Siku Musa alipoikataa nyumba ya Farao na Siasa za Tanzania

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Na. M. M. Mwanakijiji

Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao. Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu. (Waeb. 11:24,25)

Mojawapo ya masimulizi ya vitabu vya dini za Kikristu na Kiislamu ambayo yanakubaliana sana na kulingana kwa kiasi kikubwa ni lile simulizi la Nabii Musa. Jinsi gani alizaliwa, wapi alizaliwa, kwanini alitelekezwa, na jinsi gani mama yake alipata nafasi ya kumnyonyesha kwa ruhusa na baraka ya nyumba ya Farao (Firauni – nitatumia maneno haya kwa kubadilishana) yote yanalingana sana.

Na pia jinsi ambavyo ilimlazimu Musa kuikimbia nyumba ya Farao na fahari zake zote, utajiri wake na elimu yote ambayo aliipata kule na kwenda kuunganika na Wanawaisraeli waliokuwa Utumwani kule Misri na kwa uamuzi wake huo kujiweka kuwa ni adui wa kudumu wa Farao.

Haya yote yanaonekana katika Agano la Kale la Biblia Takatifu na katika Qurani Tukufu. Hata hivyo, kwa namna ya pekee mwandishi wa kitabu cha Waebrania anatueleza kwa namna ya pekee kabisa ni kwa sababu gani Musa aliicha nyumba ya Firauni. Mwandishi anasema "Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima".....


.....Watanzania wenzangu, mnaweza kufikiria nazungumzia habari za dini. Kwa namna fulani inaweza kugusa dini lakini hayo nitawaachia wachungaji, mapadre, mashehe na walimu mbalimbali wa dini.



Mimi nazungumzia haja na ulazima wa watoto wa Tanzania kukataa kuitwa wana na mabinti wa Utawala wa Kifisadi! Simzungumzii Musa wa Biblia wala Farao wa Misri; siwazungumzii wana Waisraeli wa Mashariki ya kati. Nazungumzia mahusiano kati ya watawala na watawaliwa wa hapa Tanzania....


Makala hii imetoka kwenye Tanzania Daima.
 

Attachments

  • Musakumkataafarao2.doc
    62.5 KB · Views: 171
Last edited:
Asante MMKJJ kwa simulizi mwananana ya Siku Musa alipoikataa Nyumba ya Farao na Maamuzi ya Mtu Mzima.

Niko na wewe katika maamuzi ya Musa alipokuwa mtu mzima akaamua kuikataa nyumba ya Farao, ila siko na wewe katika Watu wazima wetu unaodhani wamekuwa Watu wazima ukiamini watakuwa tayari kuikataa nyumba ya Farao, umepotea.

Enzi za Musa kulikuwa na genuinity na drive behind ni uchungu wa dhati dhidi ya nduguze Waebrania. Watu wazima wenu ni wanafiki na drive behind sio uchungu kwa Watanzania, bali wana agenda zao, na amini usiamini the drive behind ni njaa zao, hata kama kiranja anaonekana ni mtu wa shibe, tajiri na msamaria mwema lakini pia ana lake jambo, the bottom line ni njaa. Sio lazima njaa ya tumbo, hata njaa ya madaraka ni njaa. Njaa ya kutaka kuabudiwa ni njaa, njaa ya kulalamika kila siku kuwa unaonewa pia ni njaa.

Unafiki ninaouna hapa ni kujidai umekuwa mtu mzima kutaka kuondoka nyumba ya Farao huku unamkumbatia huyo huyo Firauni. Hivi anayeongoza Misri ni nani?. Ni Farao, maroroso yote yanayotokea Misri kuwanyanyasa wana wa Israel, yanabaraka za Farao, Musa alimkataa Farao na mambo yake yote. Watu wazima wetu, wanamkubali Farao ila wanayakataa mambo yake yote kama alivyofanya Mrema 1995. Hawa waliobaki ni wanafiki tuu na hili litathibitishwa with time.

Mzee Mwanakijiji nakuaminia kwa insight uliyonayo, lazima unaweza kuona ajenda ya kiranja wao anayepiga kelele za ufisadi huku ana ajenda yake akimpaka mafuta Farao kwa mgongo wa Chupa, eti "ni rafiki yangu mkubwa"?!. Kwa vile saa hizi ni kelele za ufisadi zimepamba moto, tuwe wote kwenye hili, ajenda zitakapoibuka, tutafarakana maana kitakacho fuatia ni anguko la wanafiki.
 
Surely MKJJ tatizo ni kuwa kabla Mussa hajaenda kwenye jengo la kifalme alizaliwa huko 'tandale' akatupwa mtoni na kama zali akaingia Ikulu.

Baadae alijijua kuwa yeye ni mwebrania na akawatetea watu wake.

Lazima tukae chini kutafakari je, ufisadi unaanzia mara tu mtu anapopata uwaziri au urais?? au unaanzia huku kwenye kata, mashuleni, kwenye taasisi za umma, michezo....then tunawachagua mafisadi wakubwa zaidi kuwa viongozi!

Tunakazi tunatakiwa kupigwa shule ya Mungu! Jangwani Miaka 40! hili watanzania hatutaki kulisikia!
 
Na. M. M. Mwanakijiji


Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao. Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu. (Waeb. 11:24,25)

Mojawapo ya masimulizi ya vitabu vya dini za Kikristu na Kiislamu ambayo yanakubaliana sana na kulingana kwa kiasi kikubwa ni lile simulizi la Nabii Musa. Jinsi gani alizaliwa, wapi alizaliwa, kwanini alitelekezwa, na jinsi gani mama yake alipata nafasi ya kumnyonyesha kwa ruhusa na baraka ya nyumba ya Farao (Firauni – nitatumia maneno haya kwa kubadilishana) yote yanalingana sana.

Na pia jinsi ambavyo ilimlazimu Musa kuikimbia nyumba ya Farao na fahari zake zote, utajiri wake na elimu yote ambayo aliipata kule na kwenda kuunganika na Wanawaisraeli waliokuwa Utumwani kule Misri na kwa uamuzi wake huo kujiweka kuwa ni adui wa kudumu wa Farao.

Haya yote yanaonekana katika Agano la Kale la Biblia Takatifu na katika Qurani Tukufu. Hata hivyo, kwa namna ya pekee mwandishi wa kitabu cha Waebrania anatueleza kwa namna ya pekee kabisa ni kwa sababu gani Musa aliicha nyumba ya Firauni. Mwandishi anasema “Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima”.....


.....Watanzania wenzangu, mnaweza kufikiria nazungumzia habari za dini. Kwa namna fulani inaweza kugusa dini lakini hayo nitawaachia wachungaji, mapadre, mashehe na walimu mbalimbali wa dini.



Mimi nazungumzia haja na ulazima wa watoto wa Tanzania kukataa kuitwa wana na mabinti wa Utawala wa Kifisadi! Simzungumzii Musa wa Biblia wala Farao wa Misri; siwazungumzii wana Waisraeli wa Mashariki ya kati. Nazungumzia mahusiano kati ya watawala na watawaliwa wa hapa Tanzania....


Jipatie nakala yako hapa.

Mzee MM what if you would try to be David and not Moses? Chukua kombeo achilia jiwe kwenye paji la uso wa Goliat na sisi wakike tutakupokea kwa kelele za Mfalme aliua elfu lakini Daudi ameua makumi elfu. Alafu unajua nini ile technology ya Musa ya kugawa bahari ya Sham kwa fimbo imepitwa na wakati ipo hii ya 21st century ya mwanaume wa wanaume yeye anaenda against natural forces hahitaji kugawa maji na kupita nchi kavu yeye anatembea juu ya maji bila kuzama. Unaionaje hii kwanini utumie analogy (sp?) technology wakati ni enzi za electronics hizi. Enzi hizo za Musa walitakiwa kusoma mbao za mawe kuzijua sheria siku hizi tunatembea nazo ndani mwetu na tunauwezo wa kuinfluence hata wasio penda kwasababu tunazo funguo. "All the powers and authority is given to me and I am giving them to u to go and make my desciples!" But why are the sons and daughters of the King live like slaves? Because they are hold captive at the will of the devil; for these they dont need prayer they need the knowldge of their father for they resist themselves; but with them I command u to instruct them humbly with patience and all deligence as they are not like Yambre and .... who withstood Moses for these I tell u turn away from them as they are always searching truth while denying it and because of their nature they will never find it; they covet; sleeping inside the widowed houses, Idiolators; people of no faith; hypochrites, wicked and witches...for them the end is near for they will not continue for so long before they fall.
 
Watoto wa tanzania wakubali kuwa ufisadi na mafisadi, na si kitu kingine, ndicho kincholeta umasikini wa nchi hii, halafu waendelee bila kumtazama mtu usoni, In ballot box kusema SASA BASI... INATOSHA.
 
Off tangent, ku attribute hizi story kwenye bible ni sawasawa na ku-attribute "The Merchants of Venice" kwa wasemaji wa kiswahili kwa J.K Nyerere, bila kumtaja William Shakespeare.

Hizi story zilikuwapo kabla ya Musa na Webrania walikuwa wasanii tu walio zi plagiarize na kuzifanya zao.

I get your deeper meaning, though I am appalled by the level of miseducation carried by the his-story behind, although the intentions are good, the effect is further miseducation.

A 4.6 BILLION YEAR OLD PROPHECY

And then there is the plagiarized story of Moses. Upon Moses' birth, it is said that he was placed in a reed basket and set adrift in a river in order to avoid infanticide. He was later rescued by a daughter of royalty and raised by her as a Prince.36 This baby in a basket story was lifted directly from the myth of Sargon of Akkad of around 2250 BC. Sargon was born, placed in a reed basket in order to avoid infanticide, and set adrift in a river. He was in turn rescued and raised by Akki, a royal mid-wife.37, 38

Furthermore, Moses is known as the Law Giver, the giver of the Ten Commandments, the Mosaic Law.39 However, the idea of a Law being passed from God to a prophet on a mountain is also a very old motif. Moses is just a law giver in a long line of law givers in mythological history.40 In India, Manou was the great law giver.41 In Crete, Minos ascended Mount Dicta, where Zeus gave him the sacred laws.42 While in Egypt there was Moses, who carried stone tablets and upon them the laws of god were written.43

And as far as the Ten Commandments, they are taken outright from Spell 125 of the Egyptian Book of the Dead.44 What the Book of the Dead phrased "I have not stolen" became "Thou shall not steal," "I have not killed" became "Thou shall not kill," "I have not told lies" became "Thou shall not bear false witness" and so forth.45 In fact, the Egyptian religion is likely the primary foundational basis for the Judeo-Christian theology. Baptism,46 afterlife,47 final judgment, 48 virgin birth 49 and resurrection,50 crucifixion,51 the ark of the covenant,52 circumcision,53, 54 saviors,55 holy communion,56 the great flood,57 Easter,58 Christmas,59, 60 Passover,61 and many, many more, are all attributes of Egyptian ideas, long predating Christianity and Judaism.

Justin Martyr, one of the first Christian historians and defenders, wrote: "When we say that he, Jesus Christ, our teacher, was produced without sexual union, was crucified and died, and rose again, and ascended into Heaven, we propound nothing different from what you believe regarding those who you esteem Sons of Jupiter."62 In a different writing, Justin Martyr said "He was born of a virgin; accept this in common with what you believe of Perseus."63 It's obvious that Justin and other early Christians knew how similar Christianity was to the Pagan religions. However, Justin had a solution. As far as he was concerned, the Devil did it. The Devil had the foresight to come before Christ, and create these characteristics in the Pagan world.64
 
Aaaah wewe na hii mi conspiracy theories yako bana....

Hakuna conspiracy theory unapoiona, hiyo niliyotoa hapo ni expose ya conspiracy theory, the conspiracy theory being the bible.

The bible authors conspired to monopolize world culture and religion by plagiarizing and faking these story as their own.

Who is giving a conspiracy theory now?
 
Hakuna conspiracy theory unapoiona, hiyo niliyotoa hapo ni expose ya conspiracy theory, the conspiracy theory being the bible.

The bible authors conspired to monopolize world culture and religion by plagiarizing and faking these story as their own.

Who is giving a conspiracy theory now?

The one saying the bible is a conspiracy....
 
wabongo ndivyo tulivyo; Bluray, ukitaka kuzungumzia the history of the bible, the conspiracy and whatever have you why not start a thread kule kwingine bila ya kulazimika kuhijack mada nyingine?

Haya ya kusema kuplagiarize mbona hadithi zetu nyingi za sungura na fisi ambazo tuliamini ni za kiafrika kumbe msingi wake ni hadithi za Hisopo (Aesop). Sasa ndiyo ulimwengu ulivyo na mfano wa Musa hapa hauna lengo la kuzungumzia bible authorship (kama ni ya kiungu au ya kibinadamu).

Ndio maana nimesema hapo juu "mimi nazungumzia...".

Mfano niliotumia wa Musa was not intended to be "all inclusive" na kufananisha kila kitu kwa kila jambo kama wengine wanavyochukulia.

Kwamba Musa aliweza kuikataa nyumba ya farao yawezekana kulisababisha na hali halisi iliyomkuta na bila ya shaka haikuwa jambo jepesi lakini alijua ni la lazima.

Ujumbe ni kuwa kuna wakati mtu mzima anatakiwa kuchukua
 
Tusubiri Mh Zitto na yeye achangie,naona amepotea sana hapa forum,nadhani atakuwa anaifahamu torati kwani yeye kama Muslim,anashare torati na christians.
 
Back
Top Bottom