Siku ambayo CCM wataumbuka

the ultimatum

JF-Expert Member
Dec 16, 2012
401
104
Ni matarajio ya wana CCM wote kuona CHADEMA inasambaratika. Mbinu nyingi sana zinatumika na ambazo zimekwishatumika ili kuisambaratisha CHADEMA. Mbinu nyingi ambazo zimetumika CHADEMA wameweza kuzibaini na kusonga mbele kitu ambacho kilitia na kinaendelea kutilia shaka mipango ovu inayofanywa na CCM dhidi ya CHADEMA.

Suala la kuvuliwa uongozi kwa Zitto na wenzake katika chama ni kete nyingine na ambayo ni ya juu kabisa kwa wana CCM ya kujaribu kuitumia ili kuisamabaratisha CHADEMA.

Kinachotokea ni kwamba kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015 kuna hatari kubwa sana ya kutokea mpasuko wa makundi ya urais ndani ya CCM hivyo kuicha CHADEMA iende kwenye uchaguzi mkuu kwa nguvu na kasi hii kunahatari kubwa sana ya CHADEMA kuchukua dola.

Kinachonifanya niamini kuwa ipo siku wana CCM wataumbuka ni kwamba; kwakuwa wao wanaamini kwa suala la Zitto CHADEMA imeshajichimbia kaburi, na kwakuwa tumeshaona jitihada kadha wa kadha zinazofanya na baadhi ya makada waliowahi kutimuliwa CHADEMA katika kuuaminisha umma kuwa maamuzi ya kamati kuu ya kuwavua uongozi Zitto na wenzake hayakuwa sahihi na kwakuwa kuna kila dalili za kuamini kuwa watu hawa wanatumiwa na CCM ili kutimiza malengo yao ya kuisambaratisha CHADEMA, siku ambayo wataumbuka ni kama ifuatavyo.

Ni siku ambayo aidha Zitto hatavuliwa uanachama na kamati kuu labda kutokana na utetezi wake aliotakiwa auwasilishe ndani ya siku 14 yeye pamoja na wenzake. Ni siku ambayo Zitto atakili pamoja na mapungufu ya kibinadamu kuwa mikakati ambayo walikuwa wakiifanya haikuwa na nia ya kuleta umoja wa kichama bali kudhoofisha. Ni siku ambayo kiongozi Zitto Zuberi kabwe pamoja na kutambua umuhimu wa kuiondosha CCM madarakani kwa wakati huu wenye uhitaji mkubwa kwa watanzania, akaamua kuungana kwa nguvu zote kwenye M4C ya chama, ikiwa ni pamaoja na kufanya mikutano mikubwa ya pamoja na viongozi wote wa chama akiwemo Mbowe, Slaa na wengine katika ukanda ambapo Zitto ametokea na maeneo mengine kote nchini.


Hakika kama hili hilatatokea litakuwa ni pigo kubwa sana kwa CCM na vibaraka wake na kiama cha CCM kitakuwa kimetimia.
 
Zitto huyu aliejaa kiburi na majivuno aombe radhi? Haitakaa itokee. Ambaye anaona ni sawa tu CDM ife lakini awe wa mwisho. Anaeshangiliwa na magamba? Hawezi kuwaangusha magamba, hawezi kuwaudhi, ni heriawaudhi wanaCDM wenzie kuliko maCCM, hawezi kuwasaliti magamba na kumfaidisha Slaa na Mbowe.
 
Kiburi alichonacho zito ir kusema ukweli ndo kiburi mmataka chama kiwe mradi wawatu wachache
 
Zitto huyu aliejaa kiburi na majivuno aombe radhi? Haitakaa itokee. Ambaye anaona ni sawa tu CDM ife lakini awe wa mwisho. Anaeshangiliwa na magamba? Hawezi kuwaangusha magamba, hawezi kuwaudhi, ni heriawaudhi wanaCDM wenzie kuliko maCCM, hawezi kuwasaliti magamba na kumfaidisha Slaa na Mbowe.

Zitto ni kiongozi mahili, naamini ataangalia namna bora ya kufanya kama anajali mustakbari mwema wa Tanzania na watanzania
 
CHADEMA hii hii ya sasa isiyoweza kutatua matatizo yao ya ndani kati ya wabunge wake less 25 wa kuchaguliwa ipewe dola?!!!!....Hell NO..hiyo haitatokea!!!

This country will be running on it's own bullshit
 
Zitto ndio basi tena. maccm weshamuharibia tayari, atafute chuo cha kufundisha, wajitokeze wafadhili wampatie majuzuu kazi ianze mara moja.
 
CHADEMA hii hii ya sasa isiyoweza kutatua matatizo yao ya ndani kati ya wabunge wake less 25 wa kuchaguliwa ipewe dola?!!!!....Hell NO..hiyo haitatokea!!!

This country will be running on it's own bullshit

Kwa sababu wewe ndiye mpiga kura pekee hapa Tanzania, hebu ongea vitu vyenye afya banaa!
 
Kwa sababu wewe ndiye mpiga kura pekee hapa Tanzania, hebu ongea vitu vyenye afya banaa!

mkuu napenda ccm itoke hata leo
lakini kwa mwendo wa CDM kwa sasa sijui...kuna watu ndani yake wanaanza kugeuzac hama kuwa viongozi na si wananchi. Na hapo ndipo panaanza kuleta mashaka....kale ka tabia ka Mzee Lyatonga Mrema ktk nccr na tlp ndiko kameanza kuchipuka.

Viongozi waliomo wameanz akujisahau na wanajiona ni ma Master perfect....jambo ambalo ni hatari.
 
mkuu napenda ccm itoke hata leo
lakini kwa mwendo wa CDM kwa sasa sijui...kuna watu ndani yake wanaanza kugeuzac hama kuwa viongozi na si wananchi. Na hapo ndipo panaanza kuleta mashaka....kale ka tabia ka Mzee Lyatonga Mrema ktk nccr na tlp ndiko kameanza kuchipuka.

Viongozi waliomo wameanz akujisahau na wanajiona ni ma Master perfect....jambo ambalo ni hatari.

Siasa ni pamoja na kupata massive support. Watu ndio wanaopiga kura, ni vema kujiuliza katika hilo Chadema wamefanikiwa kwa kiwango gani?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom