Mallia
JF-Expert Member
- Jan 31, 2018
- 437
- 1,530
Niko Magomeni hapa mwenye macho haambiwi ona kuwa huu mradi kwa sasa umelemewa na sio salama tena kwa afya za watu na usalama wao pia.
Gari 100 haziwezi kuwamudu watu wote wa Dar es salaam ambao wanatumia usafiri huu , magari yamechakaa na yanajaza watu kupitiliza kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa watu, huu mradi unatakiwa uwe na basi mpya haraka iwezekanavyo au ziruhusiwe daladala pembeni ziokoe jahazi.
Madereva wanafanya kazi kwa mazoea na hasira badala ya ukarimu na weledi yaani ni kama wanagawa lifti vile watu wanagombania dereva anafunga mlango kwa makusudi watu wanabanwa milangoni.
Huu mradi kama umewashinda wekeni daladala pembeni msiwape wananchi shida, msitake hadi siku gari lilipuke watu wafe ndio muanze kuchukua Tahadari hii hali sio nzuri.
Gari 100 haziwezi kuwamudu watu wote wa Dar es salaam ambao wanatumia usafiri huu , magari yamechakaa na yanajaza watu kupitiliza kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa watu, huu mradi unatakiwa uwe na basi mpya haraka iwezekanavyo au ziruhusiwe daladala pembeni ziokoe jahazi.
Madereva wanafanya kazi kwa mazoea na hasira badala ya ukarimu na weledi yaani ni kama wanagawa lifti vile watu wanagombania dereva anafunga mlango kwa makusudi watu wanabanwa milangoni.
Huu mradi kama umewashinda wekeni daladala pembeni msiwape wananchi shida, msitake hadi siku gari lilipuke watu wafe ndio muanze kuchukua Tahadari hii hali sio nzuri.