Siku moja na Sheikh Ponda Mahakamani Morogoro 2015

Pamoja na kumkubali sana Sheikh Ponda lakini jambo moja najiuliza, kiwanja cha kujenga chuo kikuu kinabadirishwa na kujengwa msikiti? Hivi Morogoro misikiti imejaa kiasi kwamba chuo kikuu kiwe hakina maana tena badala yake pajengwe msikiti? Hi inanifikirisha kidogo
Mazindu...
Kuna kisa ambacho hukijui.

EAMWS ilikuwa inajenga chuo kikuu mwaka wa 1968.

Bahati mbaya sana ikatokea fitna.

Pakawa na hofu kwa nini Waislam wawe na Chuo Kikuu?

Ukazushwa mgogoro mkubwa ndani ya EAMWS na serikali ilihusika katika fitna hii kwa kiasi kikubwa.

Serikali ikaipiga marufuku EAMWS na ikawaundia Waislam BAKWATA.

Mradi wa Chuo Kikuu na miradi ya ujenzi wa shule yote ikafa.

Kiwanja hiki kikawa sasa BAKWATA wanawauzia matajiri.

Pale Sheikh Ponda alipofikia kuchukua kiwanja katika hilo eneo ili ujengwe msikiti kiwanja chote kilikuwa kimemalizika kuuzwa.

Ponda alichukua sehemu ile ndogo ili angalau pawe kumbukumbu kwa ajili ya Sheikh Hassan bin Ameir.

Rudia kusoma kisa hiki utaelewa vizuri.
 
Mzee Said, hivi Mzee Waikela bado yupo hai? Mwamba sana huyu mzee..Namkumbuka alikuwa anakaa mtaan Ng'ambo au Kanyeye. Ni mzee anayeheshimika Sana na waislamu na wanaharakati. Ni mtu mwenye kauli thabiti! Huwezi taja uhuru wa Tanganyika bila kulitaja jina la huyu mzee ( hii ni kwa watu maalumu tu wanaojua mchango wake kwenye uhuru wa Tanganyika)
Last...
Mzee Waikela yu hai.
 
Mazindu...
Kuna kisa ambacho hukijui.

EAMWS ilikuwa inajenga chuo kikuu mwaka wa 1968.

Bahati mbaya sana ikatokea fitna.

Pakawa na hofu kwa nini Waislam wawe na Chuo Kikuu?

Ukazushwa mgogoro mkubwa ndani ya EAMWS na serikali ilihusika katika fitna hii kwa kiasi kikubwa.

Serikali ikaipiga marufuku EAMWS na ikawaundia Waislam BAKWATA.

Mradi wa Chuo Kikuu na miradi ya ujenzi wa shule yote ikafa.

Kiwanja hiki kikawa sasa BAKWATA wanawauzia matajiri.

Pale Sheikh Ponda alipofikia kuchukua kiwanja katika hilo eneo ili ujengwe msikiti kiwanja chote kilikuwa kimemalizika kuuzwa.

Ponda alichukua sehemu ile ndogo ili angalau pawe kumbukumbu kwa ajili ya Sheikh Hassan bin Ameir.

Rudia kusoma kisa hiki utaelewa vizuri.
Sawa mzee wangu, nimekuelewa. Tuendelee na mjadara
 
Last...
Mzee Waikela yu hai.
Afadhali.. udongo wa mjerumani ule. Nadhani atakuwa na miaka 90 na zaidi sasa. Alikuwa rafiki mkubwa wa Babu yangu. Akinituma nimpelekee barua ya vikao mbalimbali Tabora miaka ya 90 mwanzoni. Namjua vizuri. Mwamba sana yule mzee
 
Afadhali.. udongo wa mjerumani ule. Nadhani atakuwa na miaka 90 na zaidi sasa. Alikuwa rafiki mkubwa wa Babu yangu. Akinituma nimpelekee barua ya vikao mbalimbali Tabora miaka ya 90 mwanzoni. Namjua vizuri. Mwamba sana yule mzee
Last Emperor,
Kuna watu wanne katika historia ya Tanganyika ambao wamekabiliana na Julius Nyerere uso kwa macho baada ya kupishana katika mambo muhimu ya siasa katika TANU na wakasema maneno makali.

