Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 37,311
- 86,734
Hamjambo Wote!
1. Sijui kama naeleweka.
Yaani nikuumize, nikutese, nikuharibie maisha alafu Siku yamenipata ulete ngonjera za ajabuajabu. Sijui UTU. Sijui Imani!
2. Aiseeh! Hakuna cha utu kwa mtu asiye na Utu.
3. Hakuna cha staha sijui stara kwa watu waliokosa stara na stags.
4. Hakuna cha kuheshimu sijui ndugu za marehemu, Sijui watoto, sijui mke, sijui wazazi.
5. Hakuna! Kama niliwafanyia uhuni, ushenzi, niiwaumiza, niliwasumbua, niliwadhulumu.
6. Kwa nafasi Yangu, mkashindwa kunilipa roho zenu zisuuzike, mkabaki na kinyongo.
7. Aiseeh! Msiniletee unafiki wenu hapa.
Nipeni ninachostahili.
8. Wapeno familia Yangu inavyostahili.
9. Wapeni watoto wangu inavyostahili.
10. Kama Baba Yao sikuwa na heshima. Nilikuwa dhulmati na hawakuwahi kutoka kuzungumza jinsi ninavyotenda mabaya. Ni kwamba watoto wangu nao ni wanufaika na matendo ya mimi Baba yao.
11. Ikiwa Matendo hayo niliyafanya kwa siri, kiasi kwamba watoto wangu na familia Yangu isijue.
12. Basi muwahukumu watoto wangu kulingana na matendo yao. Na wala sio ya mimi Baba yao.
13. Wale watoto wangu wanaofanya matabia ya hovyo kama Mimi Baba yao basi waunganisheni kwenye adhabu yalawama na kejeli za Mimi Baba yao.
14. Lakini wale ambao ni watoto Wema licha ya mimi Baba yao kuwa Mbaya. Basi waoneeni jicho la Fadhili. Na wema.
15. Nataka kusema hivi;
16. Wewe Kama Baba yako ni mwenye heshima basi tutakuheshimu kwa heshima ya Babaako.
17. Halikadhalika, Kama Baba yako ni mshenzi basi tutakulaumu na kukudharau kwa makosa ya Baba yako.
18. Vingineyo ukiri na uwe tofauti na Babaako na useme hadharani kwa level ya uovu wa Babaako.
19. Masala ya Marehemu hasemwi ni Mila potofu za kizamani. Mimi hiyo Mila siitaki. Na Sisi Watibeli hatunaga Mila za kinafiki kama hizo.
20. Sisi Marehemu anapewa vidonge vyake. Na aliowaacha kama wananufaika na wema wake halikadhalika watahangaika kwa ubaya wake.
21. Sherehekeeni kifo changu. Zomeeni. Kejelini. Tukaneni
22. Kwa sababu sikuwa Mwema. Na ninastahili kufanyiwa hivyo.
23. Familia Yangu ndio vizuri ijisikie vibaya kwa kuwa na mtu mshenzi kutoka ukoo na familia yao.
24. Mama Yangu ajisikie vibaya kwa kuzaa na kunyonyesha toto lililoleta matatizo kwenye Dunia.
25. Lazima mwisho WA ubaya uwe Aibu.
Mwisho wa dhulma iwe fedheha na dharau.
27. Msisite na kamwe usionee huruma kumdharau mtu wa Aina Yangu ikiwa nilileta matatizo katika ulimwengu wa watu.
28. Hivyo ndivyo haki ilivyo.
29. Hata hivyo. Wale waliofanyiwa mabaya ni hiyari yao watoe msamaha na wala hawalazimishwi na yeyote.
Ni hiyari Yao kusema aaah! Tumuache.
30. Lakini sio mtu back ambaye hajui maumivu ya Mimi mtu mbadi ndio awe kiherehere ninapopewa haki Yangu kama marehemu mshenzi niliyeta matatizo duniani kwa watu wengi. Ili kwa pesa za dhulma na machozi ya watu nikuze watoto wangu
31. Kufikia hapo sina la ziada.
Ruhusa mayo na wala sitawalaumu.
