Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,857
- 30,205
SIKU AISHA ''DAISY'' SYKES ALIPOFUATANA NA BABA YAKE MSASANI KWA MWALIMU NYERERE KUHUSU HISTORIA YA TANU 1968
Hakika wengi wangependa kama historia hii niliyoandika isingekuwa kweli na watu hawa niliowarejesha kwenye historia ya Mwalimu Nyerere, TANU na uhuru wa Tanganyika baada ya kufutwa wangekuwa hawakuwapo bali ni hadithi ya mtunga hadithi hodari.
Lakini watu hawa walikuwapo na wanafahamika na mmoja wa watu hawa ni babu yangu, Salum Abdallah ambae nimeeleza historia yake kwa ushahidi wa historia yenyewe na picha.
Daisy ameeleza historia ya baba yake wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika na katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake aliandika makala ambayo mimi nimeiandikia utangulizi.
Nakuwekea kipande cha makala hiyo na utangulizi wangu kukudhihirishia kuwa haya nikwaambiayo ni kweli:
Utangulizi
Aisha ‘’Daisy’’ Sykes Buruku ni binti ya Abdulwahid Sykes mmoja kati ya wazalendo 17 waliounda chama cha TANU kilichopigania uhuru wa Tanganyika.
Daisy kama anavyofahamika zaidi kwa jina hili, ni msichana wa kwanza Mwafrika kusoma Shule ya Wasichana ya Aga Khan mwanzoni mwa miaka ya 1950 na msichana wa pili kuingia Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki, Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 1960.
Daisy amefahamiana na wazalendo wengi mmoja wapo akiwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na machifu mashuhuri kama Mangi Mkuu Thomas Marealle waliokuwa wakifika nyumbani kwa baba yake wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
Katika kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha baba yake, Daisy ameandika makala haya kukumbuka siku zile zilizojenga haiba ya baba yake na ya wazalendo walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Kwa miaka mingi Daisy amekuwa akiishi na kufanya kazi nje ya Tanzania:
BABA YANGU ABDULWAHID SYKES KAMA NINAVYOMKUMBUKA
Na Daisy Sykes Buruku
''Juma moja kabla ya kifo chake nilimuuliza baba swali ambalo jibu alilijua lakini katika hulka yake ya kawaida ya kutopenda kujikweza hakutaka achukue sifa zote kwa ule ukweli na matokeo yake.
Wakati ule nilikuwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki Dar- es- Salaam na mwalimu wangu wa Historia Dr. John Iliffe kwa kutambua kuwa natoka familia ya Sykes waasisi wa mwamko wa siasa katika Tanganyika na mchango wa wazee wangu katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika alinitaka niandike mafanikio ya Watanganyika wa kizazi kile pamoja na historia ya babu yangu Abdallah Kleist Sykes.
Dk. John Iliffe alinitia moyo nifanye utafiti na kuandika historia hii na nilikubali kufanya hivyo.
Nilikuwa na swali kuhusu nani khasa walikuwapo katika mkutano na kushiriki wa kuibadili TAA kuwa TANU.
Baba akashauri kuwa tuombe miadi na Rais wa Tanzania Mwalimu Nyerere ili anipe ukweli niliokuwa nautafuta na kusadikisha mambo mengine yanayohusiana na historia hiyo.
Hivyo tukaenda Msasani kuonana na Mwalimu Jumamosi moja asubuhi.
Kama ilivyotegemewa Mwalimu alifurahi sana kutuona maana ilikuwa muda mrefu watu hawa waliokuwa marafiki wakubwa sana kupata kuonana.
Mwalimu alitoa ushirikiano mkubwa sana kwangu kupata ukweli kutoka kwake katika yale niliyotaka kujua kutoka kwake.
Hii ndiyo ilikuwa siku yao ya mwisho kuonana.''
Picha 1. Daisy Sykes Buruku
2. Waasisi wa TANU 1954
3. John Iliffe
Hakika wengi wangependa kama historia hii niliyoandika isingekuwa kweli na watu hawa niliowarejesha kwenye historia ya Mwalimu Nyerere, TANU na uhuru wa Tanganyika baada ya kufutwa wangekuwa hawakuwapo bali ni hadithi ya mtunga hadithi hodari.
Lakini watu hawa walikuwapo na wanafahamika na mmoja wa watu hawa ni babu yangu, Salum Abdallah ambae nimeeleza historia yake kwa ushahidi wa historia yenyewe na picha.
Daisy ameeleza historia ya baba yake wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika na katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake aliandika makala ambayo mimi nimeiandikia utangulizi.
Nakuwekea kipande cha makala hiyo na utangulizi wangu kukudhihirishia kuwa haya nikwaambiayo ni kweli:
Utangulizi
Aisha ‘’Daisy’’ Sykes Buruku ni binti ya Abdulwahid Sykes mmoja kati ya wazalendo 17 waliounda chama cha TANU kilichopigania uhuru wa Tanganyika.
Daisy kama anavyofahamika zaidi kwa jina hili, ni msichana wa kwanza Mwafrika kusoma Shule ya Wasichana ya Aga Khan mwanzoni mwa miaka ya 1950 na msichana wa pili kuingia Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki, Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 1960.
Daisy amefahamiana na wazalendo wengi mmoja wapo akiwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na machifu mashuhuri kama Mangi Mkuu Thomas Marealle waliokuwa wakifika nyumbani kwa baba yake wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
Katika kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha baba yake, Daisy ameandika makala haya kukumbuka siku zile zilizojenga haiba ya baba yake na ya wazalendo walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Kwa miaka mingi Daisy amekuwa akiishi na kufanya kazi nje ya Tanzania:
BABA YANGU ABDULWAHID SYKES KAMA NINAVYOMKUMBUKA
Na Daisy Sykes Buruku
''Juma moja kabla ya kifo chake nilimuuliza baba swali ambalo jibu alilijua lakini katika hulka yake ya kawaida ya kutopenda kujikweza hakutaka achukue sifa zote kwa ule ukweli na matokeo yake.
Wakati ule nilikuwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki Dar- es- Salaam na mwalimu wangu wa Historia Dr. John Iliffe kwa kutambua kuwa natoka familia ya Sykes waasisi wa mwamko wa siasa katika Tanganyika na mchango wa wazee wangu katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika alinitaka niandike mafanikio ya Watanganyika wa kizazi kile pamoja na historia ya babu yangu Abdallah Kleist Sykes.
Dk. John Iliffe alinitia moyo nifanye utafiti na kuandika historia hii na nilikubali kufanya hivyo.
Nilikuwa na swali kuhusu nani khasa walikuwapo katika mkutano na kushiriki wa kuibadili TAA kuwa TANU.
Baba akashauri kuwa tuombe miadi na Rais wa Tanzania Mwalimu Nyerere ili anipe ukweli niliokuwa nautafuta na kusadikisha mambo mengine yanayohusiana na historia hiyo.
Hivyo tukaenda Msasani kuonana na Mwalimu Jumamosi moja asubuhi.
Kama ilivyotegemewa Mwalimu alifurahi sana kutuona maana ilikuwa muda mrefu watu hawa waliokuwa marafiki wakubwa sana kupata kuonana.
Mwalimu alitoa ushirikiano mkubwa sana kwangu kupata ukweli kutoka kwake katika yale niliyotaka kujua kutoka kwake.
Hii ndiyo ilikuwa siku yao ya mwisho kuonana.''
Picha 1. Daisy Sykes Buruku
2. Waasisi wa TANU 1954
3. John Iliffe