Mtu wa kwanza ni Sheikh Suleiman Takadir (1958), Titi Mohamed (1963),Bilali Rehani Waikela (1963) na Schneider Abdillah Plantan (1965?).

Hakika Bilali Rehani Waikela ni mwamba.

Yeye alikuwa katika kamati ya Waislam iliyochaguliwa kufanya sulhu kati ya EAMWS na kundi dogo la Waislam wenye nguvu na ushawishi mkubwa ndani yaTANU na serikali ambao walikuwa wanataka EAMWS ivunjwe.

Kiongozi wa kamati hii alikuwa Mussa Kwikima.
Baada ya kushindakana kupatikana sulhu serikali iliivunja EAMWS na kuunda BAKWATA.

Baada ya hapo ikatoka amri kuwa nyaraka zote za mgogoro ule zichomwe moto zisiwepo na atakaekutwa na nyaraka hizo atashughulikiwa.

Inaelekea wajumbe wa kamati ile wote walizichoma moto nyaraka zao.
Bilal Rehani Waikela yeye nyaraka zake alizificha mahali kwa muda wa takriban miaka 20.

Katika miaka ya 80 alizichukua nyaraka zile akampa kijana mmoja kutoka Tabora jina lake Mohamed Lulengelule ambae alikuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na kiongozi wa Muslim Students Association of the University of Dar es Salaam (MSAUD) azifikishe Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam zihifadhiwe.

Hivi ndivyo mimi Nyaraka za Waikela zilivyoweza kunifikia na nikazisoma zote.

Nyaraka hizi ni ''minutes'' za mikutano, taarifa za kamati, ''cuttings'' za magazeti The Nationalist, Tanganyika Standard nk. nk.

Kutokana na Nyaraka za Waikela nikaandika paper, ''Islam and Politics in Tanzania,'' (1989) paper ambayo niliwasilisha kwenye mkutano Nairobi mwaka wa wa 1989.

Unaweza kuipata hapa: “Islam and Politics in Tanzania,” (1989) Al Haq International Karachi, Vol 1/No. 3 August - December, 1993.

Hii paper nimeitia kama sehemu ya tatu na ya mwisho katika kitabu cha Abdul Sykes.

Nilikutana na Mzee Waikela nyumbani kwake Gongoni Tabora na elimu aliyonipa kuhusu uhuru wa Tanganyika na mchango wa Waislam nisingeweza kuipata popote.

Hakika nakubaliana na wewe unaposema Mzee Waikela ni mwamba.
Mimi nakuongezea lingine Mzee Waikela ana hazina kubwa kichwani kwake.

Laiti kama asingehifadhi zile nyaraka historia ya kuundwa kwa BAKWATA isingefahamika.
 
Last Emperor,
Kuna watu wanne katika historia ya Tanganyika ambao wamekabiliana na Julius Nyerere uso kwa macho baada ya kupishana katika mambo muhimu ya siasa katika TANU na wakasema maneno makali.

Mtu wa kwanza ni Sheikh Suleiman Takadir (1958), Titi Mohamed (1963),Bilali Rehani Waikela (1963) na Schneider Abdillah Plantan (1965?).

Hakika Bilali Rehani Waikela ni mwamba.

Yeye alikuwa katika kamati ya Waislam iliyochaguliwa kufanya sulhu kati ya EAMWS na kundi dogo la Waislam wenye nguvu na ushawishi mkubwa ndani yaTANU na serikali ambao walikuwa wanataka EAMWS ivunjwe.

Kiongozi wa kamati hii alikuwa Mussa Kwikima.
Baada ya kushindakana kupatikana sulhu serikali iliivunja EAMWS na kuunda BAKWATA.

Baada ya hapo ikatoka amri kuwa nyaraka zote za mgogoro ule zichomwe moto zisiwepo na atakaekutwa na nyaraka hizo atashughulikiwa.

Inaelekea wajumbe wa kamati ile wote walizichoma moto nyaraka zao.
Bilal Rehani Waikela yeye nyaraka zake alizificha mahali kwa muda wa takriban miaka 20.

Katika miaka ya 80 alizichukua nyaraka zile akampa kijana mmoja kutoka Tabora jina lake Mohamed Lulengelule ambae alikuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na kiongozi wa Muslim Students Association of the University of Dar es Salaam (MSAUD) azifikishe Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam zihifadhiwe.

Hivi ndivyo mimi Nyaraka za Waikela zilivyoweza kunifikia na nikazisoma zote.

Nyaraka hizi ni ''minutes'' za mikutano, taarifa za kamati, ''cuttings'' za magazeti The Nationalist, Tanganyika Standard nk. nk.

Kutokana na Nyaraka za Waikela nikaandika paper, ''Islam and Politics in Tanzania,'' (1989) paper ambayo niliwasilisha kwenye mkutano Nairobi mwaka wa wa 1989.

Unaweza kuipata hapa: “Islam and Politics in Tanzania,” (1989) Al Haq International Karachi, Vol 1/No. 3 August - December, 1993.

Hii paper nimeitia kama sehemu ya tatu na ya mwisho katika kitabu cha Abdul Sykes.

Nilikutana na Mzee Waikela nyumbani kwake Gongoni Tabora na elimu aliyonipa kuhusu uhuru wa Tanganyika na mchango wa Waislam nisingeweza kuipata popote.

Hakika nakubaliana na wewe unaposema Mzee Waikela ni mwamba.
Mimi nakuongezea lingine Mzee Waikela ana hazina kubwa kichwani kwake.

Laiti kama asingehifadhi zile nyaraka historia ya kuundwa kwa BAKWATA isingefahamika.
HAKIKA!!!
 
Asante sana kwakuendelea kutupa historia hususani mchango wa waislamu ktk kupigania uhuru wa nchi.
Hakuna asiyetambua nguvu kubwa ya waislam ktk kupata uhuru na hatimaye kuundwa serikali ya kizalendo.
Lkn ifike pahala waislam wakiongozwa na wazee kama nyie waache kulia lia. Yapo makundi mengi tofauti yaliporwa mali zao/nyadhifa/haki na serikali ya kizalenfo.

Wapo machifu waliolazimishwa kuacha milki na tawala zao wakabaki machiefu jina. Hawa machifu walikuwa na ardhi, majeshi, utawala na maamuzi, walikusanya kodi n.k, lkn kwa kuwa walielewa serikali ya kizalendo nini wakaacha vyote wakaunga mkono juhudi.

Zipo taasisi za kidini za kikristo, hizi zilihodhi karibia kila sekta ya huduma na uchumi, kuanzia mahospitali, mashamba, shule, vyuo, mifugo nk. Tena hawa ndio walifilisiwa kweli kweli lkn waliunga mkono juhudi na wakakubali kuanza upya.

Sasa shida ipo kwa waislam tena wachache sana wakiongozwa na wazee wenye mawazo mgando kuaminisha umma kama wameonewa kuliko makundi yawayo tanganyika.
Camon people let us be positive, to hell with these -ve thinkings
Kwa uelewa wangu hizo mali za Waisilamu kwa kipindi hicho hazikutakiwa kupelekwa BAKWATA kwa kuwa BAKWATA sio Serikali. Ilitakiwa zibinafsishwe na zirudishwe Serikalini kama ilivyofanyika kwa mali zilizokuwa zinamilikiwa na Madhehebu ya Kikristo.
 
Kwa uelewa wangu hizo mali za Waisilamu kwa kipindi hicho hazikutakiwa kupelekwa BAKWATA kwa kuwa BAKWATA sio Serikali. Ilitakiwa zibinafsishwe na zirudishwe Serikalini kama ilivyofanyika kwa mali zilizokuwa zinamilikiwa na Madhehebu ya Kikristo.
Mawe...
Ilikuwapo sheria kuwa mali zinauzwa na kinachopatika kinagawiwa wanachama.

