Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Na. M. M. Mwanakijiji
Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao. Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu. (Waeb. 11:24,25)
Mojawapo ya masimulizi ya vitabu vya dini za Kikristu na Kiislamu ambayo yanakubaliana sana na kulingana kwa kiasi kikubwa ni lile simulizi la Nabii Musa. Jinsi gani alizaliwa, wapi alizaliwa, kwanini alitelekezwa, na jinsi gani mama yake alipata nafasi ya kumnyonyesha kwa ruhusa na baraka ya nyumba ya Farao (Firauni – nitatumia maneno haya kwa kubadilishana) yote yanalingana sana.
Na pia jinsi ambavyo ilimlazimu Musa kuikimbia nyumba ya Farao na fahari zake zote, utajiri wake na elimu yote ambayo aliipata kule na kwenda kuunganika na Wanawaisraeli waliokuwa Utumwani kule Misri na kwa uamuzi wake huo kujiweka kuwa ni adui wa kudumu wa Farao.
Haya yote yanaonekana katika Agano la Kale la Biblia Takatifu na katika Qurani Tukufu. Hata hivyo, kwa namna ya pekee mwandishi wa kitabu cha Waebrania anatueleza kwa namna ya pekee kabisa ni kwa sababu gani Musa aliicha nyumba ya Firauni. Mwandishi anasema "Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima".....
.....Watanzania wenzangu, mnaweza kufikiria nazungumzia habari za dini. Kwa namna fulani inaweza kugusa dini lakini hayo nitawaachia wachungaji, mapadre, mashehe na walimu mbalimbali wa dini.
Mimi nazungumzia haja na ulazima wa watoto wa Tanzania kukataa kuitwa wana na mabinti wa Utawala wa Kifisadi! Simzungumzii Musa wa Biblia wala Farao wa Misri; siwazungumzii wana Waisraeli wa Mashariki ya kati. Nazungumzia mahusiano kati ya watawala na watawaliwa wa hapa Tanzania....
Makala hii imetoka kwenye Tanzania Daima.
Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao. Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu. (Waeb. 11:24,25)
Mojawapo ya masimulizi ya vitabu vya dini za Kikristu na Kiislamu ambayo yanakubaliana sana na kulingana kwa kiasi kikubwa ni lile simulizi la Nabii Musa. Jinsi gani alizaliwa, wapi alizaliwa, kwanini alitelekezwa, na jinsi gani mama yake alipata nafasi ya kumnyonyesha kwa ruhusa na baraka ya nyumba ya Farao (Firauni – nitatumia maneno haya kwa kubadilishana) yote yanalingana sana.
Na pia jinsi ambavyo ilimlazimu Musa kuikimbia nyumba ya Farao na fahari zake zote, utajiri wake na elimu yote ambayo aliipata kule na kwenda kuunganika na Wanawaisraeli waliokuwa Utumwani kule Misri na kwa uamuzi wake huo kujiweka kuwa ni adui wa kudumu wa Farao.
Haya yote yanaonekana katika Agano la Kale la Biblia Takatifu na katika Qurani Tukufu. Hata hivyo, kwa namna ya pekee mwandishi wa kitabu cha Waebrania anatueleza kwa namna ya pekee kabisa ni kwa sababu gani Musa aliicha nyumba ya Firauni. Mwandishi anasema "Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima".....
.....Watanzania wenzangu, mnaweza kufikiria nazungumzia habari za dini. Kwa namna fulani inaweza kugusa dini lakini hayo nitawaachia wachungaji, mapadre, mashehe na walimu mbalimbali wa dini.
Mimi nazungumzia haja na ulazima wa watoto wa Tanzania kukataa kuitwa wana na mabinti wa Utawala wa Kifisadi! Simzungumzii Musa wa Biblia wala Farao wa Misri; siwazungumzii wana Waisraeli wa Mashariki ya kati. Nazungumzia mahusiano kati ya watawala na watawaliwa wa hapa Tanzania....
Makala hii imetoka kwenye Tanzania Daima.
Attachments
Last edited: