Natafuta matibabu
JF-Expert Member
- Aug 1, 2020
- 262
- 301
Baada ya kumaliza masomo yangu ya chuo miaka 3 iliyopita, nilibahatika kwenda kufanya mafunzo kwa vitendo kwenye taasisi moja.
Wakati wa hayo mafunzo nilizoeana vyema na watumishi wa pale hasa wale wa kwenye Idara niliyokuwamo. Ukaribu, maelewano, ushirikiano katika kazi ulikuwa ni wa kushibana, ulikuwa kama familia.
Baada ya muda wangu wa mafunzo kwa vitendo kukamilika niliondoka kuingia mtaani, kusaka ajira. Kama tulivyokuwa tunajua utawala wa awamu ya 5 na ajira ulivyo, nilibatizwa kwa moto mtaani. Nilikiona cha mtema kuni.
Kuna siku nilipata wasaa wa kuitembelea hiyo taasisi niliyofanyia mafunzo, nilifika hadi kuwajulia hali wana Idara kwenye Idara niliyokuwemo kipindi cha mafunzo. Ilikuwa ni furaha kwangu na kwao kuonana tena baada ya kuachana kwa muda mrefu.
Katika kupiga stori mimi nikiwa nawauliza jinsi wanavyoendelea na kazi, swali lao kwangu ambalo kila mmoja wao anashauku ya kutaka kujua jibu ni "Siku hizi uko wapi?'' Hapa wakiwa wanamaanisha nafanya kazi wapi baada ya kumaliza mafunzo, kwa kuwa sina kazi naendelea kupambana huwa nakereheka sana nikiulizwa hizi swali. Naishia kuwajibu nipo tu mtaani, ila hawaamini wanadhani huenda nina kazi/kuajiriwa sehemu ambapo wanapenda kuifahamu.
Hongera Mama katika awamu yako ya Sita, bila shaka nitaweza kupata jibu la swali langu hili linalonikosesha amani. Kikubwa naomba Mungu haki itendeke huko kwenye mamlaka husika maana figisu huwa hazikosekani
__________________
UPDATES: 2023.
Tayari nishakuwa mtumishi wa Umma, jibu la swali "Siku hizi uko wapi?" lishapatikana.
Asanteni wote mlionitia moyo humu.
Wakati wa hayo mafunzo nilizoeana vyema na watumishi wa pale hasa wale wa kwenye Idara niliyokuwamo. Ukaribu, maelewano, ushirikiano katika kazi ulikuwa ni wa kushibana, ulikuwa kama familia.
Baada ya muda wangu wa mafunzo kwa vitendo kukamilika niliondoka kuingia mtaani, kusaka ajira. Kama tulivyokuwa tunajua utawala wa awamu ya 5 na ajira ulivyo, nilibatizwa kwa moto mtaani. Nilikiona cha mtema kuni.
Kuna siku nilipata wasaa wa kuitembelea hiyo taasisi niliyofanyia mafunzo, nilifika hadi kuwajulia hali wana Idara kwenye Idara niliyokuwemo kipindi cha mafunzo. Ilikuwa ni furaha kwangu na kwao kuonana tena baada ya kuachana kwa muda mrefu.
Katika kupiga stori mimi nikiwa nawauliza jinsi wanavyoendelea na kazi, swali lao kwangu ambalo kila mmoja wao anashauku ya kutaka kujua jibu ni "Siku hizi uko wapi?'' Hapa wakiwa wanamaanisha nafanya kazi wapi baada ya kumaliza mafunzo, kwa kuwa sina kazi naendelea kupambana huwa nakereheka sana nikiulizwa hizi swali. Naishia kuwajibu nipo tu mtaani, ila hawaamini wanadhani huenda nina kazi/kuajiriwa sehemu ambapo wanapenda kuifahamu.
Hongera Mama katika awamu yako ya Sita, bila shaka nitaweza kupata jibu la swali langu hili linalonikosesha amani. Kikubwa naomba Mungu haki itendeke huko kwenye mamlaka husika maana figisu huwa hazikosekani
__________________
UPDATES: 2023.
Tayari nishakuwa mtumishi wa Umma, jibu la swali "Siku hizi uko wapi?" lishapatikana.
Asanteni wote mlionitia moyo humu.