Serikali haikuweza kufanya hili hivyo ikatungwa sheria kuwa mali za EAMWS zikabidhiwe BAKWATA.
 
SIKU MOJA NA SHEIKH PONDA MAHAKAMANI MOROGORO

Miaka saba iliyopita siku kama ya leo.

Siku nyingi zilikuwa zimepita sijamuona Sheikh Ponda si kwa kuwa alikuwa kifungoni mahabusi bali nilikuwa nje ya Dar es Salaam kwa muda mrefu.

Nikaamua kwenda kumuona mahakamani Morogoro kesi yake ilipokuwa inasikilizwa.

Nikapanda basi la kwanza ili niwahi mahakamani Morogoro.

Kufikia mahakamani nikakuta ulinzi mkali kupita kawaida na kisa ni kuwa kabla sijafika Waislam walikuwa wametiana misukosuko na polisi nje ya jengo la mahakama.

Kwa ajili hii polisi wakawa wamewazuia Waislam kuingia mahakamani.

Baadhi ya watu wanaonifahamu kuniona nimefika pale wakanifuata kunisalimia na kunifahamisha yaliyotokea pale punde wakisikitika kuwa nimekuja kutoka mbali lakini sitaweza kusalimiana na Sheikh Ponda.

Hata hivyo wakanishauri kwenda pale getini nizungumze na askari huenda akaniruhusu kuingia mahakamani kusikiliza kesi na kupata nafasi ya kuonana na Sheikh Ponda.

Baada ya kunisaili yule askari akaniruhusu kupita akiniambia kuwa amefanya staha ya umri wangu na kuwa ni ndugu yake sheikh na nimekuja kutoka mbali.

Mahakamani nilimkuta Mzee Bilal Rehani Waikela katoka Tabora kaja Morogoro kusikiliza kesi ya Sheikh Ponda.

Ilikuwa hapo Morogoro miaka mitatun iliyopita asubuhi najitayarisha kwenda studio za Radio Imaan kufanya kipindi ndipo niliposikia katika taarifa ya habari kuwa Sheikh Ponda amekwenda kwenye kiwanja cha iliyokuwa EAMWS kiwanja palipokusudiwa kujengwa Chuo Kikuu Cha Waislam mwaka wa 1968 na amechukua sehemu ndogo kurejesha kwa Waislam na patajengwa msikiti utakaoitwa Masjid Sheikh Hassan bin Ameir.

Yaliyomfika Sheikh Ponda yanafahamika.

Kumuona Mzee Waikela ndani ya mahakama na Sheikh Ponda kasimama kizimbani machozi yalinilengalenga.

Machozi yalinitoka kwa kuwa nilikuwa naijua nafasi ya Mzee Waikela na Sheikh Hassan bin Ameir katika historia ya Tanganyika.

Miaka mingi imepita toka watu hawa walipokuwa pamoja kama viongozi wa Waislam katika EAMWS.

Lakini niliingiwa na simanzi na kumuonea wivu Sheikh Ponda kuwa leo jina lake linatajwa pamoja na jina la Sheikh Hassan bin Ameir na mwanafunzi wa Sheikh Hassan bin Ameir, Mzee Waikela yuko mahakamani kusikiliza kesi yake.

Sheikh Ponda aliposhinda kesi zote alinialika kwenye shule ambayo yeye ni kiongozi, Ilala Islamic nimzungumze na vijana kuhusu mchango wa Sheikh Hassan bin Ameir katika elimu na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sheikh Ponda ana historia kubwa sana
Naamini iko siku In Shaa Allah atanyanyua kalamu kuiandika.

View attachment 2069458
Kulia ni Wakili Msomi Juma Nassor na Sheikh Ponda Mahakamani Morogoro

View attachment 2069462
Kushoto wa kwanza ni Mzee Bilal Rehani Waikela akiwa mahakamani Morogoro
Pole sana Mzee naona ukiwa jirani kabisa na Mzee Waikela
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom