Siku nilipompiga mchawi

Papa Mobimba

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
1,153
1,359
Hiki ni kisa cha kweli. Kwa mtu ambaye ambaye haamini uchawi anaweza kuona ni kisa cha kutunga. Kisa hiki kilitokea katika mojawapo ya vijiji cha mikoa ya kanda ya Ziwa.

Saa saba usiku
Nashtuka usingizini nakusikia mtu akipiga mlango wa nyumba niliyokuwa nimelala. Nachungulia dirishani naona moto unawaka. Babu yangu alikuwa amekwisha nifundishi mambo ya kufanya ninapohisi kuna mchawi.

Naamua kutoka nje nikiwa na panga langu. Baada ya kufika nje mchawi anajaribu kukimbia. Anashindwa. Ananiongelesha lakini simjubi. Maana nikimjibu tu ana uwezo wa kutoweka. Huyu ni mama mmoja. Mtu mzima kidogo anaweza kuwa na miaka 70. Nikamfuata alipokuwa. Nikampiga kwa upande wa panga. Nikampiga kisawasawa. Akawa analia. Majirani wachache wanasikia. Akawa ananibembeleza, nimsamehe. Baada ya kumshushia kipigo, nikamwambia. Ondoa uwalete na wenzako.

Siku ya tatu
Siku tatu baada ya kumshushia kipigo, akaja mtoto wake wa kiume. Akaniambia nasikia ulitaka kumuua mama yangu. Nikamuambia. Sio mimi. Nilimpigia wapi? Akaondoka.

Wiki ya pili
Baada ya wiki mbili kupita bibi alinifuata nyumbani alikuwa amebeba kuku (jogoo) pamoja na unga wa mahindi kama amboni nne. Akaniambia nimekuletea mjukuu wangu. Usipopokea hivi vitu vyangu mimi nitakufa. Nikapokea vile vitu nikamtemea mate. Akaondoka.

Kuanzia siku hiyo nikawa nimekomesha michezo yote ya kijinga. Hata hivyo bado naishi kwa tahadhari kubwa. Naamini siku moja watarudi tena. Wachawi huwa hawakubali kushindwa ama kudhalilishwa. Wakirudi ama zangu ama zao!
 
Hiki ni kisa cha kweli. Kwa mtu ambaye ambaye haamini uchawi anaweza kuona ni kisa cha kutanga. Kisa hiki kilitokea katika mojawapo ya vijiji cha mikoa ya kanda ya Ziwa.

Saa saba usiku
Nashtuka usingizini nakusikia mtu akipiga mlango wa nyumba niliyokuwa nimelala. Nachungulia dirishani naona moto unawaka. Babu yangu alikuwa amekwisha nifundishi mambo ya kufanya ninapohisi kuna mchawi.

Naamua kutoka nje nikiwa na panga langu. Baada ya kufika nje mchawi anajaribu kukimbia. Anashindwa. Ananiongelesha lakini simjubi. Maana nikimjibu tu ana uwezo wa kutoweka. Huyu ni mama mmoja. Mtu mzima kidogo anaweza kuwa na miaka 70. Nikamfuata alipokuwa. Nikampiga kwa upande wa panga. Nikampiga kisawasawa. Akawa analia. Majirani wachache wanasikia. Akawa ananibembeleza, nimsamehe. Baada ya kumshushia kipigo, nikamwambia. Ondoa uwalete na wenzako.

Siku ya tatu
Siku tatu baada ya kumshushia kipigo, akaja mtoto wake wa kiume. Akaniambia nasikia ulitaka kumuua mama yangu. Nikamuambia. Sio mimi. Nilimpigia wapi? Akaondoka.

Wiki ya pili
Baada ya wiki mbili kupita bibi alinifuata nyumbani alikuwa amebeba kuku (jogoo) pamoja na unga wa mahindi kama amboni nne. Akaniambia nimekuletea mjukuu wangu. Usipopokea hivi vitu vyangu mimi nitakufa. Nikapokea vile vitu nikamtemea mate. Akaondoka.

Kuanzia siku hiyo nikawa nimekomesha michezo yote ya kijinga. Hata hivyo bado naishi kwa tahadhari kubwa. Naamini siku moja watarudi tena. Wachawi huwa hawakubali kushindwa ama kudhalilishwa. Wakirudi ama zangu ama zao!
Duh mkuu njoo inbox unifundishe namna ya kukamata wachawi
 
Hiki ni kisa cha kweli. Kwa mtu ambaye ambaye haamini uchawi anaweza kuona ni kisa cha kutanga. Kisa hiki kilitokea katika mojawapo ya vijiji cha mikoa ya kanda ya Ziwa.

Saa saba usiku
Nashtuka usingizini nakusikia mtu akipiga mlango wa nyumba niliyokuwa nimelala. Nachungulia dirishani naona moto unawaka. Babu yangu alikuwa amekwisha nifundishi mambo ya kufanya ninapohisi kuna mchawi.

Naamua kutoka nje nikiwa na panga langu. Baada ya kufika nje mchawi anajaribu kukimbia. Anashindwa. Ananiongelesha lakini simjubi. Maana nikimjibu tu ana uwezo wa kutoweka. Huyu ni mama mmoja. Mtu mzima kidogo anaweza kuwa na miaka 70. Nikamfuata alipokuwa. Nikampiga kwa upande wa panga. Nikampiga kisawasawa. Akawa analia. Majirani wachache wanasikia. Akawa ananibembeleza, nimsamehe. Baada ya kumshushia kipigo, nikamwambia. Ondoa uwalete na wenzako.

Siku ya tatu
Siku tatu baada ya kumshushia kipigo, akaja mtoto wake wa kiume. Akaniambia nasikia ulitaka kumuua mama yangu. Nikamuambia. Sio mimi. Nilimpigia wapi? Akaondoka.

Wiki ya pili
Baada ya wiki mbili kupita bibi alinifuata nyumbani alikuwa amebeba kuku (jogoo) pamoja na unga wa mahindi kama amboni nne. Akaniambia nimekuletea mjukuu wangu. Usipopokea hivi vitu vyangu mimi nitakufa. Nikapokea vile vitu nikamtemea mate. Akaondoka.

Kuanzia siku hiyo nikawa nimekomesha michezo yote ya kijinga. Hata hivyo bado naishi kwa tahadhari kubwa. Naamini siku moja watarudi tena. Wachawi huwa hawakubali kushindwa ama kudhalilishwa. Wakirudi ama zangu ama zao!
Wewe na huyo bibi wote wachawi sema wewe ni zaidi
 
Back
Top Bottom