubuhi katika vituo vya kuuza magazeti, na wengi walikuwa wanakosa.

Nakumbuka siku ya kusafirisha kwenda Arusha - Tulikuwa tunaishi Mbezi juu DSM, hivyo RTD walipotangaza kuwa ndege ndio inapaa uwanjani, na sisi ambao hatukuwa uwanjani tuliishuhudia ndege ya JESHI ikipaa hivyo tuliipepea mikono kwa huzuni kubwa ile ndege ikipaa na kuondoka.

NI HUZUNI SANA!!!!!!!!!!

Nashindwa kuendelea kwa uchungu!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Mkuu
Mizabwa mwl wako aliwezaje kutangaza kifo cha PM kabla ya rais?. Maana taarifa kamili ilitolewa saa za jioni na si mchana.
 
Back
Top Bottom