Siku Freeman Mbowe akaamua kujiengua CHADEMA, je wabunge wa viti maalum wataendelea kubaki ndani ya chama hicho?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,367
Wadau, amani iwe kwenu.

Katika viongozi wa kisiasa waliofanikiwa kugroom wanasiasa vijana wa kike basi ni huyu Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikael Mbowe. Ni Mbowe ndiye aliyemuibua Halima James Mdee kusikojulikana. Ni Mbowe ndiye aliyefanikiwa kumfanya Joyce Mukya kuwa mbunge wa viti maalum kwa awamu mbili mfululizo. Ni Freeman Mbowe ndiye aliyemfanya Esther Matiko akakubalika na kung'ara kisiasa.

Namkumbuka sana FAREEMAN MBOWE alivyomtengeneza Jesca Kishoa hadi kuwa mhimili mkubwa kisiasa. Hata ndoa ya Kafulila na Kishoa iligharamiwa kwa kiasi kikubwa na Mbowe ili kumfanya mwanasiasa huyo awe na utulivu wa kisiasa. Mnakumbuka ujio wa Bulaya CCM? Ni nani aliyefanikisha kama si Mdee na Mbowe?

Madam Wema Sepetu nusura aukwae ubunge wa viti maalum. ilikuwa ni jitihada zake ili kuhakikisha CHADEMA inakuwa na wabunge vijana wenye mvuto katika jamii. Majadiliano yalikuwa yanaendelea baina ya Mbowe na Mange Kimambi ili 2020 autwae ubunge wa viti maalum.

Mpaka hapo naamini tunakubaliana kuwa wabunge wengi wa viti maalum na hata wa kiume kama akina John Mnyika ni uzao wa Freeman Mbowe. Siku Mbowe akaamua kujiengua kwenye chama hicho au hata kuwa nje tu ya uongozi wa CHADEMA, yupo mbunge wa viti Maalum atakuwa na ujasiri wa kubaki? Kama yupo basi nitajieni nimtunuku nishani ya ushujaa.

Nawasilisha
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Katika viongozi wa kisiasa waliofanikiwa kugroom wanasiasa vijana wa kike basi ni huyu Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikael Mbowe. Ni Mbowe ndiye aliyemuibua Halima James Mdee kusikojulikana. Ni Mbowe ndiye aliyefanikiwa kumfanya Joyce Mukya kuwa mbunge wa viti maalum kwa awamu mbili mfululizo. Ni Freeman Mbowe ndiye aliyemfanya Esther Matiko akakubalika na kung'ara kisiasa.

Namkumbuka sana FAREEMAN MBOWE alivyomtengeneza Jesca Kishoa hadi kuwa mhimili mkubwa kisiasa. Hata ndoa ya Kafulila na Kishoa iligharamiwa kwa kiasi kikubwa na Mbowe ili kumfanya mwanasiasa huyo awe na utulivu wa kisiasa. Mnakumbuka ujio wa Bulaya CCM? Ni nani aliyefanikisha kama si Mdee na Mbowe?

Madam Wema Sepetu nusura aukwae ubunge wa viti maalum. ilikuwa ni jitihada zake ili kuhakikisha CHADEMA inakuwa na wabunge vijana wenye mvuto katika jamii. Majadiliano yalikuwa yanaendelea baina ya Mbowe na Mange Kimambi ili 2020 autwae ubunge wa viti maalum.

Mpaka hapo naamini tunakubaliana kuwa wabunge wengi wa viti maalum na hata wa kiume kama akina John Mnyika ni uzao wa Freeman Mbowe. Siku Mbowe akaamua kujiengua kwenye chama hicho au hata kuwa nje tu ya uongozi wa CHADEMA, yupo mbunge wa viti Maalum atakuwa na ujasiri wa kubaki? Kama yupo basi nitajieni nimtunuku nishani ya ushujaa.

Nawasilisha


Bora hao ni Wanawake lkn Wanaume wote waliokuwa chadema pia watamfwata aendako, sijui huwa anawafanya nini hawa watu!
 
Mbowe yuko chadema kimaslahi si rahisi kujiengua! Anapata mshahara na marupurupu ya ubunge na ruzuku yote ya chama ni hela nyingi sana hiyo. Akitoka huko ataikosa
 
Mbowe yuko chadema kimaslahi si rahisi kujiengua! Anapata mshahara na marupurupu ya ubunge na ruzuku yote ya chama ni hela nyingi sana hiyo. Akitoka huko ataikosa
Nilikuwa nawaza tu kwa mapana. Najua wazi kuwa hawezi kutoka CHADEMA japo kwenye siasa kila kitu kinawezekana
 
Mkuu, mbona matusi sana? Nini kimekutokea siku hizi?
Acha ujinga wewe, umekalia kupagawa kwa kuangalia Avatar ya ShushushuVip.

Namna hivyo ndivyo mnavyojenga Viwanda ambapo kiwanda kidogo ni vyerehani 4.
 
Acha ujinga wewe, umekalia kupagawa kwa kuangalia Avatar ya ShushushuVip.

Namna hivyo ndivyo mnavyojenga Viwanda ambapo kiwanda kidogo ni vyerehani 4.
Kamanda, pamoja na ukamanda wa FREEMAN MBOWE, alilegea kwa Madam Wema Sepetu
 
Ondoa ramli zako hapa. Sasa unatuuliza sisi tufanyeje? Huna cha kuandika leo? Kaa kimya.
 
Najaribu kuwaza tu kamanda. kama unaona nimekukwaza nisamehe kamanda wangu
Tatizo unawaza kwa chura ndio maana unaposti upumbavu tu.

Badala ya kutumia akili kufikiria namna gani mtajenga viwanda wewe umekalia ujinga na upopoma hapa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom