Siku mabeberu wakichoka kumvumilia kiongozi wa malaika ndiyo mtajua dunia ina wenyewe

RTI

JF-Expert Member
Dec 20, 2018
2,423
7,124
Siku hizi kumezuka tabia ya wafuasi wa kiongozi mtarajiwa wa malaika kuwatuhumu watu wanao mkosoa kiongozi huyo ya kwamba wanatumwa na mabeberu kumhujumu.

Mimi huwa ninacheka sana kuona mfuasi wa kiongozi huyo wa malaika anasema kwa kujiamini eti mabeberu hawaitakii mema nchi yetu. Hivi ngoja niwaulize nyinyi wafuasi wa kiongozi wa malaika mtarajiwa.

Hivi siku mabeberu wakiamuwa kumhujumu kweli kama mnavyodai, kiongozi huyo atakuwa na ubavu kweli wa kukabiliana na hujuma hizo?

Hivi siku mabeberu wakiamua kuiadhibu nchi yetu tutakuwa na ubavu wa kukabiliana nao? Au mnashinda humu mnaongea ili kujifurahisha?

Ngoja sasa niwaambie, nguvu ya mabeberu ni kubwa mno na hatuna uwezo wa kukabiliana nao hata kidogo. Mabeberu wakiamua wana uwezo wa kuigeuza pesa yetu kuwa makaratasi yasiyo kuwa na thamani, yaani unaweza kuwa na milioni mia ndani lakini hiyo hela haina uwezo hata wakununulia mkate watoto wako wale.

Wana uwezo wa kuwafanya muishi gizani na msisafiri kwa kuzuia mafuta kuingia nchini. Wana uwezo wa kuzuia dawa za mahosipitalini mkafa kama wadudu. Yaani wanauwezo wa kuyafanya maisha ya baadhi ya mataifa kuwa magumu na yasiyovumilika.

Kwa hiyo, muachage kushabikia mambo msioyajua ili kumfurahisha kiongozi wa malaika, hao mnao sema ni maadui zenu siku wakiamua kuwa maadui zenu ndiyo mtajua dunia ina wenyewe na hao mnaowaabudu na kuwasifu hata wakifanya maovu ni takataka.
 
Tanzania sio Zimbabwe Mkuu, Tanzania ina utamaduni wa ndani hakuna mwenye uwezo wa kuingilia siasa zetu. Wapinzani walikuwa wanamtumia yule mama aliyekaimu Ubalozi wa USA nchini kujipa matumaini hewa. Kumbe bwana mkubwa Trump hata hamjui huyo Balozi aliyekaimu, wala hana muda na siasa za Tanzania.

Trump ana muda na biashara tunayofanya ya kununua midege tu.

Siasa zetu zinaishia humu humu
Jipe moyo tu... mtaenda kununua mkate huku mmebeba hela ya kutoshs mkate mmoja kwenye kiroba
 
Tanzania sio Zimbabwe Mkuu, Tanzania ina utamaduni wa ndani hakuna mwenye uwezo wa kuingilia siasa zetu

Wapinzani walikuwa wanamtumia yule mama aliyekaimu Ubalozi wa USA nchini kujipa matumaini hewa

Kumbe Bwana mkubwa Trump hata hamjui Huyo balozi aliyekaimu wala hana muda na siasa za Tanzania

Trump ana muda na biashara tunayofanya ya kununua Midege tu

Siasa zetu zinaishia humu humu
Kwani anayeitwa beberu na wapenzi wa kiongozi wa malaika ni Trump pekee?
 
Hahaha nani sasa hakuna mwingine mwenye maslahi na Tanzania
Uingereza alishaacha mambo ya kuingilia siasa za ndani anaangaika na Brexit. Juzi Chancellor Angela Merkel alimpigia simu kumpongeza Mzalendo Magufuli. Ufaransa wala haiijui Tz, kwahiyo jiandaeni kisaikolojia tu, hamna chenu.
Kwani anayeitwa beberu na wapenzi wa kiongozi wa malaika ni Trump pekee?
 
Hahaha Mabeberu yalimshindwa kumtoa dhaifu nkurunzinza wa Burundi

Ndio waje wagusa kwa Tanzania

Tanzania ina utamaduni wa ndani hakuna mwenye uwezo wa kuingilia siasa zetu


Vibaraka wa Mabeberu mtaongea kila lugha
Kwa hiyo wakiamuwa kumtoa wanashindwa?
 
Hahaha nani sasa hakuna mwingine mwenye maslahi na Tanzania
Uingereza alishaacha mambo ya kuingilia siasa za ndani anaangaika na Brexit

Juzi chancellor Angela Merkel alimpigia simu kumpongeza Mzalendo Magufuli

Ufaransa wala haijui Tz

Kwahiyo jiandaeni kisaikolojia tu,hamna chenu
Hizo ndizo akili zenu lakini siku wakimchoka ndio mtajua huyo mnao muabudu kama mungu wenu si chochote mbele ya hao watu.
 
Wewe
Hahaha Mabeberu yalimshindwa kumtoa dhaifu nkurunzinza wa Burundi, ndiyo waje kugusa kwa Tanzania?
Tanzania ina utamaduni wa ndani hakuna mwenye uwezo wa kuingilia siasa zetu.

Vibaraka wa Mabeberu mtaongea kila lugha.
Uwezo wako wa kuelewa mambo ni mdogo sana kulingana na hoja iliyopo mezani siyo kila mada uchangie unajidhalilisha pamoja hao wanao kulipa.
 
Siku hizi kumezuka tabia ya wafuasi wa kiongozi mtarajiwa wa malaika kuwatuhumu watu wanao mkosoa kiongozi huyo ya kwamba wana tumwa na mabeberu kumhujumu.

Mimi huwa ninacheka sana kuona mfuasi wa kiongozi huyo wa malaika anasema kwa kujiamini eti mabeberu hawaitakii mema nchi yetu. Hivi ngoja niwaulize nyinyi wafuasi wa kiongozi wa malaika mtarajiwa.

Hivi siku mabeberu wakiamuwa kumhujumu kweli kama mnavyodai, kiongozi huyo atakuwa na ubavu kweli wa kukabiliana na hujuma hizo?

Hivi siku mabeberu wakiamua kuiadhibu nchi yetu tutakuwa na ubavu wa kukabiliana nao? Au mnashinda humu mnaongea ili kujifurahisha?

Ngoja sasa niwaambie, nguvu ya mabeberu ni kubwa mno na hatuna uwezo wa kukabiliana nao hata kidogo. Mabeberu wakiamua wana uwezo wa kuigeuza pesa yetu kuwa makaratasi yasiyo kuwa na thamani, yaani unaweza kuwa na milioni mia ndani lakini hiyo hela haina uwezo hata wakununulia mkate watoto wako wale.

Wana uwezo wa kuwafanya muishi gizani na msisafiri kwa kuzuia mafuta kuingia nchini. Wana uwezo wa kuzuia dawa za mahosipitalini mkafa kama wadudu. Yaani wanauwezo wa kuyafanya maisha ya baadhi ya mataifa kuwa magumu na yasio vumilika.

Kwa hiyo muachage kushabikia mambo msioyajua ili kumfurahisha kiongozi wa malaika, hao mnao sema ni maadui zenu siku wakiamua kuwa maadui zenu ndiyo mtajua dunia ina wenyewe na hao mnaowaabudu na kuwasifu hata wakifanya maovu ni takataka.
Kamtishie mkeo nyumbani kwako.
 
Back
Top Bottom