Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Mkapa, rais wa kwanza wa Tanzania kuchaguliwa katika mfumo wa vyama vingi, ameandika hayo katika kitabu chake cha “My Life, My Purpose (Maisha Yangu, Kusudi Langu)” ambacho kinazungumzia matukio na maamuzi aliyofanya katika utawala wake wa kuanzia mwaka 1995 hadi 2005, akijutia na kukubali kubeba lawama zote kwa baadhi ya matukio, huku akieleza somo alilopata.
Mkapa amesema ili kuwa na usawa katika mfumo wa vyama vingi nchini, ni muhimu kuwa na chombo huru kilichojumuisha vyama vyote.
“Kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi itakayokubalika na Vyama vyote vya Siasa ndio chachu ya kulea na kukuza demokrasia nchini,” anasema Mkapa, ambaye anasema alipata funzo kubwa la umuhimu wa kushirikiana na vyama vya siasa baada ya mauaji ya wafuasi 22 wa CUF yaliyofanywa na polisi kisiwani Pemba mwaka 2001.
Zaidi soma >Benjamin Mkapa: Natamani kuwe na Tume Huru ya Uchaguzi, Wapinzani wahusishwe kwenye kupiga na kuhesabu kura na kutangazwa mshindi