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
1. Sijui kama naeleweka.
Yaani nikuumize, nikutese, nikuharibie maisha alafu Siku yamenipata ulete ngonjera za ajabuajabu. Sijui UTU. Sijui Imani!
2. Aiseeh! Hakuna cha utu kwa mtu asiye na Utu.
3. Hakuna cha staha sijui stara kwa watu waliokosa stara na stags.
4. Hakuna cha kuheshimu sijui ndugu za marehemu, Sijui watoto, sijui mke, sijui wazazi.
5. Hakuna! Kama niliwafanyia uhuni, ushenzi, niiwaumiza, niliwasumbua, niliwadhulumu.
6. Kwa nafasi Yangu, mkashindwa kunilipa roho zenu zisuuzike, mkabaki na kinyongo.
7. Aiseeh! Msiniletee unafiki wenu hapa.
Nipeni ninachostahili.
8. Wapeno familia Yangu inavyostahili.
9. Wapeni watoto wangu inavyostahili.
10. Kama Baba Yao sikuwa na heshima. Nilikuwa dhulmati na hawakuwahi kutoka kuzungumza jinsi ninavyotenda mabaya. Ni kwamba watoto wangu nao ni wanufaika na matendo ya mimi Baba yao.
11. Ikiwa Matendo hayo niliyafanya kwa siri, kiasi kwamba watoto wangu na familia Yangu isijue.
12. Basi muwahukumu watoto wangu kulingana na matendo yao. Na wala sio ya mimi Baba yao.
13. Wale watoto wangu wanaofanya matabia ya hovyo kama Mimi Baba yao basi waunganisheni kwenye adhabu yalawama na kejeli za Mimi Baba yao.
14. Lakini wale ambao ni watoto Wema licha ya mimi Baba yao kuwa Mbaya. Basi waoneeni jicho la Fadhili. Na wema.
15. Nataka kusema hivi;
16. Wewe Kama Baba yako ni mwenye heshima basi tutakuheshimu kwa heshima ya Babaako.
17. Halikadhalika, Kama Baba yako ni mshenzi basi tutakulaumu na kukudharau kwa makosa ya Baba yako.
18. Vingineyo ukiri na uwe tofauti na Babaako na useme hadharani kwa level ya uovu wa Babaako.
19. Masala ya Marehemu hasemwi ni Mila potofu za kizamani. Mimi hiyo Mila siitaki. Na Sisi Watibeli hatunaga Mila za kinafiki kama hizo.
20. Sisi Marehemu anapewa vidonge vyake. Na aliowaacha kama wananufaika na wema wake halikadhalika watahangaika kwa ubaya wake.
21. Sherehekeeni kifo changu. Zomeeni. Kejelini. Tukaneni
22. Kwa sababu sikuwa Mwema. Na ninastahili kufanyiwa hivyo.
23. Familia Yangu ndio vizuri ijisikie vibaya kwa kuwa na mtu mshenzi kutoka ukoo na familia yao.
24. Mama Yangu ajisikie vibaya kwa kuzaa na kunyonyesha toto lililoleta matatizo kwenye Dunia.
25. Lazima mwisho WA ubaya uwe Aibu.
Mwisho wa dhulma iwe fedheha na dharau.
27. Msisite na kamwe usionee huruma kumdharau mtu wa Aina Yangu ikiwa nilileta matatizo katika ulimwengu wa watu.
28. Hivyo ndivyo haki ilivyo.
29. Hata hivyo. Wale waliofanyiwa mabaya ni hiyari yao watoe msamaha na wala hawalazimishwi na yeyote.
Ni hiyari Yao kusema aaah! Tumuache.
30. Lakini sio mtu back ambaye hajui maumivu ya Mimi mtu mbadi ndio awe kiherehere ninapopewa haki Yangu kama marehemu mshenzi niliyeta matatizo duniani kwa watu wengi. Ili kwa pesa za dhulma na machozi ya watu nikuze watoto wangu
31. Kufikia hapo sina la ziada.
Ruhusa mayo na wala sitawalaumu.
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam